Zaburi
96 Mumuimbie Yehova wimbo mupya.+
Mumuimbie Yehova, dunia yote!+
2 Mumuimbie Yehova; musifu jina lake.
Mutangaze habari njema za wokovu wake siku kwa siku.+
4 Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.
Ni mwenye kuogopesha sana kuliko miungu mingine yote.
5 Miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu yenye haina mafaa yoyote,+
Lakini Yehova ndiye alifanya mbingu.+
7 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi familia za vikundi vya watu,
Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
8 Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili;+
Mulete zawadi na muingie katika viwanja vyake.
10 Mutangaze kati ya mataifa: “Yehova amekuwa Mufalme!+
Dunia* imewekwa imara kabisa, haiwezi kuhamishwa.*
Atahukumu vikundi vya watu kwa haki.”*+
11 Mbingu zishangilie, na dunia ifurahi;
Bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza;+
12 Maeneo ya mashamba na vyote vyenye kuwa ndani yake vishangilie.+