Zaburi
Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+
48 Yehova ni mukubwa na anastahili kabisa kusifiwa
Katika muji wa Mungu wetu, katika mulima wake mutakatifu.
2 Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+
Ni Mulima Sayuni wenye kuwa mbali sana kaskazini,
Muji wa Mufalme Mukubwa.+
4 Kwa maana angalia! wafalme wamekusanyika;*
Wamesonga mbele pamoja.
5 Wakati waliona hilo, walishangaa.
Walishikwa na wasiwasi na kukimbia kwa woga mukubwa.
6 Kutetemeka kuliwashika wakiwa kule,
Uchungu kama wa mwanamuke mwenye kuzaa.
7 Kwa upepo wa mashariki unavunja-vunja mashua* za Tarshishi.
8 Mambo yenye tulisikia, tumejionea sasa sisi wenyewe
Katika muji wa Yehova wa majeshi, katika muji wa Mungu wetu.
Mungu ataufanya kuwa imara kabisa milele.+ (Sela)
10 Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yako
Inafika mupaka kwenye miisho ya dunia.+
Mukono wako wa kuume umejaa haki.+
13 Muweke mioyo yenu juu ya maboma yake.*+
Muchunguze minara yake yenye ngome,
Ili muelezee vizazi vyenye kuja kuhusu muji huo.
14 Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele.