Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • jy sura 28 uku. 70-uku. 71 fu. 6
  • Sababu Gani Wanafunzi wa Yesu Hawafunge?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Wanafunzi wa Yesu Hawafunge?
  • Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
jy sura 28 uku. 70-uku. 71 fu. 6
Wanafunzi wa Yohana Mubatizaji wanauliza Yesu juu ya kufunga

SURA YA 28

Sababu Gani Wanafunzi Wa Yesu Hawafunge?

MATAYO 9:14-17 MARKO 2:18-22 LUKA 5:33-39

  • WANAFUNZI WA YOHANA WANAULIZA YESU JUU YA KUFUNGA

Yohana Mubatizaji iko katika gereza tangu muda fulani kisha Yesu kuenda kwenye Pasaka ya mwaka wa 30 wakati wetu. Yohana alipenda wanafunzi wake wakuwe wafuasi wa Yesu, lakini haiko wote ndio wamefanya hivyo katika miezi ya kisha kufungwa kwa Yohana.

Sasa, wakati Pasaka ya mwaka wa 31 wakati wetu inakaribia, wanafunzi fulani wa Yohana wanakuja kumuona Yesu na kumuuliza hivi: “Sababu gani sisi na Wafarisayo tunazoea kufunga lakini wanafunzi wako hawafunge?” (Matayo 9:14) Wafarisayo wanafanya mafungo kama desturi ya kidini. Kisha muda fulani, Yesu anatumia mufano wenye kuzungumuzia Mufarisayo mumoja mwenye kiburi ambaye anasali hivi: “Ee Mungu, ninakushukuru kwa sababu mimi siko kama watu wengine wote . . . Ninafunga mara mbili kwa juma.” (Luka 18:11, 12) Inawezekana pia kufunga imekuwa desturi kwa wanafunzi wa Yohana. Ao pengine wamekuwa wakifunga ili kuomboleza kufungwa kwa Yohana katika gereza. Watu wengine wanajiuliza pia sababu gani wanafunzi wa Yesu hawafunge pengine kwa kujiunga na wengine wenye kuonyesha huzuni juu ya mambo yenye yamefikia Yohana.

Yesu anajibu kwa kutumia mufano huu: “Marafiki wa bwana-arusi hawana sababu ya kuomboleza wakati bwana-arusi iko pamoja nao, haiko vile? Lakini siku zitakuja wakati bwana-arusi ataondolewa kwao, halafu watafunga.”—Matayo 9:15.

Yohana mwenyewe anamuita Yesu bwana-arusi. (Yohana 3:28, 29) Kwa hiyo, wanafunzi wa Yesu hawafunge wakati Yesu iko pamoja nao. Kisha, wakati Yesu atakufa, wanafunzi wake wataomboleza na hawatapenda kula. Lakini mambo yatabadilika kabisa wakati Yesu atafufuliwa! Kwa hiyo hawatakuwa na sababu ya kufunga ili kuomboleza.

Kisha, Yesu anatoa mifano hii mbili: “Hakuna mutu mwenye anashonea kipande cha nguo mupya kwenye nguo ya inje ya zamani, kwa maana kipande hicho cha nguo mupya kitakokota nguo hiyo ya zamani na itapasuka mubaya sana. Wala watu hawatie divai mupya ndani ya chupa za ngozi za kuwekea divai zenye kuzeeka. Kama wanafanya vile, chupa hizo zitapasuka na divai itamwangika na chupa hizo zitaharibika. Lakini watu wanatia divai mupya ndani ya chupa mupya za ngozi za kuwekea divai.” (Matayo 9:16, 17) Yesu anapenda kusema nini?

Yesu anasaidia wanafunzi wa Yohana Mubatizaji waelewe kwamba hawapaswe kutazamia kama wafuasi wa Yesu watafuata tabia za zamani za dini ya Kiyahudi, kama vile desturi ya kufunga. Hakuja kutia viraka na kuendeleza aina fulani ya ibada yenye kuzeeka, yenye ilikuwa karibu kuachwa. Ibada yenye Yesu anatia watu moyo kufuata haitegemee dini ya Kiyahudi na desturi zake za wanadamu. Wala, haiko anajaribu kutia kipande cha nguo mupya juu ya nguo yenye kuzeeka ao kutia divai ya mupya ndani ya chupa ya ngozi yenye kuzeeka.

MIFANO KUHUSU KUFUNGA

Chupa ya ngozi

Yesu alitumia mufano wenye wasikilizaji wengi wangeelewa haraka: kushona. Ikiwa mutu angeshonea kipande cha nguo ya mupya juu ya nguo yenye imekwisha kutumiwa ao yenye kuzeeka, ni nini ingeweza kutokea? Wakati wa kufua, nguo mupya inaweza kukokota sehemu fulani ya nguo yenye kuzeeka, na kufanya nguo hiyo ipasuke.

Vilevile, wakati fulani divai iliwekwa katika chupa zenye kutengenezwa na ngozi za wanyama. Kisha wakati fulani, ngozi hiyo ingekauka na kuwa ya nguvu-nguvu. Ilikuwa hatari kutia divai ya mupya katika chupa kama hiyo. Divai ya mupya ingeendelea kuchachuka, na kuvimbisha chupa hiyo ya ngozi. Hilo lingeweza kupasua chupa ya ngozi yenye kuzeeka na ambayo ni ya nguvu-nguvu.

  • Katika siku za Yesu, ni nani walikuwa wanafunga na sababu gani?

  • Sababu gani wanafunzi wa Yesu hawafunge wakati iko pamoja nao, lakini ni nini pengine ingewafanya wafikie kufunga?

  • Mifano ya Yesu juu ya kipande cha nguo mupya na divai mupya inamaanisha nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine