Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 14
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Waamuzi

      • Muamuzi Samsoni anatafuta bibi Mufilisti (1-4)

      • Roho ya Yehova inawezesha Samsoni kuua simba (5-9)

      • Kitendawili cha Samsoni kwenye karamu ya ndoa (10-19)

      • Mwanaume mwingine anapewa bibi ya Samsoni (20)

Waamuzi 14:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mwanamuke mumoja kati ya mabinti wa Wafilisti.”

Waamuzi 14:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “anafaa katika macho yangu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 7:3

Waamuzi 14:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 13:1

Waamuzi 14:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Waamuzi 14:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 13:24, 25

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/1/2005, uku. 31

Waamuzi 14:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 14:2

Waamuzi 14:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 24:67; Mt 1:24

Waamuzi 14:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 14:8, 9

Waamuzi 14:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 16:5

Waamuzi 14:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 16:15

Waamuzi 14:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 16:16, 18

Waamuzi 14:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao pengine, “mbele aingie katika chumba cha ndani.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 14:14
  • +Amu 14:15

Waamuzi 14:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 13:24, 25; 14:6; 15:14
  • +Yosh. 13:2, 3; Amu 1:18
  • +Amu 14:12

Waamuzi 14:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Amu 14:2
  • +Amu 14:11; 15:1, 2

Maandiko ingine

Amu. 14:3Kum 7:3
Amu. 14:4Amu 13:1
Amu. 14:6Amu 13:24, 25
Amu. 14:7Amu 14:2
Amu. 14:8Mwa 24:67; Mt 1:24
Amu. 14:14Amu 14:8, 9
Amu. 14:15Amu 16:5
Amu. 14:16Amu 16:15
Amu. 14:17Amu 16:16, 18
Amu. 14:18Amu 14:14
Amu. 14:18Amu 14:15
Amu. 14:19Amu 13:24, 25; 14:6; 15:14
Amu. 14:19Yosh. 13:2, 3; Amu 1:18
Amu. 14:19Amu 14:12
Amu. 14:20Amu 14:2
Amu. 14:20Amu 14:11; 15:1, 2
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Waamuzi 14:1-20

Waamuzi

14 Kisha Samsoni akashuka mupaka Timna, na kule Timna akamuona mwanamuke mumoja Mufilisti.* 2 Basi akapanda na kumuambia baba yake na mama yake: “Nimeona mwanamuke mumoja Mufilisti kule Timna, na ninataka munichukulie mwanamuke huyo akuwe bibi yangu.” 3 Lakini baba yake na mama yake wakamuambia: “Je, hauwezi kupata bibi kati ya watu wa jamaa yako na kati ya watu wetu?+ Je, ni lazima uende na kuchukua bibi kati ya Wafilisti wenye hawatahiriwe?” Lakini Samsoni akamuambia baba yake: “Unichukulie mwanamuke huyo, kwa sababu yeye ndiye ananifaa.”* 4 Baba yake na mama yake hawakujua kwamba hilo lilitoka kwa Yehova, kwa sababu Mungu alikuwa anatafuta nafasi ya kupiga Wafilisti, kwa maana Wafilisti walikuwa wanatawala juu ya Israeli wakati huo.+

5 Basi Samsoni akashuka na baba yake na mama yake mupaka Timna. Wakati alifika katika mashamba ya mizabibu ya Timna, angalia! simba* akakuja akimungurumia. 6 Kisha roho ya Yehova ikamutia nguvu,+ na akapasua simba huyo vipande mbili, kama vile mutu anapasua mwana-mbuzi kwa mikono yake tu. Lakini hakuambia baba yake ao mama yake jambo lenye alikuwa amefanya. 7 Kisha akashuka na kuzungumuza na ule mwanamuke, na mwanamuke huyo alikuwa angali mwenye kufaa mbele ya macho ya Samsoni.+

8 Kisha pale, wakati alikuwa anarudia kukamata ule mwanamuke ili aende naye nyumbani,+ akaenda pembeni kuangalia ule muzoga wa simba, na katika muzoga huo kulikuwa nyuki wengi na asali. 9 Basi akakamata asali hiyo katika mikono yake na kuikula wakati alikuwa anatembea. Wakati alikuta baba yake na mama yake, akawapatia sehemu ya asali ili wakule. Lakini hakuwaambia kuwa aliiparuza kutoka katika muzoga wa simba.

10 Baba yake akashuka mupaka kwa ule mwanamuke, na Samsoni akafanya karamu kule, kwa maana ni vile vijana walizoea kufanya. 11 Wakati walimuona, wakaleta marafiki makumi tatu (30) wa bwana-arusi ili wamusindikize. 12 Kisha Samsoni akawaambia: “Tafazali, niwaambie kitendawili. Ikiwa katika siku saba (7) za karamu munaleta maana yake na kuniambia jibu, nitawapatia nguo makumi tatu (30) za kitani na nguo makumi tatu za kuvaliwa pamoja. 13 Lakini kama munashindwa kuniambia jibu, mutanipatia nguo makumi tatu (30) ya kitani na nguo zingine makumi tatu.” Wakasema: “Utuambie kitendawili chako; tunapenda kukisikia.” 14 Basi akawaambia:

“Katika mwenye kula mulitoka kitu cha kula,

Na katika mwenye nguvu mulitoka kitu kitamu.”+

Hawakuweza kuleta maana ya kitendawili hicho kwa siku tatu (3). 15 Siku ya ine (4) wakamuambia bibi ya Samsoni: “Umushawishi bwana yako+ ili atuambie maana ya kitendawili hicho. Kama haufanye vile, tutakuteketeza kwa moto wewe pamoja na watu wa nyumba ya baba yako. Je, mulitualika hapa ili mukamate mali zetu?” 16 Basi bibi ya Samsoni akamulilia na kusema: “Unanichukia; haunipendi.+ Uliambia watu wangu kitendawili, lakini haujaniambia maana yake.” Samsoni akamuambia: “Angalia, sikuambia hata baba yangu wala mama yangu! Nikuambie wewe?” 17 Lakini aliendelea kumulilia katika zile siku zenye zilibakia za karamu hiyo ya siku saba (7). Mwishowe Samsoni akamuambia siku ya saba, kwa sababu alikuwa amemukaza sana. Kisha akaambia watu wake maana ya kitendawili hicho.+ 18 Basi siku ya saba (7) mbele ya jua kushuka,* watu wa muji wakamuambia Samsoni:

“Ni nini kitamu kuliko asali,

Na ni nani mwenye nguvu kuliko simba?”+

Akawajibu:

“Kama hamungelima na ngombe wangu mudogo,+

Hamungeleta maana ya kitendawili changu.”

19 Kisha roho ya Yehova ikamutia nguvu,+ akaenda Ashkeloni,+ akapiga na kuua watu makumi tatu (30), akakamata nguo zao na kuzipatia watu wenye walikuwa wameleta maana ya kitendawili hicho.+ Akapanda nyumbani kwa baba yake akiwa amekasirika sana.

20 Bibi ya Samsoni+ akapewa mumoja wa wale marafiki wa bwana-arusi wenye walikuwa wamemusindikiza Samsoni.+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine