Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 14
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Wafalme

      • Unabii wa Ahiya juu ya Yeroboamu (1-20)

      • Rehoboamu anatawala juu ya Yuda (21-31)

        • Shishaki anashambulia (25, 26)

1 Wafalme 14:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 11:30, 31

1 Wafalme 14:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

1 Wafalme 14:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 18:1; 1 Sa. 4:3

1 Wafalme 14:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Utamuambia hivi na hivi.”

1 Wafalme 14:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 11:30, 31; 12:20

1 Wafalme 14:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:16
  • +1 Fal. 15:5; Mdo 13:22

1 Wafalme 14:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “sanamu za kuyeyushwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 27:15; 2Nya 11:15
  • +Ne 9:26; Zab 50:17

1 Wafalme 14:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “nitakatilia mbali.”

  • *

    Tnn., “mutu yeyote mwenye kukojoa kwenye ukuta.” Huu ni usemi wa Kiebrania wa kuzarau wenye kumaanisha wanaume.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 15:25-29

1 Wafalme 14:13

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Mkaribie Yehova, uku. 244

    Munara wa Mulinzi,

    1/7/2010, uku. 29

    1/7/2005, uku. 31

1 Wafalme 14:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “atakatilia mbali.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 15:25-29

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Unabii wa Isaya 1, uku. 133-134

1 Wafalme 14:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, Efrati.

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 8:7-9; 29:28; Yosh. 23:15; 2 Fal. 17:6
  • +Kum 28:64; 2 Fal. 15:29; 18:11
  • +Kum 12:3

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Unabii wa Isaya 1, uku. 133-134

1 Wafalme 14:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 12:28-30; 13:33, 34

1 Wafalme 14:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Hapa kizingiti ni ubao wenye kuwa chini ya mulango.

1 Wafalme 14:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 12:15; 13:3

1 Wafalme 14:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “siku za utawala wa Yeroboamu zilikuwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 13:20
  • +1 Fal. 15:25

1 Wafalme 14:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 78:68; 132:13
  • +Kut 20:24; Kum 12:5, 6; 1 Fal. 8:16, 17
  • +1 Fal. 11:1; 2Nya 12:13

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/12/2011, uku. 10

1 Wafalme 14:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 11:7; 2Nya 12:1
  • +Isa 65:2

1 Wafalme 14:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Angalia Maana ya Maneno.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:1
  • +Isa 65:7
  • +Kum 12:2, 3; Isa 57:5; Yer 2:20; Ho 4:13

1 Wafalme 14:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 23:17, 18; 1 Fal. 15:11, 12; 22:46; 2 Fal. 23:7; Ho 4:14

1 Wafalme 14:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 11:40
  • +2Nya 12:2-4

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 295

1 Wafalme 14:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 7:51; 15:18; 2 Fal. 18:14, 15; 24:12, 13
  • +1 Fal. 10:16, 17; 2Nya 12:9-11

1 Wafalme 14:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wakimbiaji.”

1 Wafalme 14:29

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1Nya 27:24; 2Nya 12:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2009, uku. 32

1 Wafalme 14:30

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 15:6

1 Wafalme 14:31

Maelezo ya Chini

  • *

    Anaitwa pia Abiya.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 11:43
  • +1 Fal. 11:1; 2Nya 12:13
  • +1Nya 3:10; Mt 1:7

Maandiko ingine

1 Fa. 14:21 Fal. 11:30, 31
1 Fa. 14:4Yosh. 18:1; 1 Sa. 4:3
1 Fa. 14:71 Fal. 11:30, 31; 12:20
1 Fa. 14:81 Fal. 12:16
1 Fa. 14:81 Fal. 15:5; Mdo 13:22
1 Fa. 14:9Kum 27:15; 2Nya 11:15
1 Fa. 14:9Ne 9:26; Zab 50:17
1 Fa. 14:101 Fal. 15:25-29
1 Fa. 14:141 Fal. 15:25-29
1 Fa. 14:15Kum 8:7-9; 29:28; Yosh. 23:15; 2 Fal. 17:6
1 Fa. 14:15Kum 28:64; 2 Fal. 15:29; 18:11
1 Fa. 14:15Kum 12:3
1 Fa. 14:161 Fal. 12:28-30; 13:33, 34
1 Fa. 14:192Nya 12:15; 13:3
1 Fa. 14:202Nya 13:20
1 Fa. 14:201 Fal. 15:25
1 Fa. 14:21Zab 78:68; 132:13
1 Fa. 14:21Kut 20:24; Kum 12:5, 6; 1 Fal. 8:16, 17
1 Fa. 14:211 Fal. 11:1; 2Nya 12:13
1 Fa. 14:221 Fal. 11:7; 2Nya 12:1
1 Fa. 14:22Isa 65:2
1 Fa. 14:23Law. 26:1
1 Fa. 14:23Isa 65:7
1 Fa. 14:23Kum 12:2, 3; Isa 57:5; Yer 2:20; Ho 4:13
1 Fa. 14:24Kum 23:17, 18; 1 Fal. 15:11, 12; 22:46; 2 Fal. 23:7; Ho 4:14
1 Fa. 14:251 Fal. 11:40
1 Fa. 14:252Nya 12:2-4
1 Fa. 14:261 Fal. 7:51; 15:18; 2 Fal. 18:14, 15; 24:12, 13
1 Fa. 14:261 Fal. 10:16, 17; 2Nya 12:9-11
1 Fa. 14:291Nya 27:24; 2Nya 12:15
1 Fa. 14:301 Fal. 15:6
1 Fa. 14:311 Fal. 11:43
1 Fa. 14:311 Fal. 11:1; 2Nya 12:13
1 Fa. 14:311Nya 3:10; Mt 1:7
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Wafalme 14:1-31

Cha Kwanza cha Wafalme

14 Wakati huo Abiya mwana wa Yeroboamu akakuwa mugonjwa. 2 Kwa hiyo Yeroboamu akamuambia bibi yake: “Tafazali, simama, na ujibadilishe sura ili wasijue kwamba wewe ni bibi ya Yeroboamu, na uende Shilo. Angalia! Ahiya nabii iko* kule. Yeye ndiye alisema kwamba mimi nitakuwa mufalme juu ya watu hawa.+ 3 Kamata mikate kumi (10), keki zenye zilinyunyiziwa* kitu, na chupa ya asali, na uende kwake. Kisha atakuambia kile kitamupata kijana huyu mudogo.”

4 Bibi ya Yeroboamu akafanya mambo yenye Yeroboamu alisema. Akasimama na kuenda Shilo+ na akakuja kwenye nyumba ya Ahiya. Macho ya Ahiya yalikuwa yanaangalia mbele tu, na hakuweza kuona kwa sababu ya uzee.

5 Lakini Yehova alikuwa amemuambia Ahiya: “Angalia, bibi ya Yeroboamu anakuja kutafuta habari kwako juu ya mwana wake, kwa maana ni mugonjwa. Nitakuambia mambo ya kumuambia.* Wakati atafika, atajifanya asiweze kutambuliwa.”

6 Wakati tu Ahiya alisikia sauti ya miguu ya mwanamuke huyo wakati alikuwa anakuja katika muingilio, akasema: “Ingia, bibi ya Yeroboamu. Sababu gani unajifanya usiweze kutambuliwa? Nimeagizwa nikutolee ujumbe mukali. 7 Uende, umuambie Yeroboamu, ‘Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Nilikuinua kutoka kati ya watu wako ili kukufanya kuwa kiongozi juu ya watu wangu Israeli.+ 8 Kisha nikanyanganya ufalme kutoka kwa nyumba ya Daudi na kukupatia wewe.+ Lakini haukukuwa kama mutumishi wangu Daudi, mwenye alishika amri zangu na mwenye alinifuata kwa moyo wake wote, akifanya tu mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho yangu.+ 9 Lakini umefanya mambo ya mubaya zaidi kuliko wote wenye walikutangulia, na ulijitengenezea mungu mwingine na sanamu za metali* ili kunikasirisha,+ na ni mimi ndiye umegeuzia mugongo wako.+ 10 Kwa sababu hiyo ninaleta musiba juu ya nyumba ya Yeroboamu, na nitaharibu* kutoka kwa Yeroboamu kila mwanaume,* kutia ndani wenye hawana uwezo na wenye kuwa wazaifu katika Israeli, na nitafagia kabisa nyumba ya Yeroboamu,+ kama vile wakati mutu anaondoa kabisa mavi mupaka yote yaishe! 11 Mutu yeyote wa Yeroboamu mwenye atakufia katika muji, imbwa watamukula; na mutu yeyote mwenye atakufia katika eneo la mashamba, ndege wa mbinguni watamukula, kwa maana Yehova amesema hayo.”’

12 “Sasa simama; uende kwenye nyumba yako. Wakati utatia muguu wako katika muji, ule mutoto atakufa. 13 Israeli wote watamuombolezea na kumuzika, kwa maana ni yeye tu katika familia ya Yeroboamu ndiye atalalishwa katika kaburi, kwa sababu ni yeye tu katika nyumba ya Yeroboamu ndiye Yehova Mungu wa Israeli amepata jambo fulani la muzuri ndani yake. 14 Yehova atajisimamishia mufalme juu ya Israeli mwenye ataharibu* nyumba ya Yeroboamu+ kuanzia siku hiyo na kuendelea, ndiyo, hata sasa. 15 Yehova atapiga na kuua Israeli kama utete wenye kuyumba-yumba ndani ya maji, na atangoa Israeli kutoka katika inchi hii ya muzuri yenye alipatia mababu zao,+ na atawatawanya ngambo ya Muto,*+ kwa sababu walitengeneza miti yao mitakatifu,*+ na kumukasirisha Yehova. 16 Na ataacha Israeli kwa sababu ya zambi zenye Yeroboamu ametenda na amefanya Israeli watende.”+

17 Basi bibi ya Yeroboamu akasimama na kuenda na akafika Tirsa. Wakati alifika kwenye kizingiti* cha nyumba, kijana huyo mudogo akakufa. 18 Kwa hiyo wakamuzika, na Israeli wote wakamuombolezea, kulingana na neno la Yehova lenye alikuwa amesema kupitia mutumishi wake Ahiya nabii.

19 Na mambo mengine ya historia ya Yeroboamu, namna alipigana vita+ na namna alitawala, yameandikwa katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli. 20 Na urefu wa utawala wa Yeroboamu ulikuwa* miaka makumi mbili na mbili (22), kisha akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake;+ na Nadabu mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.+

21 Wakati huo, Rehoboamu mwana wa Sulemani alikuwa mufalme katika Yuda. Rehoboamu alikuwa na miaka makumi ine na moja (41) wakati alikuwa mufalme, na alitawala kwa miaka kumi na saba (17) katika Yerusalemu, muji wenye Yehova alikuwa amechagua+ kati ya makabila yote ya Israeli kuwa mahali pa kutia jina lake.+ Jina la mama ya Rehoboamu lilikuwa Naama Mwamoni.+ 22 Na Yuda alikuwa anafanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova,+ na kupitia zambi zenye walitenda walimukasirisha kuliko vile mababu zao walifanya.+ 23 Pia waliendelea kujijengea mahali pa juu, nguzo takatifu, na miti mitakatifu*+ juu ya kila kilima kirefu+ na chini ya kila muti wenye majani mengi.+ 24 Kulikuwa pia wanaume makahaba wa hekalu katika inchi.+ Walitenda kulingana na mambo yote yenye kuchukiza ya mataifa yenye Yehova alikuwa amefukuza kutoka mbele ya Waisraeli.

25 Katika mwaka wa tano (5) wa Mufalme Rehoboamu, Mufalme Shishaki+ wa Misri akapanda ili kushambulia Yerusalemu.+ 26 Akakamata hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mufalme.+ Akakamata kila kitu, kutia ndani ngao zote za zahabu zenye Sulemani alikuwa ametengeneza.+ 27 Basi Mufalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba zichukue mahali pa ngao hizo, na akaziweka chini ya ulinzi wa wakubwa wa walinzi,* wenye walilinda muingilio wa nyumba ya mufalme. 28 Wakati wowote wenye mufalme alikuja kwenye nyumba ya Yehova, walinzi walikuwa wanazibeba, kisha walikuwa wanazirudisha katika chumba cha walinzi.

29 Na mambo mengine ya historia ya Rehoboamu, yote yenye alifanya, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda?+ 30 Kulikuwa vita yenye kuendelea kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.+ 31 Kisha Rehoboamu akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake na akazikwa pamoja na mababu zake katika Muji wa Daudi.+ Jina la mama yake lilikuwa Naama Mwamoni.+ Na Abiyamu*+ mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine