Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 12 uku. 26-27
  • Mutoto wa Dada Yake na Paulo Hakuwa Anaogopa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mutoto wa Dada Yake na Paulo Hakuwa Anaogopa
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Musikilize . . . Namna Ninajitetea”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Ukuwe Hodari​—Yehova Ni Musaidizi Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • “Niko Safi Kutokana Na Damu ya Watu Wote”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • “Kutoa Ushahidi Kamili”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 12 uku. 26-27
Mutoto wa dada yake na Paulo anazungumuza na mukubwa wa wasoda

SOMO LA 12

Mutoto wa Dada Yake na Paulo Hakuwa Anaogopa

Ni vizuri tuzungumuze sasa juu ya habari ya kijana mumoja mwenye aliokoa mujomba yake. Mujomba yake ni mutume Paulo. Hatujue jina la ule kijana, lakini tunajua tu mambo yenye alifanya. Mambo yenye ule kijana alifanya yalionyesha kama hakuwa anaogopa hata kidogo. Unapenda kusikia mambo yenye ule kijana alifanya?—

Mutume Paulo alikuwa mwenye kufungwa kule Yerusalemu. Alifungwa juu alikuwa anahubiri habari ya Yesu. Wanaume fulani wabaya walimuchukia mutume Paulo. Kwa hiyo, walipanga kumutendea vibaya. Walisema hivi: ‘Tumuombe mukubwa wa wasoda awaambie wasoda wamulete mutume Paulo ku tribinale. Tutajificha pembeni ya barabara na wakati Paulo na wasoda watapita kwenye ile barabara, tutamuua!’

Paulo iko katika gereza na anasikiliza habari yenye mutoto wa dada yake iko anamuelezea

Mutoto wa dada yake na Paulo anamuelezea Paulo na mukubwa wa wasoda mupango wa watu wabaya

Mutoto wa dada yake na Paulo alisikia habari ya ule mupango. Ule mutoto alifanya nini? Alienda kwenye mutume Paulo alikuwa anafungwa ili kumuelezea habari hiyo. Wakati mutume Paulo alisikia habari ya ule mupango mubaya, mara moja akamuomba ule kijana aende kumuambia mukubwa wa wasoda. Unawaza ilikuwa mwepesi kwa kijana ule kuenda kumuambia mukubwa wa wasoda ule mupango?— Ni juu ule mukubwa wa wasoda alikuwa mutu wa cheo kikubwa. Hata vile, ule kijana hakuogopa. Alienda kumuambia ule mukubwa wa wasoda ule mupango mubaya.

Kwa hiyo, ule mukubwa wa wasoda alijua sasa kile atafanya. Alikamata kikundi cha wasoda karibu 500 ili kumuchunga mutume Paulo! Aliwaambia wamupeleke Paulo kule Kaisaria usiku. Unawaza wale wanaume waliweza kumuua mutume Paulo?— Wale wanaume wabaya hawangeweza tena kumushambulia mutume Paulo! Mupango wao mubaya ulishindwa.

Hadisi hii inakufundisha nini?— Na weye unaweza kuwa kama mutoto wa dada yake na Paulo. Unaweza kuwa bila woga. Hatupashwe kuogopa wakati tunaelezea wengine habari za Yehova. Na weye haupashwe kuogopa na unapashwa kuendelea kuelezea wengine habari za Yehova, si vile?— Ukifanya vile, unaweza kuokoa mutu fulani.

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Matendo 23:12-24

  • Mathayo 24:14; 28:18-20

  • 1 Timotheo 4:16

MAULIZO:

  • Wanaume fulani wabaya walifanya mupango gani juu ya Paulo?

  • Mutoto wa dada yake na Paulo alifanya nini? Ni juu ya nini iliomba mutu asiogope ili aweze kufanya vile?

  • Unaweza kufanya nini ili kuonyesha kama weye pia hauna woga kama ule kijana?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine