Kwa Tito
2 Lakini, wewe endelea kusema mambo yenye kupatana na fundisho lenye faida.*+ 2 Wanaume wenye kuzeeka* wakuwe wenye kiasi, wenye kuchukua mambo kwa uzito, wenye akili ya muzuri, wenye nguvu katika imani, katika upendo, na katika uvumilivu. 3 Vilevile, wanamuke wenye kuzeeka* wanapaswa kuwa wenye kumuogopa Mungu, wasikuwe wachongezi, wasikuwe watumwa wa divai nyingi, wakuwe walimu wa mambo ya muzuri; 4 ili waweze kushauri* wanamuke vijana wapende bwana zao, wapende watoto wao, 5 wakuwe wenye akili ya muzuri, safi, wenye kufanya kazi katika nyumba zao,* wema, wenye kujinyenyekeza kwa bwana zao,+ ili neno la Mungu lisitukanwe.
6 Vilevile, endelea kutia moyo wanaume vijana wakuwe na akili ya muzuri,+ 7 ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa mufano muzuri wa matendo ya muzuri katika mambo yote. Fundisha mambo safi* kwa uzito wote,+ 8 ukitumia maneno yenye faida* yenye hayawezi kulaumiwa,+ ili kupatisha haya wale wenye kupinga, kwa sababu hawana jambo lolote la mubaya la kusema juu yetu.+ 9 Watumwa wajinyenyekeze kwa mabwana wao katika mambo yote,+ wajikaze kuwapendeza, wasiwajibu bila adabu, 10 wasikuwe wanawaiba,+ lakini wakuwe waaminifu kabisa, ili katika mambo yote wapambe mafundisho ya Mwokozi wetu, Mungu.+
11 Kwa sababu Mungu ameonyesha fazili zenye hazistahiliwe kwa kuletea watu wa namna zote wokovu.+ 12 Hiyo inatufundisha kukataa matendo ya kukosa kumuogopa Mungu+ na tamaa za ulimwengu na kuishi kwa akili ya muzuri na katika haki, na kwa ushikamanifu kwa Mungu katika mupangilio huu wa mambo,*+ 13 wakati tunangojea tumaini lenye furaha+ na kufunuliwa kwenye utukufu kwa Mungu mukubwa na kwa Mwokozi wetu, Yesu Kristo, 14 mwenye alijitoa kwa ajili yetu+ ili atukomboe*+ kutoka katika kila namna ya uvunjaji wa sheria na kujisafishia watu wenye kuwa mali yake ya pekee, wenye bidii kwa ajili ya matendo ya muzuri.+
15 Endelea kusema mambo haya na kutia moyo na kukaripia kwa mamlaka yote.+ Usiache mutu yeyote akuzarau.