MIKA
1 Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Mika*+ wa Moresheti, katika siku za Yotamu,+ Ahazi,+ na Hezekia,+ wafalme wa Yuda,+ lenye alipata katika maono kuhusu Samaria na Yerusalemu:
2 “Musikie, ninyi vikundi vyote vya watu!
Sikiliza, Ee dunia na vitu vyote vyenye kujaa ndani yako,
Na Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova akuwe shahidi juu yenu,+
—Yehova katika hekalu lake takatifu.
3 Kwa maana angalia! Yehova anatoka mahali pake;
Atashuka na kukanyanga mahali kwenye kuinuka katika dunia.
4 Milima itayeyuka chini yake,+
Na mabonde* yatapasuka
Kama nta* karibu na moto,
Kama maji yenye kumwangwa kwenye muteremuko mukali.
Uasi wa Yakobo ni nini?
Haiko Samaria?+
Mahali pa juu pa Yuda ni nini?+
Haiko Yerusalemu?
6 Nitafanya Samaria kuwa rundo la mabomoko katika shamba,
Mahali pa kupanda mizabibu;
Nitatupa* majiwe yake katika bonde,
Na nitafunua misingi yake.
7 Sanamu zake zote za kuchongwa zitavunjwa-vunjwa,+
Na zawadi zote zenye alilipwa kwa sababu ya ukahaba wake zitateketezwa* kwa moto.+
Nitaharibu sanamu zake zote.
Kwa sababu alizikusanya kutokana na malipo ya ukahaba,
Na zitakuwa tena malipo ya makahaba.”
Nitalia kama mbweha,
Na kuomboleza kama mbuni.
Pigo hilo limeenea mupaka kwenye mulango mukubwa wa watu wangu, mupaka Yerusalemu.+
10 “Musitangaze jambo hili katika Gati;
Musilie hata kidogo.
Katika Bet-afra* mujizungushe-zungushe katika mavumbi.
11 Muende mukiwa uchi na wenye haya, Enyi wakaaji* wa Shafiri.
Wakaaji wa Saanani hawajatokea.*
Katika Bet-ezeli watu watalia, itaondoa tegemeo lao kutoka kwenu.
12 Kwa sababu wakaaji wa Maroti wamengojea* mambo ya muzuri,
Lakini mambo ya mubaya yameshuka kutoka kwa Yehova mupaka kwenye mulango mukubwa wa Yerusalemu.
13 Mufunge gari kwenye kikundi cha farasi, Enyi wakaaji* wa Lakishi.+
Ninyi ndio muliingiza binti ya Sayuni katika zambi,
Kwa maana uasi wa Israeli umepatikana ndani yenu.+
14 Kwa hiyo mutapatia Moreshet-gati zawadi za kuagana.*
Nyumba za Akzibu+ zilikuwa kitu cha kudanganya kwa wafalme wa Israeli.
15 Bado nitawaletea mushindi,*+ Enyi wakaaji* wa Maresha.+
Utukufu wa Israeli utafika Adulamu.+
16 Mujifanyie vipara na munyoe nywele zenu kwa sababu ya watoto wenu wapendwa.
Mujifanyie vipara kama vya tai,
Kwa maana wamepelekwa mbali na wewe, katika uhamisho.”+
2 “Ole wao wenye kupanga mambo yenye kuumiza,
Wale wenye kupanga maovu katika vitanda vyao!
Na wakati mwangaza wa asubui unatokea wanayatimiza,
Kwa sababu wako na uwezo wa kufanya vile.+
2 Wanatamani mashamba na kuyanyanganya;+
Pia nyumba, na kuzikamata;
Na wanamunyanganya mutu nyumba yake kwa udanganyifu,+
Na uriti wake.
3 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:
‘Angalia, ninapanga kuletea familia hii musiba+ wenye hamutaepuka.*+
Hamutatembea tena kwa kiburi,+ kwa sababu ni wakati wa musiba.+
Watasema: “Tumeharibiwa kabisa!+
Alifanya sehemu ya watu wangu iende katika mikono ya watu wengine—ona namna anaiondoa kwangu!+
Anagawia mashamba yetu mutu mwenye haiko muaminifu.”
5 Kwa hiyo hakuna mwenye atanyoosha kamba ya kupimia,
Na kutugawia inchi kwa kura katika kutaniko la Yehova.
6 “Muache kuhubiri!” ni vile wanahubiri,
“Hawapaswe kuhubiri mambo haya;
Hatutafezeheshwa!”
7 Watu wanasema, Ee nyumba ya Yakobo:
“Roho ya Yehova imeshindwa kuvumilia?
Haya ndiyo matendo yake?”
Je, maneno yangu hayaletee faida wenye kutembea kwa unyoofu?
8 Lakini hivi karibuni watu wangu wamesimama kama adui.
Munaondoa waziwazi mapambo yenye kupendeza pamoja na* nguo,
Juu ya watu wenye kupita bila wasiwasi, kama wale wenye kutoka kwenye vita.
9 Munaondoa wanamuke wa watu wangu katika nyumba zao za muzuri;
Munakamata utukufu wangu kutoka kwa watoto wao milele.
10 Musimame na muende zenu, kwa sababu hapa haiko mahali pa kupumuzikia.
Kwa sababu ya uchafu,+ kutakuwa uharibifu, uharibifu mukubwa.+
11 Kama mutu anafuata upepo na udanganyifu, na kusema uongo huu:
“Nitawahubiria juu ya divai na pombe,”
Basi angekuwa tu muhubiri wa watu hawa!+
12 Kwa kweli nitawakusanya ninyi wote, Ee Yakobo;
Kwa kweli nitakusanya pamoja Waisraeli wote wenye kubakia.+
Nitawaunganisha, kama kondoo katika zizi,*
Kama kundi katika malisho yake;+
Kutakuwa makelele ya watu.’+
13 Mwenye kutoboa tundu ataenda mbele yao;
Na watatoboa tundu na kupita katika mulango mukubwa na kuenda inje kupitia mulango huo.+
Mufalme wao atapita mbele yao,
Na Yehova atawaongoza.”+
Munapaswa kujua yenye kuwa haki, haiko vile?
2 Lakini munachukia mambo ya muzuri+ na munapenda mambo ya mubaya;+
Munachuna watu wangu ngozi na kuondoa nyama kwenye mifupa yao.+
3 Pia munakula nyama ya watu wangu+
Na kuwachuna ngozi,
Munavunja mifupa yao, na kuiponda-ponda,+
Kama kitu chenye kupikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.
4 Wakati huo watamuita Yehova awasaidie,
Lakini hatawajibu.
5 Yehova anasema hivi juu ya manabii wenye kupotosha watu wake,+
Wenye kutangaza ‘Amani!’+ wakati wanatafuna kwa meno yao,+
Lakini wenye kutangaza* vita juu ya mutu yeyote mwenye hatie kitu katika vinywa vyao:
Jua litashuka juu ya manabii,
Na muchana utageuka kuwa giza kwao.+
Wote watafunika masharubu yao,*
Kwa maana hakuna jibu kutoka kwa Mungu.’”
8 Lakini mimi, ninajaa nguvu kupitia roho ya Yehova,
Na haki na uwezo,
Ili nimuambie Yakobo uasi wake na Israeli zambi yake.
9 Tafazali musikie jambo hili, ninyi vichwa vya nyumba ya Yakobo
Na ninyi makamanda wa nyumba ya Israeli,+
Wenye kuchukia haki na kupotosha mambo yote yenye kunyooka,+
10 Wenye kujenga Sayuni kwa kumwanga damu na Yerusalemu kwa ukosefu wa haki.+
11 Viongozi wake* wanapokea rushwa* ili kuhukumu,+
Makuhani wake wanafundisha ili wapate malipo,+
Na manabii wake wanafanya uaguzi ili wapate feza.+
Na hata hivyo wanamutegemea Yehova,* kwa kusema:
“Je, Yehova haiko pamoja na sisi?+
Hakuna musiba wenye utatupata.”+
12 Basi kwa sababu yenu,
Sayuni italimwa kama shamba,
Yerusalemu itakuwa marundo ya mabomoko,+
Na mulima wa Nyumba* utakuwa kama mahali pa juu katika pori.*+
4 Katika kipindi cha mwisho cha zile siku,*
Mulima wa nyumba ya Yehova+
Utawekwa imara kabisa kwenye kichwa cha milima,
Na utainuliwa juu ya vilima,
Na vikundi vya watu vitamiminika kule.+
2 Na mataifa mengi yataenda na kusema:
“Mukuje, tupande kwenye mulima wa Yehova
Na kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo.+
Atatufundisha njia zake,
Na tutatembea katika njia zake.”
Kwa maana sheria itatoka* Sayuni,
Na neno la Yehova litatoka Yerusalemu.
3 Atafanya hukumu kati ya vikundi vingi vya watu+
Na kunyoosha* mambo kuhusu mataifa yenye nguvu yenye kuwa mbali.
Taifa halitainua upanga juu ya taifa,
Wala hawatajifunza vita tena.+
4 Watakaa,* kila mutu chini ya muzabibu wake na chini ya muti wake wa tini,+
Na hakuna mutu mwenye atawaogopesha,+
Kwa maana kinywa cha Yehova wa majeshi kimesema.
5 Kwa maana vikundi vya watu vitatembea, kila mutu katika jina la mungu wake,
Lakini sisi tutatembea katika jina la Yehova Mungu wetu+ milele na milele.
6 “Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,
“Nitakusanya ule mwenye alikuwa anatembea kwa kukokota muguu,*
Na kukusanya mwenye kutawanyika,+
Pamoja na wale wenye nilitendea kwa ukali.
7 Ule mwenye alikuwa anatembea kwa kukokota muguu* nitamufanya kuwa baki,+
Na ule mwenye alikuwa amepelekwa mbali nitamufanya kuwa taifa lenye nguvu;+
Na Yehova atakuwa mufalme juu yao kwenye Mulima Sayuni,
Kuanzia sasa na milele.
8 Sasa wewe, Ee munara wa kundi,
Kilima cha binti ya Sayuni,+
Utakuja kwako, ndiyo, utawala wa kwanza* utakuja kwako,+
Ufalme wa binti ya Yerusalemu.+
9 Sasa sababu gani unalalamika kwa sauti kubwa?
Je, hauna mufalme,
Ao mushauri wako ameangamia,
Na hivyo maumivu yamekushika kama mwanamuke mwenye kuzaa?+
10 Ukuwe katika maumivu makali na ulie kwa maumivu, Ee binti ya Sayuni,
Kama mwanamuke mwenye kuzaa,
Kwa kuwa sasa utatoka katika muji na kukaa katika mashamba.
Utaenda mupaka Babiloni,+
Na utakombolewa kule;+
Kule Yehova atakununua tena kutoka katika mukono wa maadui wako.+
11 Sasa mataifa mengi yatakusanyika ili kukushambulia;
Yatasema, ‘Muache achafuliwe,
Na muache macho yetu yaone namna jambo hili litapata Sayuni.’
12 Lakini hawajue mawazo ya Yehova,
Hawaelewe kusudi* lake;
Kwa maana atawakusanya kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka kama nafaka yenye imetoka kuvunwa.
13 Simama na upige-pige nafaka, Ee binti ya Sayuni;+
Kwa maana nitabadilisha pembe zako kuwa chuma,
Na nitabadilisha kwato* zako kuwa shaba,
Na utaponda-ponda vikundi vingi vya watu.+
Utamutolea Yehova faida yao yenye haiko ya haki,
Na mali zao utazipatia Bwana wa kweli wa dunia yote.”+
Wanamupiga muamuzi wa Israeli kwenye shavu kwa fimbo.+
2 Na wewe, Ee Betlehemu Efrata,+
Mwenye kuwa mudogo sana kati ya maelfu ya* Yuda,
Mwenye atatawala katika Israeli kwa ajili yangu atatokea kwako,+
Asili yake ni ya kuanzia nyakati za zamani, kuanzia siku za zamani sana.
3 Kwa hiyo atatia watu wake katika mikono ya adui
Mupaka wakati ule mama mwenye kuzaa atakuwa amezaa.
Na ndugu zake wenye walibakia watarudia kwa watu wa Israeli.
Kama Mwashuru atashambulia inchi yetu na kukanyanga minara yetu yenye ngome,+
Tutainua wachungaji saba (7) ili wapambane naye, ndiyo, wakubwa* munane (8) kutoka kati ya wanadamu.
Na atatuokoa kutoka kwa Mwashuru,+
Wakati atashambulia inchi yetu na kuingia katika eneo letu.
7 Na wenye walibakia wa Yakobo watakuwa katikati ya vikundi vingi vya watu
Kama umande kutoka kwa Yehova,
Kama matone ya mvua juu ya mimea
Yenye hayamutumainie mutu
Wala kungojea wana wa binadamu.
8 Na wenye walibakia wa Yakobo watakuwa kati ya mataifa,
Katikati ya vikundi vingi vya watu,
Kama simba kati ya wanyama wa pori,
Kama mwana-simba* kati ya makundi ya kondoo,
Mwenye anapita na kurukia na kupasua vipande-vipande;
Na hakuna mwenye anaweza kuwaokoa.
9 Mukono wako utainuka juu ya wapinzani wako,
Na maadui wako wote wataharibiwa.”
10 “Katika siku hiyo,” ni vile Yehova anasema,
“Nitaondoa farasi wenu katikati yenu na kuharibu magari yenu.
11 Nitaharibu miji ya inchi yenu
Na kubomoa ngome zenu zote.
13 Nitaharibu kutoka katikati yenu sanamu zenu za kuchongwa na nguzo zenu,
Na hamutainamia tena kazi ya mikono yenu.+
15 Kwa hasira na kasirani kali nitalipiza kisasi
Juu ya mataifa yenye hayakutii.”
6 Tafazali, musikie jambo lenye Yehova anasema.
Musimame, mupeleke kesi ya hukumu mbele ya milima,
Na vilima visikie sauti yenu.+
2 Musikie kesi ya hukumu ya Yehova, Enyi milima,
Ninyi misingi imara ya dunia,+
Kwa maana Yehova iko* na kesi ya hukumu pamoja na watu wake;
Atabishana na Israeli:+
3 “Watu wangu, nimewafanya nini?
Nimewachokesha namna gani?+
Mushuhudie juu yangu.
4 Kwa maana niliwatosha katika inchi ya Misri,+
Niliwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa;+
Nilituma Musa, Haruni, na Miriamu mbele yenu.+
5 Watu wangu, tafazali, mukumbuke jambo lenye Mufalme Balaki wa Moabu alipendekeza,+
Na jambo lenye Balaamu mwana wa Beori alimujibu+
—Mambo yenye yalitokea kuanzia Shitimu+ mupaka Gilgali+—
Ili mujue matendo yenye haki ya Yehova.”
6 Nitakuja na nini mbele ya Yehova?
Nitainama na nini mbele ya Mungu mwenye kuwa juu?
Je, nikuje mbele yake na matoleo mazima ya kuteketezwa,
Na vitoto-dume vya ngombe vya mwaka mumoja?+
7 Je, Yehova atafurahia maelfu ya kondoo-dume,
Na makumi ya maelfu ya mito ya mafuta?+
Je, nitoe mwana wangu muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya uasi wangu,
8 Ee mwanadamu, amekuambia mambo mema.
Na Yehova anataka* ufanye nini?
9 Sauti ya Yehova inaita muji;
Watu wenye kuwa na hekima yenye kutenda wataogopa jina lako.
Musikilize fimbo na mwenye aliiweka.+
10 Je, hazina za uovu zingali katika nyumba ya muovu
Na kipimo cha efa* chenye hakienee chenye kuchukiza?
11 Je, ninaweza kuwa na mwenendo safi* kama niko na mizani* ya uovu,
Na mufuko wa majiwe ya kupimia ya udanganyifu?+
12 Kwa maana matajiri wake wamejaa jeuri,
Na wakaaji wake wanasema uongo;+
Ulimi wao unasema udanganyifu katika kinywa chao.+
13 “Kwa sababu hiyo, nitakuumiza kwa kukupiga,+
Na kukufanya kuwa ukiwa kwa sababu ya zambi zako.
14 Utakula lakini hautashiba;
Utakuwa bila kitu ndani yako.+
Vitu vyenye utaondoa, hautavibeba kwa usalama,
Na vyenye unabeba, nitavitoa kwa upanga.
15 Utapanda mbegu, lakini hautavuna.
Utakanyanga zeituni, lakini hautatumia hayo mafuta;
Na utatengeneza divai mupya, lakini hautaikunywa.+
16 Kwa sababu unafuata maagizo ya Omri na kazi yote ya nyumba ya Ahabu,+
Na unafuata mashauri yao.
Ndiyo sababu nitakufanya kuwa kitu cha kuogopesha sana
Na wakaaji wake watakuwa kitu cha kupigia muluzi;+
Na utabeba zarau ya vikundi vya watu.”+
7 Ole wangu! Mimi ni kama mutu mwenye,
Kisha kukusanya matunda ya kipindi cha joto
Na masalio kisha mavuno ya zabibu,
Hapate kishada cha zabibu za kula,
Wala tini ya kwanza-kwanza yenye ninatamani sana.*
2 Mushikamanifu amekosekana katika dunia;
Hakuna munyoofu kati ya wanadamu.+
Wote wanavizia ili kumwanga damu.+
Kila mumoja anawinda ndugu yake kwa wavu wa* kukokotwa.
3 Mikono yao inajua kabisa kufanya mambo ya mubaya;+
Mukubwa anaomba mambo fulani,
Muamuzi anaomba zawabu,+
Mutu wa maana anaonyesha wazi tamaa yake,*+
Na wanafanya mupango mubaya pamoja.*
4 Mutu mwema zaidi kati yao ni kama miiba,
Na mutu munyoofu zaidi kati yao ni mubaya zaidi kuliko ukuta wa miiba.
Siku ya walinzi wenu na ya ninyi kutoa hesabu itakuja.+
Sasa watahangaika sana.+
5 Usiamini mwenzako
Ao kutumainia rafiki yako wa karibu.+
Ukuwe muangalifu juu ya mambo yenye unaambia mwenye kulala kwenye kifua chako.
6 Kwa maana mwana anazarau baba yake,
Binti anasimama kupingana na mama yake,+
Na binti-mukwe anapinga mama-mukwe wake;+
Maadui wa mutu ni watu wa nyumba yake.+
7 Lakini mimi, nitaendelea kumungojea Yehova.+
Nitaonyesha mutazamo wa kumungojea* Mungu wa wokovu wangu.+
Mungu wangu atanisikia.+
8 Usishangilie juu yangu, Ee adui* yangu.
Hata kama nimeanguka, nitasimama;
Hata kama ninakaa katika giza, Yehova atakuwa mwangaza wangu.
9 Nitavumilia kasirani kali ya Yehova
—Kwa maana nimemutendea zambi+—
Mupaka wakati atatetea kesi yangu ya hukumu na kufanya nitendewe haki.
Atanileta inje kwenye mwangaza;
Nitaangalia uadilifu* wake.
10 Adui yangu pia ataona,
Haya itamufunika mwenye aliniambia:
“Yehova Mungu wako iko* wapi?”+
Macho yangu yatamuangalia adui yangu.
Sasa atakanyangwa kama matope katika barabara.
11 Itakuwa siku ya kujenga kuta zako za majiwe;
Siku hiyo mipaka yako itapanuliwa.*
12 Siku hiyo watu watakuja kwako
Kutoka Ashuru na miji ya Misri,
Na kutoka Misri mupaka kwenye ule Muto;*
Kutoka bahari mupaka bahari na kutoka mulima mupaka mulima.+
13 Na inchi itakuwa ukiwa kwa sababu ya wakaaji wake,
Kwa sababu ya mambo yenye wamefanya.*
14 Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la uriti wako,+
Mwenye alikuwa anaishi peke yake katika pori—katikati ya shamba la matunda.
Uwaache wakule katika Bashani na Gileadi+ kama vile katika siku za zamani.
15 “Kama vile katika siku zenye ulitoka katika inchi ya Misri,
Nitamuonyesha mambo ya ajabu.+
16 Mataifa yataona na kusikia haya hata kama yako na nguvu nyingi.+
Watatia mikono yao juu ya vinywa vyao;
Masikio yao yatakuwa kama ya viziwi.
17 Watalambula mavumbi kama nyoka;+
Kama wanyama wa dunia wenye kutambaa watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Watakuja kwa Yehova Mungu wetu wakiwa na woga,
Na watakuogopa.”+
18 Ni Mungu gani mwenye kuwa kama wewe,
Mwenye kusamehe makosa na mwenye haangalie makosa+ ya mabaki ya uriti wake?+
Hataendelea kuwa na kasirani milele,
Kwa maana anafurahia upendo mushikamanifu.+
19 Atatuonyesha tena rehema;+ atashinda* makosa yetu.
Utatupa zambi zao zote katika sehemu za chini kabisa za bahari.+
20 Utaonyesha uaminifu kwa Yakobo,
Upendo mushikamanifu kwa Abrahamu,
Kama vile uliapia mababu zetu tangu siku za zamani.+
Kifupi cha jina Mikaeli (lenye kumaanisha “Ni Nani Mwenye Kuwa Kama Mungu?”) ao Mikaya (lenye kumaanisha “Ni Nani Mwenye Kuwa Kama Yehova?”).
Ao “maeneo tambarare ya chini.”
Inaonekana ni kitu chenye kutengenezwa na nyuki ili kuweka asali na chenye kinayeyuka haraka.
Tnn., “Nitamwanga.”
Ao “malipo yote ya ukahaba wake yatateketezwa.”
Maana yake “Katika nyumba ya Afra.”
Tnn., “Ee mukaaji mwanamuke.”
Tnn., “Mukaaji mwanamuke wa Saanani hajatokea.”
Tnn., “Mukaaji mwanamuke wa Maroti amengojea.”
Tnn., “Ee mukaaji mwanamuke.”
Ao “za kwaheri.”
Ao “mutu wa kukamata mali zenu.”
Tnn., “Ee mukaaji mwanamuke.”
Tnn., “hamutaondoa shingo zenu.”
Ao pengine, “kutoka kwenye.”
Zizi ni lupango ya kuchungia wanyama.
Ao “chungu cha kupikia chenye mudomo mukubwa.”
Tnn., “kutakasa.”
Ao “watafunga vinywa vyao.” Masharubu ni nywele zenye kuota kwenye mudomo wa juu.
Tnn., “Vichwa vyake.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “wanasema kama wanamutegemea Yehova.”
Ao “mulima wa hekalu.”
Ao “kilima chenye miti.”
Ao “Katika siku za mwisho.”
Ao “agizo litatoka.”
Ao “kurekebisha.”
Mundu ni kisu chenye kujikunja chenye kinatumiwa ili kuvuna.
Ao “Wataishi.”
Ao “anachechemea.”
Ao “anachechemea.”
Ao “zamani.”
Ao “shauri.”
Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
Ao “ukoo mbalimbali wa.”
Ao “viongozi.”
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Tnn., “kutoka katika mukono wenu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ao “zambi ya nafsi yangu?”
Ao “anaomba.”
Ao “ukuwe mwenye haki; bila upendeleo.”
Ao “ukuwe mwenye fazili na mushikamanifu katika upendo wako.” Tnn., “upende upendo mushikamanifu.”
Angalia Nyongeza B14.
Ao “Je, ninaweza kuwa bila kosa.”
Ao “kilo.”
Ao “nafsi yangu inatamani sana.”
Ao “makila ya.”
Ao “tamaa ya nafsi yake.”
Tnn., “wanausuka pamoja.”
Ao “Nitamungojea kwa uvumilivu.”
Katika Kiebrania, neno lenye kutafsiriwa “adui” liko katika jinsia ya kike.
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “eko.”
Ao pengine, “amri itakuwa mbali sana.”
Ni kusema, Efrati.
Tnn., “Kwa sababu ya matunda ya matendo yao.”
Ao “atakanyangia chini, atatiisha.”