Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • gf somo 12 uku. 20
  • Ni Nini Hutokea Wakati Wa Kifo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Nini Hutokea Wakati Wa Kifo?
  • Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wafu Wako mu Hali Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Watu Waliokufa Wako Wapi?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Kuzungumuza na Mashetani
    Amuka!—2014
Ona Habari Zaidi
Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
gf somo 12 uku. 20

Somo 12

Ni Nini Hutokea Wakati Wa Kifo?

Kifo ni kinyume cha uhai. Kifo ni kama usingizi mzito. (Yohana 11:​11-14) Wafu hawawezi kusikia, kuona, kusema, wala kuwaza lolote. (Mhubiri 9:​5, 10) Dini isiyo ya kweli hufundisha kwamba wafu huenda katika ulimwengu wa roho ili waishi na babu zao wa kale waliokufa. Biblia haifundishi hivyo.

Wafu hawawezi kutusaidia, wala hawawezi kutuumiza. Kwa kawaida, watu hufanya matambiko na kutoa dhabihu ambazo wanaamini kuwa zitawafurahisha wafu. Mambo hayo yanamchukiza Mungu kwa sababu yanategemea mojawapo ya uwongo mbalimbali wa Shetani. Vivyo hivyo, mambo hayo hayawezi kuwapendeza wafu, kwa kuwa hawana uhai. Hatupaswi kuogopa wala kuabudu wafu. Tunapaswa kumwabudu Mungu peke yake.​—⁠Mathayo 4:⁠10.

Wafu wataishi tena. Yehova atawaamsha wafu warudi kwenye uhai katika dunia paradiso. Jambo hilo litatendeka wakati ujao. (Yohana 5:​28, 29; Matendo 24:15) Mungu anaweza kuwaamsha watu ambao wamekufa kama vile wewe unavyoweza kumwamsha mtu kutoka katika usingizi.​—⁠Marko 5:​22, 23, 41, 42.

Wazo la kwamba sisi hatufi ni uwongo ambao Shetani Ibilisi anaeneza. Shetani na roho wake waovu hufanya watu wafikiri kwamba roho za wafu ziko hai nazo husababisha magonjwa na matatizo mengine. Shetani huwadanganya watu, nyakati nyingine kupitia ndoto na maono. Yehova huwashutumu wale wanaojaribu kuongea na wafu.​—⁠Kumbukumbu la Torati 18:​10-12.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine