Mezali
20 Divai ni muzihaki,+ pombe inamufanya mutu kuwa kichwa-nguvu;+
Kila mutu mwenye anapotoshwa navyo hana hekima.+
2 Kuogopesha sana kwa mufalme ni kama mungurumo wa simba;*+
Kila mutu mwenye anaamusha kasirani yake anatia uzima wake mwenyewe katika hatari.+
4 Muvivu halime wakati wa kipindi cha baridi,
Kwa hiyo atakuwa anaomba-omba katika kipindi cha mavuno wakati hatakuwa na kitu.*+
5 Mawazo* ya moyo wa mutu ni kama maji yenye kuenda chini sana,
Lakini mutu mwenye utambuzi anayashota.
6 Watu wengi wanatangaza upendo wao mushikamanifu,
Lakini ni nani anaweza kupata mutu muaminifu?
7 Mwenye haki anatembea katika uaminifu-mushikamanifu wake.+
Watoto* wake wenye kuja kisha yeye watakuwa na furaha.+
8 Wakati mufalme anakaa kwenye kiti cha ufalme ili kuhukumu,+
Anayungulula uovu wote kwa macho yake.+
12 Sikio lenye linasikia na jicho lenye linaona
—Yehova ameumba vyote viwili.+
13 Usipende usingizi, ukiupenda utakuwa maskini.+
Fungua macho yako, na utashiba mukate.+
14 “Haiko kizuri, haiko kizuri!” ni vile mwenye kununua anasema;
Kisha anaenda zake na kujisifu.+
16 Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;+
Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+
17 Mukate wenye ulipatikana kwa udanganyifu ni mutamu kwa mutu,
Lakini kisha, kinywa chake kitajaa majiwe ya kidogo-kidogo.+
19 Muchongezi anaenda huku na huku akifunua mazungumuzo ya siri;+
Usishirikiane na mutu mwenye anapenda kupiga porojo.*
20 Kila mutu mwenye analaani baba yake na mama yake,
Taa yake itazimwa wakati giza litaingia.+
21 Uriti wenye unapatikana kwanza kwa pupa
Mwishowe hautakuwa baraka.+
22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+
Tumainia Yehova,+ naye atakuokoa.+
25 Ni mutego kwa mutu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!”+
Na kisha tu wakati fulani anachunguza kile aliwekea naziri.+
27 Pumuzi ya mutu ni taa ya Yehova,
Inachunguza kabisa utu wake wa ndani sana.