Cha Kwanza cha Wafalme
15 Katika mwaka wa kumi na munane (18) wa Mufalme Yeroboamu+ mwana wa Nebati, Abiyamu akakuwa mufalme juu ya Yuda.+ 2 Alitawala kwa miaka tatu (3) katika Yerusalemu. Jina la mama yake lilikuwa Maaka,+ mujukuu wa Abishalomu. 3 Aliendelea kutembea katika zambi zote zenye baba yake alitenda kabla yake, na moyo wake haukukuwa kamili* kumuelekea Yehova Mungu wake kama moyo wa Daudi babu yake. 4 Hata hivyo, kwa ajili ya Daudi,+ Yehova Mungu wake alimupatia taa katika Yerusalemu+ kwa kumusimamisha mwana wake kisha yeye na kwa kufanya Yerusalemu iendelee kuwa. 5 Kwa maana Daudi alifanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova, na hakugeuka na kuacha jambo lolote lenye Yeye alikuwa amemuamuru sikuzote za maisha yake, isipokuwa katika jambo la Uria Muhiti.+ 6 Na kulikuwa vita kati ya Rehoboamu na Yeroboamu siku zote za maisha yake.+
7 Na mambo mengine ya historia ya Abiyamu, yote yenye alifanya, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda?+ Kulikuwa pia vita kati ya Abiyamu na Yeroboamu.+ 8 Kisha Abiyamu akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake, na wakamuzika katika Muji wa Daudi; na Asa+ mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.+
9 Katika mwaka wa makumi mbili (20) wa Mufalme Yeroboamu wa Israeli, Asa alianza kutawala juu ya Yuda. 10 Alitawala katika Yerusalemu kwa miaka makumi ine na moja (41). Jina la tate* yake mwanamuke lilikuwa Maaka,+ mujukuu wa Abishalomu. 11 Asa alifanya mambo yenye yalikuwa sawa mbele ya macho ya Yehova,+ kama Daudi babu yake. 12 Alifukuza wanaume makahaba wa hekalu kutoka katika inchi+ na alitosha sanamu zote zenye kuchukiza* zenye mababu zake walikuwa wametengeneza.+ 13 Aliondoa hata Maaka+ tate* yake mwanamuke kutoka kwenye cheo chake cha malkia mama ya mufalme,* kwa sababu alikuwa ametengeneza sanamu chafu kwa ajili ya ibada ya muti mutakatifu.* Asa akakata sanamu yake chafu+ na kuiteketeza kwa moto katika Bonde la Kidroni.+ 14 Lakini mahali pa juu hapakuondolewa.+ Hata hivyo, moyo wa Asa ulikuwa kamili* kumuelekea Yehova maisha yake yote.* 15 Na alileta vitu vyenye yeye na baba yake walikuwa wamefanya kuwa vitakatifu katika nyumba ya Yehova—feza, zahabu, na vyombo mbalimbali.+
16 Kulikuwa vita yenye kuendelea kati ya Asa na Baasha+ mufalme wa Israeli. 17 Basi Mufalme Baasha wa Israeli alipanda ili kushambulia Yuda na akaanza kujenga* Rama+ ili kuzuia mutu yeyote asitoke inje ao kuingia ndani kwa* Mufalme Asa wa Yuda.+ 18 Halafu Asa akakamata feza yote na zahabu yenye ilikuwa imebakia katika hazina za nyumba ya Yehova na hazina za nyumba ya mufalme na kuvitia katika mukono wa watumishi wake. Kisha Mufalme Asa akawatuma kwa Ben-hadadi mwana wa Tabrimoni mwana wa Hezioni, mufalme wa Siria,+ mwenye alikuwa anaishi katika Damasko, kwa kusema: 19 “Kuko mapatano* kati yangu na wewe na kati ya baba yangu na baba yako. Ninakutumia zawadi ya feza na zahabu. Kuja, vunja mapatano yako* na Mufalme Baasha wa Israeli, ili aondoke kwangu.” 20 Ben-hadadi akamusikiliza Mufalme Asa na akatuma wakubwa wa majeshi yake ili kushambulia miji ya Israeli, na wakapiga Iyoni,+ Dani,+ Abel-bet-maaka, Kinereti yote, na inchi yote ya Naftali. 21 Wakati Baasha alisikia habari hiyo, mara moja akaacha kujenga* Rama na akaendelea kuishi katika Tirsa.+ 22 Kisha Mufalme Asa akaita Yuda wote—hakuna mwenye aliachwa—na wakabeba majiwe na mbao za Rama zenye Baasha alikuwa anatumia ili kujenga, na Mufalme Asa akazitumia kujenga* Geba+ katika Benyamini, na Mispa.+
23 Na mambo mengine ya historia ya Asa, ukubwa wake wote na mambo yote yenye alifanya na miji yenye alijenga,* je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Yuda? Lakini katika uzee wake alipata ugonjwa katika miguu yake.+ 24 Kisha Asa akalalishwa na kupumuzika pamoja na mababu zake na akazikwa pamoja nao katika Muji wa Daudi babu yake; na Yehoshafati+ mwana wake akakuwa mufalme pa nafasi yake.
25 Nadabu+ mwana wa Yeroboamu akakuwa mufalme juu ya Israeli katika mwaka wa pili wa Mufalme Asa wa Yuda, na alitawala juu ya Israeli kwa miaka mbili. 26 Aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova na alitembea katika njia ya baba yake+ na katika zambi yake yenye alifanya Israeli watende.+ 27 Baasha mwana wa Ahiya wa nyumba ya Isakari akafanya mupango mubaya juu yake, na Baasha akamupiga na kumuua kule Gibetoni,+ yenye ilikuwa ya Wafilisti, wakati Nadabu na Israeli wote walikuwa wamezunguka Gibetoni kwa ajili ya vita. 28 Kwa hiyo Baasha akamuua katika mwaka wa tatu (3) wa Mufalme Asa wa Yuda na akakuwa mufalme pa nafasi yake. 29 Na wakati tu alikuwa mufalme, alipiga na kuua nyumba yote ya Yeroboamu. Hakuacha mutu yeyote wa Yeroboamu mwenye kupumua abakie; alifanya waharibiwe kulingana na neno la Yehova lenye alikuwa amesema kupitia mutumishi wake Ahiya Mushilo.+ 30 Ilikuwa vile kwa sababu ya zambi zenye Yeroboamu alikuwa ametenda na kufanya Israeli watende na kwa sababu alikuwa amemukasirisha sana Yehova Mungu wa Israeli. 31 Na mambo mengine ya historia ya Nadabu, yote yenye alifanya, je, hayaandikwe katika kitabu cha historia ya nyakati za wafalme wa Israeli? 32 Na kulikuwa vita yenye kuendelea kati ya Asa na Mufalme Baasha wa Israeli.+
33 Katika mwaka wa tatu (3) wa Mufalme Asa wa Yuda, Baasha mwana wa Ahiya akakuwa mufalme katika Tirsa juu ya Israeli yote na alitawala kwa miaka makumi mbili na ine (24).+ 34 Lakini aliendelea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova,+ na alitembea katika njia ya Yeroboamu na katika zambi yake yenye alifanya Israeli watende.+