Waamuzi
2 Kisha malaika wa Yehova+ akapanda kutoka Gilgali+ na kuenda Bokimu na kusema: “Niliwatosha Misri na kuwaleta katika inchi yenye niliapia mababu zenu.+ Pia nilisema, ‘Sitavunja hata kidogo agano langu pamoja na ninyi.+ 2 Na ninyi kwa upande wenu, musifanye agano pamoja na wakaaji wa inchi hii,+ mubomoe mazabahu zao.’+ Lakini hamukutii sauti yangu.+ Sababu gani mumefanya hivi? 3 Ndiyo maana nilisema pia, ‘Sitawafukuza mbele yenu,+ na watakuwa mutego kwenu,+ na miungu yao itawapoteza.’”+
4 Wakati malaika wa Yehova aliambia Waisraeli wote maneno hayo, watu wakaanza kulia kwa sauti kubwa. 5 Kwa hiyo wakapatia mahali pale jina Bokimu,* na wakamutolea Yehova zabihu pale.
6 Wakati Yoshua aliruhusu watu waende, kila Mwisraeli akaenda kwenye uriti wake ili kukaa katika inchi.+ 7 Watu wakaendelea kumutumikia Yehova siku zote za Yoshua na siku zote za wazee wenye waliendelea kuishi kisha Yoshua kufa na wenye walikuwa wameona mambo yote makubwa yenye Yehova alitendea Israeli.+ 8 Kisha Yoshua mwana wa Nuni, mutumishi wa Yehova, akakufa na miaka mia moja na kumi (110).+ 9 Basi wakamuzika katika eneo la uriti wake kule Timnat-heresi,+ katika eneo lenye milima la Efraimu, upande wa kaskazini wa Mulima Gaashi.+ 10 Na watu wote wa kizazi hicho wakakusanywa pamoja na mababu zao,* na kizazi kingine kikatokea kisha wao chenye hakikumujua Yehova wala mambo yenye alikuwa amefanyia Israeli.
11 Basi Waisraeli wakafanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova na wakatumikia* Mabaali.+ 12 Basi wakamuacha Yehova, Mungu wa baba zao, mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri.+ Na wakafuata miungu mingine, miungu ya vikundi vya watu vyenye viliwazunguka pande zote,+ na wakaiinamia na kumukasirisha Yehova.+ 13 Wakamuacha Yehova na wakatumikia Baali na sanamu za Ashtoreti.+ 14 Basi kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli, akawatia katika mukono wa wanyanganyi wenye walinyanganya vitu vyao.+ Akawauzisha katika mukono wa maadui wenye waliwazunguka,+ na hawakuweza tena kusimama mbele ya maadui wao.+ 15 Kila mahali walienda, mukono wa Yehova ulikuwa juu yao ili kuwaletea musiba,+ kama vile Yehova alikuwa amesema na kama vile Yehova alikuwa amewaapia,+ na wakateseka sana.+ 16 Basi Yehova alikuwa anainua waamuzi wenye walikuwa wanawaokoa katika mukono wa wanyanganyi wao.+
17 Lakini walikataa kusikiliza hata waamuzi hao na walifanya uasherati na miungu mingine na kuiinamia. Waliacha haraka njia yenye mababu zao walikuwa wametembea ndani yake, wenye walikuwa wametii amri za Yehova.+ Hawakufanya vile. 18 Kila wakati wenye Yehova aliwainulia waamuzi,+ Yehova alikuwa pamoja na muamuzi huyo na alikuwa anawaokoa katika mukono wa maadui wao siku zote za muamuzi huyo; kwa maana Yehova aliwasikilia huruma*+ kwa sababu ya kilio chao cha maumivu chenye kilitokezwa na wale wenye waliwakandamiza+ na wale wenye walikuwa wanawatendea mubaya.
19 Lakini wakati muamuzi huyo alikufa, walikuwa wanageuka na kutenda kwa upotovu zaidi kuliko baba zao kwa kufuata miungu mingine, kwa kuitumikia na kuiinamia.+ Hawakuacha matendo yao na tabia yao ya kuwa kichwa-nguvu. 20 Mwishowe kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ na akasema: “Kwa sababu taifa hili limevunja agano langu+ lenye nilifanya pamoja na mababu zao na wamekataa kunitii,+ 21 mimi pia sitafukuza hata taifa moja kati ya mataifa yenye Yoshua aliacha wakati alikufa.+ 22 Itakuwa vile ili kujaribu Israeli kama watashika njia ya Yehova+ na kutembea katika njia hiyo kama vile baba zao walifanya.” 23 Kwa hiyo Yehova akaruhusu mataifa hayo yabakie. Hakuyafukuza haraka, wala hakuyatia katika mukono wa Yoshua.