Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Mambo ya Walawi 17
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Mambo ya Walawi

      • Tabenakulo, mahali pa kutoa zabihu (1-9)

      • Kula damu kunakatazwa (10-14)

      • Sheria kuhusu wanyama wenye walipatikana wamekufa (15, 16)

Mambo ya Walawi 17:4

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kuuawa kutoka.”

Mambo ya Walawi 17:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 3:1, 2; 7:11

Mambo ya Walawi 17:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

  • *

    Ao “ya kumutuliza.” Tnn., “ya kumupumuzisha.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 3:3-5; 7:29-31

Mambo ya Walawi 17:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mbuzi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 32:17; Yosh. 24:14
  • +Kut 34:15; Kum 31:16

Mambo ya Walawi 17:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kuuawa kutoka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 1:3; Kum 12:5, 6, 13, 14

Mambo ya Walawi 17:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi hiyo yenye inakula.”

  • *

    Ao “nitamuua kutoka.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 9:4; Law. 3:17; 7:26; 19:26; 1 Sa. 14:33; Mdo 15:20, 29

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 29

Mambo ya Walawi 17:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi ya iko.”

  • *

    Ao “kwa ajili ya nafsi zenu.”

  • *

    Ao “nafsi yenye.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 17:14; Kum 12:23
  • +Law. 8:15; 16:18
  • +Mt 26:28; Rom. 3:25; 5:9; Efe 1:7; Ebr 9:22; 13:12; 1 Pe. 1:2; 1 Yo. 1:7; Ufu 1:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Upendo wa Mungu,” uku. 75

    Munara wa Mulinzi,

    15/11/2014, uku. 10-11

    Munara wa Mulinzi,

    15/6/2004, uku. 15

Mambo ya Walawi 17:12

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 12:49
  • +Kum 12:23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/6/2004, uku. 15

Mambo ya Walawi 17:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 12:16; 15:23

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Biblia Inafundisha, uku. 129

    Munara wa Mulinzi,

    15/6/2004, uku. 15

    15/10/2000, uku. 30-31

Mambo ya Walawi 17:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi ya.”

  • *

    Ao “nafsi iko.”

  • *

    Ao “nafsi ya.”

  • *

    Ao “atauawa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 17:10, 11

Mambo ya Walawi 17:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kut 22:31; Kum 14:21
  • +Law. 11:40

Mambo ya Walawi 17:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 19:20

Maandiko ingine

Mambo ya walawi 17:5Law. 3:1, 2; 7:11
Mambo ya walawi 17:6Law. 3:3-5; 7:29-31
Mambo ya walawi 17:7Kum 32:17; Yosh. 24:14
Mambo ya walawi 17:7Kut 34:15; Kum 31:16
Mambo ya walawi 17:9Law. 1:3; Kum 12:5, 6, 13, 14
Mambo ya walawi 17:10Mwa 9:4; Law. 3:17; 7:26; 19:26; 1 Sa. 14:33; Mdo 15:20, 29
Mambo ya walawi 17:11Law. 17:14; Kum 12:23
Mambo ya walawi 17:11Law. 8:15; 16:18
Mambo ya walawi 17:11Mt 26:28; Rom. 3:25; 5:9; Efe 1:7; Ebr 9:22; 13:12; 1 Pe. 1:2; 1 Yo. 1:7; Ufu 1:5
Mambo ya walawi 17:12Kut 12:49
Mambo ya walawi 17:12Kum 12:23
Mambo ya walawi 17:13Kum 12:16; 15:23
Mambo ya walawi 17:14Law. 17:10, 11
Mambo ya walawi 17:15Kut 22:31; Kum 14:21
Mambo ya walawi 17:15Law. 11:40
Mambo ya walawi 17:16Hes 19:20
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Mambo ya Walawi 17:1-16

Mambo ya Walawi

17 Yehova akaendelea kusema na Musa: 2 “Sema na Haruni na wana wake na Waisraeli wote na uwaambie, ‘Yehova ameamuru hivi:

3 “‘“Kama mutu yeyote wa nyumba ya Israeli anachinja ngombe-dume ao mwana-kondoo dume ao mbuzi ndani ya kambi ao kama anamuchinja inje ya kambi, 4 kuliko kumuleta kwenye muingilio wa hema ya mukutano ili kumutoa kuwa toleo kwa Yehova mbele ya tabenakulo ya Yehova, mutu huyo atakuwa na hatia ya damu. Amemwanga damu na mutu huyo anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake. 5 Itakuwa vile ili Waisraeli wamuletee Yehova zabihu, zenye wanatoa kwa sasa katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba, wamuletee kuhani zabihu hizo kwenye muingilio wa hema ya mukutano. Wanapaswa kumutolea Yehova zabihu hizo zikiwa zabihu za ushirika.+ 6 Na kuhani atanyunyiza* damu ya zabihu hizo juu ya mazabahu ya Yehova kwenye muingilio wa hema ya mukutano na atachoma mafuta yake ili yatoe moshi na kuwa harufu ya kumupendeza* Yehova.+ 7 Kwa hiyo hawapaswe tena kutoa zabihu kwa pepo wachafu wenye kufanana mbuzi,*+ wenye wanafanya nao ukahaba.+ Hiyo itakuwa sheria ya kudumu kwa ajili yenu katika vizazi vyenu vyote.”’

8 “Unapaswa kuwaambia, ‘Kila mutu wa nyumba ya Israeli ao kila mugeni mwenye anaishi katikati yenu mwenye atatoa toleo la kuteketezwa ao zabihu 9 na hailete kwenye muingilio wa hema ya mukutano ili kuitolea Yehova anapaswa kuondolewa* katikati ya watu wake.+

10 “‘Kama mutu yeyote wa nyumba ya Israeli ao mugeni yeyote mwenye anaishi katikati yenu anakula damu ya namna yoyote,+ hakika nitakunja uso wangu juu ya mutu huyo mwenye anakula* damu, na nitamuondoa* katikati ya watu wake. 11 Kwa maana uzima wa mwili uko* katika damu,+ na mimi mwenyewe nimeitoa kwenye mazabahu+ kwa ajili yenu* ili mufunike zambi kwa ajili yenu wenyewe, kwa maana damu ndiyo inafunika zambi+ kupitia uzima wenye* kuwa ndani yake. 12 Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli: “Hakuna mutu* katikati yenu mwenye anapaswa kula damu, na hakuna mugeni mwenye anaishi katikati yenu+ mwenye anapaswa kula damu.”+

13 “‘Kama mutu fulani katikati ya Waisraeli ao mugeni fulani mwenye anaishi katikati yenu anawinda na anakamata munyama wa pori ao ndege mwenye anaweza kukuliwa, anapaswa kumwanga damu yake chini+ na kuifunika kwa mavumbi. 14 Kwa maana uzima wa* kila namna ya mwili ni damu yake, kwa sababu uzima uko* ndani ya damu. Kwa hiyo, niliambia Waisraeli: “Hamupaswe kula damu ya namna yoyote ya mwili kwa sababu uzima wa* kila namna ya mwili uko katika damu yake. Kila mutu mwenye anakula damu ataondolewa.”*+ 15 Kama mutu fulani, ikuwe mwenyeji ao mugeni, anakula munyama mwenye alipatikana amekufa ao mwenye alipasuliwa na munyama wa pori,+ basi anapaswa kufua nguo zake na kuoga ndani ya maji na hatakuwa safi mupaka mangaribi;+ kisha atakuwa safi. 16 Lakini kama hafue nguo hizo na haoge mwili wake, atajibu kwa sababu ya kosa lake.’”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine