Zaburi
2 Ni nani anaweza kutangaza kikamili matendo ya Yehova yenye nguvu
Ao kutangaza matendo yake yote yenye kustahili sifa?+
3 Wenye furaha ni wale wenye wanatenda haki,
Wenye sikuzote wanatenda mambo yenye kuwa sawa.+
4 Unikumbuke, Ee Yehova, wakati unaonyesha watu wako wema.*+
Unitunze kupitia matendo yako ya wokovu,
5 Ili nifurahie wema wenye unaonyesha wachaguliwa wako,+
Ili nishangilie pamoja na taifa lako,
Ili nikusifu kwa majivuno* pamoja na uriti wako.
7 Mababu zetu kule Misri hawakuona kazi zako za ajabu kuwa za maana.*
Hawakukumbuka upendo wako mwingi mushikamanifu,
Lakini waliasi kwenye bahari, pembeni ya Bahari Nyekundu.+
9 Alikemea Bahari Nyekundu, na ikakauka;
Aliwaongoza katika sehemu za chini kabisa kama vile katika jangwa;+
10 Aliwaokoa kutoka katika mukono wa adui yao+
Na aliwakomboa kutoka katika mukono wa adui.+
13 Lakini walisahau haraka mambo yenye alifanya;+
Hawakungojea shauri lake.
17 Kisha dunia ikafunguka na kumumeza Datani
Na kufunika wale wenye walikusanyika pamoja na Abiramu.+
18 Moto uliwaka kati ya kikundi chao;
Mwali wa moto uliteketeza waovu.+
19 Walitengeneza kitoto-dume cha ngombe kule Horebu
Na kuinamia sanamu ya metali;*+
20 Pa nafasi ya utukufu wangu
Walitia mufano wa ngombe-dume mwenye kula majani.+
21 Walimusahau Mungu+ Mwokozi wao,
Mwenye alifanya mambo makubwa katika Misri,+
22 Kazi za ajabu katika inchi ya Hamu,+
Matendo yenye kuogopesha sana kwenye Bahari Nyekundu.+
23 Alikuwa karibu kuagiza waharibiwe,
Lakini Musa, muchaguliwa wake, akamulilia*
Ili kuzuia kasirani yake yenye kuharibu.+
26 Kwa hiyo akainua mukono wake na kuapa kuwahusu
Kwamba angefanya waanguke katika jangwa;+
27 Angefanya wazao wao waanguke kati ya mataifa,
Na angewasambaza katika inchi mbalimbali.+
30 Lakini wakati Finehasi alisimama na kuingilia kati,
Pigo hilo likasimamishwa.+
31 Na jambo hilo likahesabiwa kwake kuwa haki
Katika vizazi vyote milele.+
33 Walitia uchungu roho yake,
Naye akaongea bila kufikiri kupitia midomo yake.+
37 Walikuwa wanatoa watoto wao wanaume kuwa zabihu
Na watoto wao wanamuke kwa pepo wachafu.+
38 Waliendelea kumwanga damu yenye haina kosa,+
Damu ya watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke
Wenye walitoa kuwa zabihu kwa sanamu za Kanaani;+
Na inchi ikachafuliwa kupitia umwangaji wa damu.
39 Wakakuwa wachafu kwa sababu ya kazi zao;
Walifanya ukahaba wa kiroho kupitia matendo yao.+
40 Kwa hiyo kasirani ya Yehova ikawaka juu ya watu wake,
Na akachukia sana uriti wake.
42 Maadui wao waliwakandamiza,
Na wakatiishwa chini ya nguvu zao.*
43 Aliwaokoa mara nyingi,+
Lakini walikuwa wanaasi na kukosa kutii,+
Na walikuwa wanashushwa chini kwa sababu ya kosa lao.+
45 Kwa ajili yao alikuwa anakumbuka agano lake,
Na alikuwa anasikia huruma,* akichochewa na upendo wake mwingi mushikamanifu.+
46 Alikuwa anawafanya wasikiliwe huruma
Na wale wote wenye waliwakamata mateka.+
47 Utuokoe, Ee Yehova Mungu wetu,+
Na kutukusanya kutoka katika mataifa+
Ili tushukuru jina lako takatifu
Na acha watu wote waseme, “Amina!”*
Mumusifu Yah!*