Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • 1 Samweli 19
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika 1 Samweli

      • Sauli anaendelea kumuchukia Daudi (1-13)

      • Daudi anamukimbia Sauli (14-24)

1 Samweli 19:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 18:9; Mez. 27:4

1 Samweli 19:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 18:1; Mez. 18:24

1 Samweli 19:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 20:9, 13; Mez. 17:17

1 Samweli 19:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 22:14

1 Samweli 19:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Alitia nafsi yake katika mukono wake.”

  • *

    Ao “wokovu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 17:49
  • +1 Sa. 20:32

1 Samweli 19:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 16:21; 18:2, 13

1 Samweli 19:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 16:14
  • +1 Sa. 18:10, 11

1 Samweli 19:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Kama haufanye nafsi yako itoroke.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 59:utangulizi; 59:3

1 Samweli 19:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mungu wa familia; sanamu.”

  • *

    Ao “makila ya.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/6/2004, uku. 29

1 Samweli 19:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 18:9

1 Samweli 19:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mungu wa familia; sanamu.”

  • *

    Ao “makila ya.”

1 Samweli 19:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 18:29

1 Samweli 19:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 7:15, 17
  • +1 Sa. 20:1

1 Samweli 19:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

1 Samweli 19:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 19:18

1 Samweli 19:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “karibu uchi.”

  • *

    Ao “eko.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Sa. 10:11

Maandiko ingine

1 Sam. 19:11 Sa. 18:9; Mez. 27:4
1 Sam. 19:21 Sa. 18:1; Mez. 18:24
1 Sam. 19:31 Sa. 20:9, 13; Mez. 17:17
1 Sam. 19:41 Sa. 22:14
1 Sam. 19:51 Sa. 17:49
1 Sam. 19:51 Sa. 20:32
1 Sam. 19:71 Sa. 16:21; 18:2, 13
1 Sam. 19:91 Sa. 16:14
1 Sam. 19:91 Sa. 18:10, 11
1 Sam. 19:11Zab 59:utangulizi; 59:3
1 Sam. 19:151 Sa. 18:9
1 Sam. 19:171 Sa. 18:29
1 Sam. 19:181 Sa. 7:15, 17
1 Sam. 19:181 Sa. 20:1
1 Sam. 19:221 Sa. 19:18
1 Sam. 19:241 Sa. 10:11
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
1 Samweli 19:1-24

Cha Kwanza cha Samweli

19 Kisha wakati fulani Sauli akazungumuza na Yonatani mwana wake na watumishi wake wote kuhusu kumuua Daudi.+ 2 Kwa kuwa Yonatani mwana wa Sauli alimupenda sana Daudi,+ Yonatani akamuambia Daudi: “Sauli baba yangu anataka kukuua. Tafazali ufanye angalisho asubui, na uende mahali pa siri na uendelee kujificha. 3 Nitatoka na kusimama karibu na baba yangu katika shamba mahali kwenye utakuwa. Nitaongea na baba yangu kukuhusu, na kama ninapata habari yoyote, hakika nitakuambia.”+

4 Kwa hiyo Yonatani akazungumuza muzuri na Sauli baba yake kumuhusu Daudi.+ Akamuambia: “Mufalme hapaswe kumutendea zambi mutumishi wake Daudi kwa sababu yeye hajakutendea zambi na mambo yenye amekufanyia yamekuletea faida. 5 Alitia uzima wake katika hatari* ili kumupiga na kumuua ule Mufilisti,+ na hivyo Yehova akapatia Israeli wote ushindi* mukubwa. Uliona jambo hilo, na ukashangilia sana. Basi sababu gani utende zambi juu ya damu yenye haina kosa kwa kumuua Daudi bila sababu?”+ 6 Sauli akamusikiliza Yonatani, na akaapa: “Kama vile hakika Yehova anaishi, hatauawa.” 7 Kisha Yonatani akamuita Daudi na kumuambia mambo hayo yote. Kwa hiyo Yonatani akamupeleka Daudi kwa Sauli, na akaendelea kumutumikia kama vile zamani.+

8 Kisha wakati fulani vita ikatokea tena, na Daudi akaenda kupigana na Wafilisti na akawapiga na kuwaua kwa mauaji makubwa, nao wakakimbia mbele yake.

9 Na roho ya mubaya kutoka kwa Yehova ikakuja juu ya Sauli+ wakati alikuwa amekaa katika nyumba yake akiwa na mukuki katika mukono wake, wakati huo Daudi alikuwa anapiga muziki kwa kinubi.+ 10 Sauli akajaribu kumupigilia Daudi kwenye ukuta kwa mukuki, lakini akamukwepa Sauli, mwenye aliingiza mukuki huo katika ukuta. Daudi akakimbia na kutoroka usiku huo. 11 Kisha wakati fulani Sauli akatuma wajumbe kwenye nyumba ya Daudi ili wailinde na kumuua asubui,+ lakini Mikali bibi ya Daudi akamuambia: “Kama hautoroke* usiku wa leo, kesho utakuwa mufu.” 12 Mara moja Mikali akamuteremusha Daudi kupitia dirisha, ili akimbie na kutoroka. 13 Mikali akakamata sanamu ya terafimu* na kuitia kwenye kitanda, na akatia wavu wa* manyoya ya mbuzi mahali kwenye Daudi anatia kichwa chake, na akaifunika na nguo.

14 Basi Sauli akatuma wajumbe wamulete Daudi, lakini bibi ya Daudi akasema: “Ni mugonjwa.” 15 Kwa hiyo Sauli akatuma wajumbe hao ili wamuone Daudi na akawaambia: “Mumulete kwangu akiwa kwenye kitanda chake ili auawe.”+ 16 Wakati wajumbe hao waliingia, sanamu ya terafimu* ilikuwa kwenye kitanda na wavu wa* manyoya ya mbuzi mahali kwenye kichwa chake kilipaswa kuwa. 17 Sauli akamuambia Mikali: “Sababu gani ulinidanganya hivi na kumuacha adui yangu+ akimbie ili atoroke?” Mikali akamujibu Sauli: “Aliniambia, ‘Uniache niende, ili nisikuue!’”

18 Sasa Daudi alikuwa amekimbia na kutoroka, na akafika kwa Samweli kule Rama.+ Akamuambia mambo yote yenye Sauli alikuwa amemutendea. Kisha yeye na Samweli wakaenda zao, na wakabakia kule Naioti.+ 19 Kisha wakati fulani Sauli akaambiwa: “Angalia! Daudi iko* Naioti kule Rama.” 20 Mara moja Sauli akatuma wajumbe ili wamukamate Daudi. Wakati waliona manabii wenye kuzeeka wakitoa unabii na Samweli akiwa amesimama na kuwaongoza, roho ya Mungu ikakuja juu ya wajumbe wa Sauli, nao pia wakaanza kutenda kama manabii.

21 Wakati walimuambia Sauli habari hiyo, mara moja akatuma wajumbe wengine, nao pia wakaanza kutenda kama manabii. Kwa hiyo Sauli akatuma tena wajumbe wengine, kikundi cha tatu (3), nao pia wakaanza kutenda kama manabii. 22 Mwishowe yeye pia akaenda Rama. Wakati alifika kwenye tangi kubwa lenye kuwa kule Seku, akauliza: “Samweli na Daudi wako wapi?” Wakajibu: “Kule Naioti+ katika Rama.” 23 Wakati Sauli alikuwa katika njia yake kutoka kule ili kuenda Naioti kule Rama, roho ya Mungu ikakuja juu yake pia, naye akatembea akitenda kama nabii mupaka wakati aliingia katika Naioti kule Rama. 24 Akavua pia nguo zake, naye pia akatenda kama nabii mbele ya Samweli, na akalala kule muchana wote na usiku huo wote akiwa uchi.* Ndiyo sababu watu wanasema: “Je, Sauli pia iko* kati ya manabii?”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine