Kutoka
3 Musa akakuwa muchungaji wa kundi la Yetro, baba-mukwe wake,+ kuhani wa Midiani. Wakati alikuwa anaongoza kundi kuelekea upande wa mangaribi wa jangwa, mwishowe akafika kwenye mulima wa Mungu wa kweli, kule Horebu.+ 2 Kisha malaika wa Yehova akamutokea katika mwali wa moto katikati ya muti mudogo wa miiba.+ Wakati Musa aliendelea kuangalia, akaona kwamba ule muti mudogo wa miiba ulikuwa unawaka moto, lakini ule muti mudogo wa miiba haukukuwa unateketea. 3 Kwa hiyo Musa akasema: “Niende karibu zaidi ili nichunguze jambo hili la ajabu kusudi nione sababu gani ule muti mudogo wa miiba hauteketee.” 4 Wakati Yehova aliona kwamba Musa anaenda karibu zaidi ili kuangalia, Mungu akamuita kutoka katikati ya ule muti mudogo wa miiba na kusema: “Musa! Musa!” naye akasema: “Mimi huyu.” 5 Kisha Mungu akasema: “Usikaribie. Vua viatu vyako kwenye miguu yako, kwa sababu mahali unasimama ni udongo mutakatifu.”
6 Akaendelea kusema: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka,+ na Mungu wa Yakobo.”+ Kisha Musa akaficha uso wake, kwa sababu aliogopa kumuangalia Mungu wa kweli. 7 Yehova akaongeza kusema: “Kwa kweli nimeona mateso ya watu wangu wenye wako Misri, na nimesikia kilio chao kwa sababu ya wale wenye kuwalazimisha kufanya kazi; ninajua muzuri maumivu yenye wako nayo.+ 8 Nitashuka ili kuwakomboa katika mukono wa Wamisri+ na kuwatosha katika inchi hiyo na kuwaleta kwenye inchi ya muzuri na kubwa, inchi yenye kutiririka maziwa na asali,+ eneo la Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.+ 9 Sasa angalia! Kilio cha watu wa Israeli kimenifikia, na nimeona pia namna Wamisri wanawakandamiza kwa ukali.+ 10 Sasa kuja, nitakutuma kwa Farao, na wewe utatosha watu wangu Waisraeli katika Misri.”+
11 Lakini, Musa akamuambia Mungu wa kweli: “Mimi niko nani ili niende kwa Farao na kutosha Waisraeli katika Misri?” 12 Basi Mungu akasema: “Nitakuwa pamoja na wewe,+ na hii ndiyo alama yenye itaonyesha kwamba ni mimi nilikutuma: Kisha wewe kutosha watu katika Misri, ninyi mutamutumikia* Mungu wa kweli kwenye mulima huu.”+
13 Lakini Musa akamuambia Mungu wa kweli: “Tuseme ninaenda kwa Waisraeli na kuwaambia, ‘Mungu wa mababu zenu amenituma kwenu,’ nao wakiniambia, ‘Jina lake ni nani?’+ Nitawaambia nini?” 14 Kwa hiyo Mungu akamuambia Musa: “Nitakuwa Kile Ninachagua* Kuwa.”*+ Na akaongeza kusema: “Utaambia Waisraeli hivi: ‘Nitakuwa amenituma kwenu.’”+ 15 Kisha Mungu akamuambia Musa tena:
“Utaambia Waisraeli hivi: ‘Yehova Mungu wa mababu zenu, Mungu wa Abrahamu,+ Mungu wa Isaka,+ na Mungu wa Yakobo,+ amenituma kwenu.’ Hilo ndilo jina langu milele,+ na ni vile ninapaswa kukumbukwa kutoka kizazi mupaka kizazi. 16 Sasa, uende ukusanye wazee wa Israeli na kuwaambia, ‘Yehova Mungu wa mababu zenu amenitokea, Mungu wa Abrahamu, Isaka, na Yakobo, na alisema: “Hakika nimewakazia uangalifu+ na nimeona mambo yenye wanawatendea katika Misri. 17 Kwa hiyo ninasema, nitawatosha katika mateso+ yenye munapata katika mikono ya Wamisri na nitawapeleka katika inchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori,+ Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.”’+
18 “Hakika watasikiliza sauti yako,+ na utaenda, wewe pamoja na wazee wa Israeli, kwa mufalme wa Misri, na mutamuambia, ‘Yehova Mungu wa Waebrania+ amezungumuza na sisi. Kwa hiyo, tafazali, acha tufanye safari ya siku tatu (3) katika jangwa ili tumutolee Yehova Mungu wetu zabihu.’+ 19 Lakini mimi mwenyewe ninajua muzuri kwamba mufalme wa Misri hatawapatia ruhusa ya kuenda kama halazimishwe na mukono wenye nguvu.+ 20 Kwa hiyo nitanyoosha mukono wangu na kupiga Misri kwa matendo yangu yote ya ajabu yenye nitafanya katika inchi hiyo, na kisha atawaruhusu muende.+ 21 Na nitafanya watu hawa wakubaliwe mbele ya macho ya Wamisri, na wakati mutaondoka, hamutaenda mikono wazi.+ 22 Kila mwanamuke anapaswa kumuomba jirani yake na mwanamuke mwenye kukaa katika nyumba yake vitu vya feza na vya zahabu na pia nguo, na mutavivalisha watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke, na mutanyanganya vitu vya Wamisri.”+