Sefania
1 Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Sefania* mwana wa Kushi mwana wa Gedalia mwana wa Amaria mwana wa Hezekia katika siku za Yosia+ mwana wa Amoni+ mufalme wa Yuda:
2 “Nitafagilia mbali kila kitu kutoka kwenye uso wa udongo,” ni vile Yehova anasema.+
3 “Nitafagilia mbali mwanadamu na munyama.
Nitafagilia mbali ndege wa mbinguni na samaki wa bahari,+
Na nitaondoa wanadamu kwenye uso wa udongo,” ni vile Yehova anasema.
4 “Nitanyoosha mukono wangu juu ya Yuda
Na juu ya wakaaji wote wa Yerusalemu,
Na nitaondoa mahali hapa mabaki* yote ya Baali,+
Jina la makuhani wa miungu ya kigeni na makuhani,+
5 Na wale wenye kuinamia jeshi la mbinguni juu ya sehemu za juu za nyumba,+
Na wale wenye kumuinamia Yehova na kuapa kuwa washikamanifu kwake+
Wakati huohuo wakiapa kuwa washikamanifu kwa Malkamu;+
6 Na wale wenye kuacha kumufuata Yehova+
Na wenye hawamutafute Yehova wala kumuuliza.”+
7 Munyamaze mbele ya Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, kwa maana siku ya Yehova iko karibu.+
Yehova ametayarisha zabihu; ametakasa wenye alialika.
8 “Katika siku ya zabihu ya Yehova nitaomba wakubwa watoe hesabu,
Wana wa mufalme,+ na wote wenye kuvaa nguo za kigeni.
9 Nitaomba kila mutu mwenye kupanda kwenye jukwaa* siku hiyo atoe hesabu,
Wale wenye kujaza nyumba ya bwana wao jeuri na udanganyifu.
10 Siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,
“Sauti ya kilio itasikika katika Mulango Mukubwa wa Samaki,+
Makelele katika Eneo la Pili la muji,+
Na kishindo kikubwa kutoka kwenye vilima.
11 Mulalamike, ninyi wakaaji wa Makteshi,*
Kwa maana wafanyabiashara wote wameangamizwa;*
Wale wote wenye kupima feza wameharibiwa.
12 Wakati huo nitatafuta-tafuta kabisa katika Yerusalemu kwa taa,
Na nitaomba wale wenye hawajali* watoe hesabu, wale wenye kusema katika moyo wao,
‘Yehova hatatenda mema, wala hatatenda mabaya.’+
13 Mali yao itanyanganywa na nyumba zao zitaharibiwa.+
Watajenga nyumba, lakini hawataishi ndani;
Na watapanda mizabibu, lakini hawatakunywa divai yake.+
14 Ile siku kubwa ya Yehova iko karibu!+
Iko karibu na inakuja haraka sana!*+
Sauti ya siku ya Yehova inaleta uchungu.+
Siku hiyo mupiganaji-vita atalia kwa sauti kubwa.+