Kumbukumbu la Torati
33 Sasa hii ndiyo baraka yenye Musa mutu wa Mungu wa kweli alitangazia Waisraeli mbele ya kifo chake.+ 2 Alisema:
“Yehova—alikuja kutoka Sinai,+
Na akawaangazia kutoka Seiri.
Aliangaza kwa utukufu kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+
Na alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+
Na wapiganaji-vita wake kwenye mukono wake wa kuume.+
5 Na akakuwa mufalme kule Yeshuruni,*+
Wakati vichwa vya watu walikusanyika pamoja,+
Pamoja na makabila yote ya Israeli.+
7 Na akamutangazia Yuda baraka hii:+
“Ee Yehova, sikia sauti ya Yuda,+
Na umurudishe kwa watu wake.
8 Kuhusu Lawi akasema:+
“Tumimu yako* na Urimu yako+ ni vya mutu mwenye kuwa mushikamanifu kwako,+
Mwenye ulijaribu kule Masa.+
Ulianza kushindana naye karibu na maji ya Meriba,+
9 Mutu mwenye aliambia baba yake na mama yake, ‘Sijawaheshimia.’
Hata ndugu zake hakuwatambua,+
Na alipuuza wana wake mwenyewe.
Kwa maana walitii neno lako,
Na walishika agano lako.+
11 Ee Yehova, bariki nguvu zake,
Na ufurahie kazi ya mikono yake.
Vunja miguu ya* wale wenye wanainuka ili kumupinga,
Ili wale wenye kumuchukia wasiinuke tena.”
12 Kuhusu Benyamini alisema:+
“Muache mupendwa wa Yehova akae kwa usalama pembeni yake;
Wakati anamulinda siku nzima,
Atakaa katikati ya mabega yake.”
13 Kuhusu Yosefu alisema:+
“Inchi yake ibarikiwe na Yehova+
Kwa vitu vya muzuri vya mbinguni,
Kwa umande na maji kutoka katika chemchemi zenye kuwa chini,+
14 Kwa vitu vya muzuri vyenye kuletwa na jua
Na mazao ya muzuri kila mwezi,+
15 Kwa vitu vya muzuri sana kutoka katika milima ya zamani*+
Na vitu vya muzuri kutoka katika vilima vyenye kudumu,
16 Kwa vitu vya muzuri vya dunia na vitu vyenye kuijaza,+
Na kwa kukubaliwa na Ule mwenye kukaa katika muti mudogo wa miiba.+
Na vikuje juu ya kichwa cha Yosefu,
Kwenye sehemu ya juu ya katikati ya kichwa cha ule mwenye alichaguliwa kutoka kati ya ndugu zake.+
17 Utukufu wake ni kama wa muzaliwa wa kwanza wa ngombe-dume,
Na pembe zake ni pembe za ngombe-dume wa pori.
Atayatumia ili kusukuma* vikundi vya watu
Mataifa yote mupaka kwenye miisho ya dunia.
Wao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,+
Nao ni maelfu ya Manase.”
18 Kuhusu Zabuloni alisema:+
“Shangilia, Ee Zabuloni, wakati unatoka inje,
Na wewe, Isakari, katika mahema yako.+
19 Wataita vikundi vya watu viende kwenye mulima.
Kule watatoa zabihu za haki.
20 Kuhusu Gadi alisema:+
“Amebarikiwa ule mwenye anapanua mipaka ya Gadi.+
Analala kule kama simba,
Akiwa tayari kupasua mukono, ndiyo, sehemu ya juu ya katikati ya kichwa.
Vichwa vya watu watakusanyika pamoja.
Haki ya Yehova ataitimiza,
Na maamuzi yake ya hukumu pamoja na Israeli.”
22 Kuhusu Dani alisema:+
“Dani ni mwana-simba.+
Ataruka kutoka Bashani.”+
23 Kuhusu Naftali alisema:+
“Naftali ametosheka kwa sababu ya kukubaliwa
Na amejaa baraka ya Yehova.
Kamata mangaribi na kusini.”
24 Kuhusu Asheri alisema:+
“Asheri amebarikiwa kuwa na wana.
Apendwe na ndugu zake,
Na atumbukize* miguu yake katika mafuta.
26 Hakuna mwenye kuwa kama Mungu wa kweli+ wa Yeshuruni,+
Mwenye anapita katika mbingu ili kukusaidia
Na kupita juu ya mawingu katika utukufu wake.+
28 Israeli atakaa kwa usalama,
Na chemchemi ya Yakobo itatengwa peke yake
Katika inchi ya nafaka na divai mupya,+
Mwenye anga zake zitaangusha matone-matone ya umande.+
29 Wewe ni mwenye furaha, Ee Israeli!+