Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Wimbo wa Sulemani 8
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Wimbo wa Sulemani

    • MUSHULAMI AKIWA YERUSALEMU (3:6–8:4)

    • MUSHULAMI ANARUDIA, ANAONYESHA USHIKAMANIFU WAKE (8:5-14)

        • Ndugu za kijana mwanamuke (5a)

          • ‘Ni nani huyu, mwenye kuegemea mupenzi wake?’

        • Kijana mwanamuke (5b-7)

          • “Upendo uko na nguvu kama kifo” (6)

        • Ndugu za kijana mwanamuke (8, 9)

          • “Kama yeye ni ukuta, . . . lakini kama yeye ni mulango, . . .” (9)

        • Kijana mwanamuke (10-12)

          • “Mimi ni ukuta” (10)

        • Muchungaji (13)

          • ‘Acha nisikie sauti yako’

        • Kijana mwanamuke (14)

          • “Ukimbie mbio kama swala”

Wimbo wa Sulemani 8:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 1:2

Wimbo wa Sulemani 8:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 3:4

Wimbo wa Sulemani 8:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 2:6

Wimbo wa Sulemani 8:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 2:7; 3:5

Wimbo wa Sulemani 8:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

  • *

    “Yah” ni kifupi cha jina Yehova.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoh 15:13; Efe 5:25; Ufu 12:11
  • +Kum 4:24; 1 Yo. 4:8

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2015, uku. 29

    15/5/2012, uku. 4

    15/11/2006, uku. 20

Wimbo wa Sulemani 8:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “Angezarauliwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Kor. 13:8, 13
  • +Rom. 8:38, 39

Wimbo wa Sulemani 8:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 1:6

Wimbo wa Sulemani 8:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mhu. 2:4

Wimbo wa Sulemani 8:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 1:6; 6:11
  • +Wim 2:14

Wimbo wa Sulemani 8:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Wim 2:9, 17

Maandiko ingine

Wim. 8:1Wim 1:2
Wim. 8:2Wim 3:4
Wim. 8:3Wim 2:6
Wim. 8:4Wim 2:7; 3:5
Wim. 8:6Yoh 15:13; Efe 5:25; Ufu 12:11
Wim. 8:6Kum 4:24; 1 Yo. 4:8
Wim. 8:71 Kor. 13:8, 13
Wim. 8:7Rom. 8:38, 39
Wim. 8:8Wim 1:6
Wim. 8:11Mhu. 2:4
Wim. 8:13Wim 1:6; 6:11
Wim. 8:13Wim 2:14
Wim. 8:14Wim 2:9, 17
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Wimbo wa Sulemani 8:1-14

Wimbo wa Sulemani

8 “Ikiwa tu ungekuwa kama ndugu yangu,

Mwenye alinyonya maziwa ya mama yangu!

Basi kama ningekukuta inje, ningekubusu.+

Na hakuna mwenye angenizarau.

 2 Ningekuongoza;

Ningekuleta kwenye nyumba ya mama yangu,+

Mwenye alinifundisha.

Ningekupatia divai yenye kutiwa manukato ili ukunywe,

Maji safi ya matunda ya makomamanga.

 3 Mukono wake wa kushoto ungekuwa chini ya kichwa changu,

Na mukono wake wa kuume ungenikumbatia.+

 4 “Ninawaapisha, Enyi mabinti wa Yerusalemu:

Musijaribu kuamusha ao kuchochea upendo ndani yangu mupaka wakati huo wenyewe utataka.”+

 5 “Ni nani huyu mwenye anapanda kutoka katika jangwa,

Akiwa ameegemea mupenzi wake?”

“Chini ya muti wa mutofaa nilikuamusha.

Kule, mama yako alikuwa katika uchungu wa kukuzaa.

Kule, mwenye alikuzaa alikuwa katika uchungu wa kuzaa.

 6 Unitie kama muhuri juu ya moyo wako,

Kama muhuri juu ya mukono wako,

Kwa maana upendo uko na nguvu kama kifo,+

Na tamaa ya mutu ya kutaka washikamane na yeye tu ni yenye kudai kama Kaburi.*

Miali yake ni moto wenye kuwaka sana, mwali wa moto wa Yah.*+

 7 Maji mengi hayawezi kuzima upendo,+

Wala mito haiwezi kuufagilia mbali.+

Kama mutu angetoa mali yote ya nyumba yake kwa ajili ya upendo,

Ingezarauliwa* kabisa.”

 8 “Tuko na dada mudogo,+

Na hana maziwa.

Tutamufanyia nini dada yetu

Siku yenye watamuomba?”

 9 “Kama yeye ni ukuta,

Tutajenga juu yake munara wa feza,

Lakini kama yeye ni mulango,

Tutamuzuia kwa mbao ya muti wa mwerezi.”

10 “Mimi ni ukuta,

Na maziwa yangu ni kama minara.

Basi mbele ya macho yake nimekuwa

Kama mutu mwenye anapata amani.

11 Sulemani alikuwa na shamba la mizabibu+ kule Baal-hamoni.

Alipatia watunzaji shamba hilo la mizabibu.

Kila mumoja wao alikuwa analeta vipande elfu moja (1 000) vya feza kwa ajili ya matunda yake.

12 Niko na shamba langu mwenyewe la mizabibu.

Vile vipande elfu moja (1 000) vya feza ni vyako, Ee Sulemani,

Na vipande mia mbili (200) ni vya wale wenye wanatunza matunda yake.”

13 “Ee wewe mwenye kukaa katika mabustani,+

Marafiki wanasikiliza sauti yako.

Acha niisikie.”+

14 “Fanya haraka, mupenzi wangu,

Na ukimbie mbio kama swala+

Kama paa mudogo

Juu ya milima ya manukato.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine