Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
24 Yehoashi alikuwa na miaka saba (7) wakati alikuwa mufalme,+ na alitawala kwa miaka makumi ine (40) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Sibia kutoka Beer-sheba.+ 2 Yehoashi aliendelea kufanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova sikuzote za Yehoyada kuhani.+ 3 Yehoyada alimuchagulia bibi wawili, na akazaa watoto wanaume na watoto wanamuke.
4 Kisha mambo hayo moyo wa Yehoashi ukatamani kutengeneza nyumba ya Yehova.+ 5 Basi akakusanya pamoja makuhani na Walawi na kuwaambia: “Muende kwenye miji ya Yuda na mukusanye feza kutoka kwa Israeli wote ili kutengeneza nyumba ya Mungu wenu+ mwaka kwa mwaka; na munapaswa kutenda haraka kuhusu jambo hili.” Lakini Walawi hawakutenda haraka.+ 6 Basi mufalme akamuita mukubwa Yehoyada na kumuambia:+ “Sababu gani haukuomba Walawi walete kutoka Yuda na Yerusalemu kodi takatifu yenye iliagizwa na Musa+ mutumishi wa Yehova, ile kodi takatifu ya kutaniko la Israeli, kwa ajili ya hema ya Ushuhuda?+ 7 Kwa maana wana wa Atalia,+ ule mwanamuke muovu, walikuwa wamevunja na kuingia ndani ya nyumba ya Mungu wa kweli,+ na walikuwa wametumia vitu vyote vitakatifu vya nyumba ya Yehova kwa ajili ya Mabaali.” 8 Kisha, kwa agizo la mufalme, sanduku+ likatengenezwa na kuwekwa inje kwenye mulango mukubwa wa nyumba ya Yehova.+ 9 Kisha, tangazo likatolewa katika Yuda yote na Yerusalemu ili kumuletea Yehova kodi takatifu+ yenye Musa mutumishi wa Mungu wa kweli alikuwa ameagiza juu ya Israeli katika jangwa. 10 Wakubwa wote na watu wote wakafurahi,+ na wakaendelea kuleta michango na kuitumbukiza katika sanduku hilo mupaka wakati lilijaa.*
11 Kila mara wakati Walawi walileta lile sanduku ili walipatie mufalme na wakati waliona kwamba kulikuwa feza nyingi ndani, mwandishi wa mufalme na mwakilishi wa mukubwa wa makuhani walikuwa wanakuja na kutosha feza hizo katika sanduku,+ na kisha walikuwa wanalirudisha kwenye lilikuwa. Ni vile walifanya siku kwa siku, na walikusanya feza kwa wingi. 12 Kisha mufalme pamoja na Yehoyada walikuwa wanazipatia wale wenye kusimamia kazi ya utumishi wa nyumba ya Yehova, na hao walikuwa wanakodi wachongaji wa majiwe na mafundi kwa ajili ya kutengeneza nyumba ya Yehova,+ na pia wafanyakazi wa chuma na shaba ili kutengeneza nyumba ya Yehova. 13 Na wale wenye kusimamia kazi wakaianzisha, na kazi hiyo ya kutengeneza ikasonga mbele chini ya usimamizi wao, na wakarudisha nyumba ya Mungu wa kweli katika hali yake yenye kufaa na wakaifanya kuwa imara. 14 Na wakati tu walimaliza, walileta feza zenye zilibakia na kuzipatia mufalme na Yehoyada, na wakazitumia ili kutengeneza vyombo kwa ajili ya nyumba ya Yehova, vyombo kwa ajili ya utumishi na kwa ajili ya kutoa matoleo na vikombe na vyombo vya zahabu na vya feza.+ Na walikuwa wanatoa zabihu za kuteketezwa+ kwa ukawaida kwenye nyumba ya Yehova siku zote za Yehoyada.
15 Wakati Yehoyada alikuwa amezeeka na mwenye kushiba miaka, akakufa; alikuwa na miaka mia moja makumi tatu (130) wakati wa kifo chake. 16 Basi wakamuzika katika Muji wa Daudi pamoja na wafalme,+ kwa sababu alikuwa ametenda mema katika Israeli+ kuhusiana na Mungu wa kweli na nyumba Yake.
17 Kisha kifo cha Yehoyada wakubwa wa Yuda walikuja na kumuinamia mufalme, na mufalme akawasikiliza. 18 Wakaacha nyumba ya Yehova Mungu wa mababu zao na wakaanza kutumikia miti mitakatifu* na sanamu, na hivyo kasirani ya Mungu ikakuja* juu ya Yuda na Yerusalemu kwa sababu ya hatia yao. 19 Aliendelea kutuma manabii kati yao ili kuwarudisha kwa Yehova, na waliendelea kuwaonya,* lakini walikataa kusikiliza.+
20 Roho ya Mungu ikakuja juu ya* Zekaria mwana wa Yehoyada+ kuhani, na akasimama juu ya watu na kuwaambia: “Mungu wa kweli anasema hivi: ‘Sababu gani munavunja amri za Yehova? Hamutapata matokeo ya muzuri! Kwa sababu mumeacha Yehova, yeye naye, atawaacha ninyi.’”+ 21 Lakini wakafanya mupango mubaya juu yake+ na wakamupiga majiwe kwa agizo la mufalme katika kiwanja cha nyumba ya Yehova.+ 22 Basi Mufalme Yehoashi hakukumbuka upendo mushikamanifu wenye Yehoyada baba yake* alikuwa amemuonyesha, na akamuua mwana wake, mwenye alisema hivi wakati alikuwa anakufa: “Yehova aone jambo hili na akuombe utoe hesabu.”+
23 Kwenye mwanzo wa mwaka, jeshi la Siria lilikuja kupigana na Yehoashi, na wakashambulia Yuda na Yerusalemu.+ Kisha wakaua wakubwa wote+ wa watu, na wakamupelekea mufalme wa Damasko vitu vyao vyote vyenye vilichukuliwa katika vita. 24 Kwa maana hata kama jeshi la Siria lenye kushambulia lilikuwa na watu kidogo, Yehova alitia katika mukono wao jeshi kubwa sana,+ kwa sababu walikuwa wamemuacha Yehova Mungu wa mababu zao; basi wakafanya* hukumu juu ya Yehoashi. 25 Na wakati waliondoka kwake (kwa maana walimuacha akiwa ameumizwa sana*), watumishi wake mwenyewe wakafanya mupango mubaya juu yake kwa sababu alikuwa amemwanga damu ya wana* wa Yehoyada+ kuhani.+ Wakamuua katika kitanda chake mwenyewe. Basi akakufa na wakamuzika katika Muji wa Daudi,+ lakini hawakumuzika katika makaburi ya wafalme.+
26 Hawa ndio walifanya mupango mubaya+ juu yake: Zabadi mwana wa Shimeati mwanamuke Mwamoni na Yehozabadi mwana wa Shimriti mwanamuke Mumoabu. 27 Kuhusu wana wake na matangazo mengi yenye yalifanywa juu yake+ na pia kazi ya kutengeneza* nyumba ya Mungu wa kweli,+ mambo hayo yote yameandikwa katika maandishi* ya Kitabu cha Wafalme. Na Amazia mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.