Isaya
Yehova aliniita mbele nizaliwe.*+
Tangu wakati nilikuwa katika tumbo la uzazi la mama yangu alitaja jina langu.
Alinifanya kuwa mushale wenye kunolewa.
Alinificha katika mufuko wake wa mishale.
3 Aliniambia: “Wewe ni mutumishi wangu, Ee Israeli,+
Mwenye kupitia yeye nitaonyesha utukufu wangu.”+
4 Lakini nilisema: “Nimefanya kazi ya jasho kwa bure.
Nilitumia nguvu zangu kwa ajili ya kitu cha kuwazia-wazia tu, kwa bure.
5 Na sasa Yehova, Yeye mwenye alinifanya tangu tumbo la uzazi ili nikuwe mutumishi wake,
Amesema kwamba nimurudishe Yakobo kwake,
Ili Israeli wakusanyike kwake.+
Nitatukuzwa mbele ya macho ya Yehova,
Na Mungu wangu atakuwa nguvu zangu.
6 Na alisema: “Haitoshe tu wewe kuwa mutumishi wangu
Ili kuinua makabila ya Yakobo
Na kurudisha wale wenye walilindwa wa Israeli.
7 Yehova, Mukombozi wa Israeli, Mutakatifu wake,+ amemuambia hivi ule mwenye kuzarauliwa,*+ ule mwenye kuchukiwa na taifa, mutumishi wa watawala:
“Wafalme wataona na watasimama,
Na wakubwa watainama
Kwa sababu ya Yehova, mwenye ni muaminifu,+
Mutakatifu wa Israeli, mwenye amekuchagua.”+
8 Yehova anasema hivi:
Na katika siku ya wokovu nilikusaidia;+
Niliendelea kukulinda ili nikutoe kuwa agano kwa ajili ya watu,+
Ili kutengeneza upya inchi,
Ili kuwafanya wariti uriti wao wenye kuwa ukiwa,+
Na wale wenye kuwa katika giza,+ ‘Mujionyeshe!’
Watakula majani pembeni ya barabara,
Malisho yao yatakuwa pembeni ya njia zenye kukanyangwa-kanyangwa.*
11 Nitafanya milima yangu yote kuwa njia,
Na njia zangu kubwa zitainuliwa.+
12 Angalia! Hawa wanakuja kutoka mbali,+
Na, angalia! hawa kutoka kaskazini na kutoka mangaribi,
Na hawa kutoka inchi ya Sinimu.”+
13 Mupige vigelegele vya shangwe, ninyi mbingu, na ushangilie, wewe dunia.+
Milima ichangamuke kwa vigelegele vya shangwe.+
14 Lakini Sayuni aliendelea kusema:
“Yehova ameniacha,+ na Yehova amenisahau.”+
15 Je, mwanamuke anaweza kumusahau mutoto wake mwenye kunyonya
Ao akose kusikilia huruma mwana wa tumbo lake la uzazi?
Hata kama wanamuke hawa wanasahau, mimi siwezi kukusahau hata kidogo.+
16 Angalia! Nimekuchora kwenye viganja vya mikono yangu.
Kuta zako ziko mbele yangu sikuzote.
17 Wana wako wanafanya haraka ili kurudia.
Wale wenye walikubomoa na kukuharibu wataondoka kwako.
18 Inua macho yako na uangalie kuzunguka pande zote.
Wote wanakusanyika pamoja.+
Wanakuja kwako.
“Kama vile hakika ninaishi,” ni vile Yehova anasema,
“Utavaa hao wote kama mapambo,
Na utajifunga hao kama vile bibi-arusi anafanya.
19 Hata kama maeneo yako yaliharibiwa na kuachwa ukiwa na inchi yako ilikuwa mabomoko,+
Sasa itakuwa kidogo sana kwa wale wenye kukaa kule,+
20 Wana wenye walizaliwa wakati ulikuwa umekosewa watoto watasema hivi katika masikio yako:
‘Mahali hapa ni pa kidogo sana kwangu.
Unipatie nafasi zaidi ili nikae hapa.’+
21 Na utasema katika moyo wako,
‘Ni nani amekuwa baba mwenye alizaa hawa kwa ajili yangu,
Kwa kuwa niko mwanamuke mwenye alikosewa watoto na niko tasa,
Mwenye alipelekwa katika uhamisho na kufungwa?
Ni nani alilea hawa?+
Angalia! Nilikuwa nimeachwa peke yangu.+
Basi hawa wametoka wapi?’”+
22 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
Watakuinamia nyuso chini+
Na kulambula mavumbi ya miguu yako,+
Na utalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova;
Wale wenye kunitumainia hawatapatishwa haya.”+
24 Je, wale wenye wamekwisha kukamatwa wanaweza kuchukuliwa kutoka kwa mutu mwenye nguvu,
Ao, je, watu wenye walikamatwa mateka wa mutu muonevu wanaweza kukombolewa?
25 Lakini Yehova anasema hivi:
“Hata watu wenye walikamatwa mateka wa mutu mwenye nguvu watachukuliwa,+
Na wale wenye walikamatwa na mutu muonevu watakombolewa.+
Nitapinga wale wenye kukupinga,+
Na nitaokoa wana wako mwenyewe.
26 Nitafanya wale wenye kukutesa wakule nyama yao wenyewe,
Na watalewa damu yao wenyewe kama vile divai tamu.