Kulingana na Marko
16 Basi wakati Sabato+ iliisha, Maria Magdalene, Maria+ mama ya Yakobo, na Salome wakanunua manukato ili wakuje na kuyapakaa kwenye mwili wa Yesu.+ 2 Na asubui sana, siku ya kwanza ya juma, wakati jua lilikuwa limetokea, wakakuja kwenye kaburi.*+ 3 Walikuwa wanaulizana: “Ni nani atatuviringishia jiwe kutoka kwenye muingilio wa kaburi?” 4 Lakini wakati waliinua macho, wakaona lile jiwe lilikuwa limeviringishwa, hata kama lilikuwa kubwa sana.+ 5 Wakati waliingia katika kaburi, wakamuona kijana mwanaume amekaa upande wa kuume, akiwa amevaa kanzu nyeupe, na wakashangaa sana. 6 Akawaambia: “Musishangae.+ Munamutafuta Yesu Munazareti mwenye aliuawa kwenye muti. Amefufuliwa;+ haiko hapa. Muangalie mahali walimulalisha.+ 7 Lakini muende, muambie wanafunzi wake na Petro, ‘Yesu anawatangulia kuingia Galilaya.+ Mutamuona kule, kama vile aliwaambia.’”+ 8 Basi wakati walitoka inje ya kaburi, wakakimbia, wakitetemeka na kushangaa sana. Na hawakumuambia mutu yeyote jambo lolote, kwa sababu walikuwa na woga.*+