Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • yc somo 14 uku. 30-31
  • Ufalme Wenye Utatawala Dunia Yote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ufalme Wenye Utatawala Dunia Yote
  • Uwafundishe Watoto Wako
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Marafiki Wa Mungu Wataishi Katika Paradiso
    Unaweza Kuwa Rafiki ya Mungu!
  • Kusudi la Mungu Ni Nini Kuhusu Dunia?
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • “Tutaonana Katika Paradiso!”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • “Utakuwa Pamoja na Mimi Katika Paradiso”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Uwafundishe Watoto Wako
yc somo 14 uku. 30-31
Yesu Kristo anatawala akiwa Mufalme juu ya dunia Paradiso

SOMO LA 14

Ufalme Wenye Utatawala Dunia Yote

Unawaza tunataka kuzungumuza juu ya Ufalme gani?— Tutazungumuza juu ya Ufalme wa Mungu wenye utarudisha paradiso duniani. Unapenda kujifunza mambo mengi juu ya Ufalme wa Mungu?—

Kila ufalme uko na mufalme mwenye kutawala. Na mufalme huyo anatawala watu wenye kuishi katika inchi yake. Unajua ni nani Mufalme wa Ufalme wa Mungu?— Ni Yesu Kristo. Anaishi mbinguni. Karibuni atatawala kila mutu mwenye kuishi duniani! Unawaza tutateseka tena wakati Yesu atakuwa Mufalme juu ya dunia yote?—

Uko na hamu ya kuona nini katika Paradiso?

Tutafurahi sana! Mu Paradiso watu hawatapigana tena, wala kuenda kwenye vita. Watu wote watapendana. Hakuna mutu atakuwa mugonjwa, wala hakuna mutu atakufa. Watu wenye kuwa vipofu wataona, na watu wenye hawasikie watasikia. Watu wenye kuwa vilema wataruka-ruka na kukimbia. Kila mutu atakuwa na chakula mingi. Na wanyama watakuwa marafiki kati yao na watakuwa marafiki yetu. Watu waliokufa wataishi tena. Wanaume na wanawake wengi wenye tumesemea katika kitabu hiki kidogo, kama vile Rebeka, Rahabu, Daudi na Eliya, wataishi tena! Na weye utapenda kukutana na watu hao?—

Yehova anakupenda na anataka ukuwe na furaha. Kama unaendelea kujifunza habari za Yehova na kumutii, utaishi milele mu paradiso ya muzuri sana! Hii habari inakufurahisha?—

SOMA KATIKA BIBLIA YAKO

  • Isaya 2:4; 11:6-9; 25:8; 33:24; 35:5, 6

  • Yohana 5:28, 29; 17:3

MAULIZO:

  • Ni nani Mufalme wa Ufalme wa Mungu?

  • Yesu atatawala nani?

  • Wakati Yesu atatawala dunia, maisha itakuwa namna gani?

  • Unapashwa kufanya nini kama unapenda kuishi milele mu Paradiso?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine