Isaya
28 Ole wake taji* lenye kujionyesha* la walevi wa Efraimu+
Na ua lenye kufifia la uzuri wake wenye utukufu,
Lenye kuwa kwenye kichwa cha bonde lenye mbolea la wale wenye wamelemewa na divai!
2 Angalia! Yehova iko* na mutu mwenye nguvu na mwenye uwezo.
Kama upepo wa mvua ya majiwe wenye mungurumo wa radi, zoruba yenye upepo mukali yenye kuharibu,
Kama zoruba yenye mungurumo wa maji ya garika yenye nguvu,
Atalitupa katika dunia kwa nguvu.
4 Na ua lenye kufifia la uzuri wake wenye utukufu
Lenye kuwa juu ya kichwa cha bonde lenye mbolea,
Litakuwa kama tini ya kwanza-kwanza mbele ya kipindi cha joto.
Wakati mutu anaiona, anaimeza wakati tu inakuwa katika mukono wake.
5 Siku hiyo Yehova wa majeshi atakuwa taji la utukufu na taji la muzuri la maua kwa watu wake wenye walibakia.+ 6 Na atakuwa roho ya haki kwa ule mwenye kukaa katika hukumu na chanzo cha nguvu kwa wale wenye kuzuia mashambulizi kwenye mulango mukubwa.+
7 Na hawa pia wanapotea kwa sababu ya divai;
Wanayumba-yumba kwa sababu ya vinywaji vyao vyenye kulewesha.
Kuhani na nabii wanapotea kwa sababu ya pombe;
Divai inawavuruga,
Na wanayumba-yumba kwa sababu ya pombe yao;
Maono yao yanafanya wapotee,
Na wanajikwaa katika hukumu.+
8 Kwa maana meza zao zimejaa matapiko machafu
—Yamejaa kila mahali.
9 Mutu atamufundisha nani ujuzi,
Na mutu atamufasiria nani ujumbe?
Je, ni wale wenye wametoka tu kuachishwa kunyonya,
Wale wenye wametoka tu kuondolewa kwenye maziwa?
10 Kwa maana ni “amri kisha amri, amri kisha amri,
Mustari kwa mustari, mustari kwa mustari,*+
Hapa kidogo, pale kidogo.”
11 Kwa hiyo atasema na watu hawa kupitia wale wenye kigugumizi* na kupitia luga ya kigeni.+ 12 Alikuwa amewaambia: “Hapa ndipo mahali pa kupumuzikia. Mwenye kuchoka apumuzike; hapa ndipo mahali pa kujiburudishia,” lakini walikataa kusikiliza.+ 13 Basi neno la Yehova litakuwa kwao:
“Amri kisha amri, amri kisha amri,
Mustari kwa mustari, mustari kwa mustari,*+
Hapa kidogo, pale kidogo,”
Ili wakati wanatembea,
Wajikwae na kuangukia nyuma
Na wavunjike na kunaswa na kukamatwa.+
14 Basi musikie neno la Yehova, ninyi wenye kujisifu
Ninyi watawala wa watu hawa wenye kuwa katika Yerusalemu,
15 Kwa maana munasema:
Wakati mafuriko yenye nguvu na ya kushitukia yatapita,
Hayatatufikia,
Kwa maana tumefanya uongo kuwa kimbilio letu
Na tumejificha katika udanganyifu.”+
16 Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
“Angalia, ninaweka katika Sayuni jiwe lenye limejaribiwa ili likuwe musingi,+
Kila mutu mwenye anaonyesha imani hataogopa.+
17 Na nitafanya haki kuwa kamba ya kupimia+
Na uadilifu* kuwa kifaa cha kusawazisha;*+
Na mvua ya majiwe itaharibu kimbilio la uongo,
Na maji yatazamisha mahali pa kujificha.
Wakati mafuriko yenye nguvu na ya kushitukia yatapita,
Yatawaponda ninyi.
19 Kila mara wakati yatapita,
Yatawafagilia ninyi mbali;+
Kwa maana yatapita asubui kisha asubui,
Muchana na usiku.
Woga mukubwa ndio utawafanya waelewe kile chenye kilisikiwa.”*
20 Kwa maana kitanda ni kifupi sana, mutu hawezi kujinyoosha juu yake,
Na kitu cha kujifunika chenye kusukwa ni chembamba, hakiwezi kumufunika mutu.
21 Kwa maana Yehova atasimama kama kwenye Mulima Perasimu,
Atainuka kama katika bonde* lenye kuwa karibu na Gibeoni,+
Ili afanye tendo lake—tendo lake la ajabu—
Na ili afanye kazi yake—kazi yake yenye haiko ya kawaida.+
Ili vifungo vyenu visikazwe zaidi,
Kwa maana nimesikia kutoka kwa Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, Yehova wa majeshi,
23 Mutege sikio na musikilize sauti yangu;
Mukaze uangalifu na musikilize kile ninasema.
24 Je, mulimaji anaendelea kulima muchana wote mbele ya kupanda mbegu?
Je, anaendelea kuchimbua na kuvunja udongo wake?+
25 Wakati amesawazisha udongo,
Je, hatawanye bizari nyeusi na kupanda bizari,
Na je, hapande ngano, mutama, na shayiri mahali pake,
Na ngano ya kusemeti+ kwenye mipaka?
27 Kwa maana bizari nyeusi haisagwe kwa kifaa cha kupiga-piga nafaka;+
Na gurudumu* la gari la kukokotwa halizungushwe juu ya bizari.
Lakini, bizari nyeusi inapigwa-pigwa kwa fimbo,
Na bizari kwa fimbo.
28 Je, mutu anaponda nafaka ili apate mukate?
Hapana, haendelee kuipiga-piga.+