Yobu
12 Kisha Yobu akajibu:
2 “Kwa kweli ninyi ndio watu wenye kujua mambo,*
Na hekima itakufa pamoja na ninyi!
3 Lakini mimi pia niko na uelewaji.*
Mimi siko mudogo kuliko ninyi.
Ni nani mwenye hajue mambo haya?
Mwenye haki na mwenye hana lawama ni kitu cha kuchekwa.
5 Mutu mwenye hana mahangaiko anazarau musiba,
Anafikiri kwamba musiba unafikia tu watu wenye miguu ya kuyumba-yumba.*
6 Mahema ya wanyanganyi yako na amani,+
Na wale wenye kumuchokoza Mungu wako salama,+
Wale wenye kuwa na mungu wao katika mikono yao.
7 Lakini, tafazali, uliza wanyama, nao watakufundisha;
Pia ndege wa anga, nao watakuambia.
8 Ao uchunguze* dunia, nayo itakufundisha;
Na samaki wa bahari watakutangazia jambo hilo.
9 Ni nani kati yao mwenye hajue
Kwamba mukono wa Yehova umefanya hayo?
12 Je, haiko wazee ndio wenye kuwa na hekima,+
Na je, uelewaji haukuje kwa sababu ya kuishi siku nyingi?
14 Akibomoa kitu, hakiwezi kujengwa tena;+
Kile amefunga, hakuna mutu anaweza kufungua.
16 Yeye iko* na nguvu na hekima yenye kutenda;+
Mwenye kudanganywa na mwenye kudanganya wote ni wake;
17 Anafanya washauri watembee miguu wazi,*
Na anafanya waamuzi kuwa wapumbavu.+
19 Anafanya makuhani watembee miguu wazi,+
Na anapindua wale wenye kuwa imara kabisa katika mamlaka;+
20 Ananyamazisha washauri wenye kutumainiwa
Na anaondoa hekima ya wazee;
21 Anamwanga zarau juu ya watu wenye vyeo,+
Na kufanya wenye nguvu kuwa wazaifu;*
22 Anafunua mambo mazito yenye kuwa katika giza,+
Na anafanya giza nzito kuwa mwangaza;
23 Anafanya mataifa yakuwe na nguvu ili ayaharibu;
Anafanya mataifa yakuwe makubwa ili ayapeleke katika uhamisho.