Isaya
64 Kama tu ungepasua mbingu na kushuka chini,
Ili milima itetemeke kwa sababu yako,
2 Kama vile wakati moto unawasha miti midogo-midogo,
Na moto unafanya maji yatokote,
Basi jina lako lingejulikana kwa wapinzani wako,
Na mataifa yangetetemeka mbele yako!
3 Wakati ulifanya mambo ya kuogopesha yenye hatukupima kutazamia,+
Ulishuka, na milima ilitetemeka mbele yako.+
4 Tangu zamani hakuna mwenye alisikia wala kutega sikio,
Wala hakuna jicho lenye lilimuona Mungu isipokuwa wewe,
Mwenye kutenda kwa ajili ya wale wenye wanaendelea kumungojea.*+
5 Umekutana na wale wenye wanafurahia kutenda mambo yenye kuwa sawa,+
Wale wenye wanakukumbuka na kufuata njia zako.
Angalia! Ulikuwa na kasirani kali, wakati huo sisi tuliendelea kutenda zambi,+
Tulifanya vile kwa wakati murefu.
Je, sasa tuokolewe?
6 Na sisi wote tumekuwa kama mutu mwenye haiko safi,
Na matendo yetu yote ya haki yako kama kipande cha nguo chenye mwanamuke anatumia katika siku zake za kuona mwezi.*+
Sisi wote tutakauka kama jani,
Na makosa yetu yatatupeperusha kama upepo.
8 Lakini sasa, Ee Yehova, uko Baba yetu.+
Tafazali, utuangalie, kwa maana sisi wote tuko watu wako.
10 Miji yako mitakatifu imekuwa jangwa.
Sayuni imekuwa jangwa,
Yerusalemu imekuwa eneo lenye limeachwa.+
11 Nyumba yetu ya* utakatifu na utukufu,*
Kwenye mababu zetu walikusifu,
Imeteketezwa kwa moto,+
Na vitu vyote vyenye tulipenda sana vimeharibiwa.
12 Kwa sababu ya hayo yote, je, bado utajizuia, Ee Yehova?
Je, utaendelea kunyamaza na kuacha tuteseke sana?+