10 Mezali za Sulemani.+
Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake,+
Lakini mwana mupumbavu ni huzuni kwa mama yake.
2 Mali zenye zilipatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,
Lakini haki ndiyo inaokoa katika kifo.+
3 Yehova hataacha mwenye haki akae na njaa,+
Lakini ataima waovu mambo yenye wanatamani sana.
4 Mikono yenye uvivu italeta umaskini,+
Lakini mikono yenye bidii inaleta utajiri.+
5 Mwana mwenye kutenda kwa ufahamu anakusanya mazao wakati wa kipindi cha joto,
Lakini mwana mwenye kutenda kwa haya analala usingizi muzito wakati wa mavuno.+
6 Baraka ziko juu ya kichwa cha mwenye haki,+
Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.
7 Kumbukumbu la mwenye haki litabarikiwa,+
Lakini jina la muovu litaoza.+
8 Mutu mwenye moyo wa hekima atakubali mafundisho,+
Lakini mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+
9 Mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu atatembea kwa usalama,+
Lakini mwenye kupotosha njia zake atajulikana.+
10 Mwenye kufinya jicho lake kwa udanganyifu anatokeza huzuni,+
Na ule mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+
11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima,+
Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.+
12 Chuki ndiyo inachochea ugomvi,
Lakini upendo unafunika makosa yote.+
13 Hekima inapatikana kwenye midomo ya mutu mwenye utambuzi,+
Lakini fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa mutu mwenye hana akili ya muzuri.+
14 Watu wenye hekima wanaweka ujuzi kama hazina,+
Lakini kinywa cha mupumbavu kinaalika uharibifu.+
15 Mali ya tajiri ni muji wake wenye ngome.
Uharibifu wa maskini ni umaskini wao.+
16 Kazi ya mwenye haki inaongoza kwenye uzima;
Lakini mazao ya muovu yanaongoza kwenye zambi.+
17 Mwenye kutii nizamu ni njia yenye inapeleka kwenye uzima,
Lakini mwenye anapuuza karipio anapoteza wengine.
18 Mwenye kuficha chuki yake anasema uongo,+
Na mwenye kueneza habari zenye kuumiza ni mujinga.
19 Wakati maneno ni mengi, kosa haliwezi kuepukwa,+
Lakini mutu yeyote mwenye anazuia midomo yake anatenda kwa busara.+
20 Ulimi wa mwenye haki uko kama feza ya muzuri kabisa,+
Lakini moyo wa muovu uko na mafaa kidogo.
21 Midomo ya mwenye haki inakulisha wengi,+
Lakini wapumbavu wanakufa kwa sababu ya kukosa akili.+
22 Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri,+
Naye haongeze maumivu yoyote pamoja nayo.
23 Kujiingiza katika mwenendo wa haya ni kama muchezo kwa mujinga,
Lakini hekima ni ya mutu mwenye utambuzi.+
24 Kile muovu anaogopa kitamufikia;
Lakini tamaa ya mwenye haki itatimizwa.+
25 Wakati zoruba itapita, muovu hatakuwa tena,+
Lakini mwenye haki ni musingi milele.+
26 Kama siki kwenye meno na moshi katika macho,
Ni vile mutu muvivu iko kwa ule mwenye kumutuma.
27 Kumuogopa Yehova kunarefusha maisha,+
Lakini miaka ya waovu itafupishwa.+
28 Tumaini la wenye haki linaleta shangwe,+
Lakini tumaini la waovu litapotea.+
29 Njia ya Yehova ni ngome kwa mutu mwenye hana lawama,+
Lakini ni uharibifu kwa watenda maovu.+
30 Mwenye haki hataangushwa hata siku moja,+
Lakini waovu hawatakaa tena katika dunia.+
31 Kinywa cha mwenye haki kinatokeza hekima,
Lakini ulimi wenye kupotoka utakatwa.
32 Midomo ya mwenye haki inajua mambo yenye kupendeza,
Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.