Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 37 uku. 90-uku. 91 fu. 1
  • Yehova Anazungumuza na Samweli

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yehova Anazungumuza na Samweli
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Aliendelea Kukomaa Mbele ya Yehova
    Tuige Imani Yao
  • Samweli Aliendelea Kufanya Mambo Mazuri
    Uwafundishe Watoto Wako
  • Alivumilia Licha ya Kuvunjwa Moyo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Alikutana na Hali Zenye Kuvunja Moyo, Lakini Alivumilia
    Tuige Imani Yao
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 37 uku. 90-uku. 91 fu. 1
Samweli anafungua milango ya tabenakulo

37

Yehova Anazungumuza na Samweli

Kuhani Mukubwa Eli alikuwa na watoto wawili wanaume wenye walikuwa makuhani ku tabenakulo. Jina la mumoja lilikuwa Hofni na la mwingine Finehasi. Hawakutii amri za Yehova, na walitendea watu mubaya sana. Wakati Waisraeli walikuwa wanakuja kumutolea Yehova zabihu, Hofni na Finehasi walikuwa wanajikamatia nyama ya muzuri sana. Eli alisikia ile mambo yenye watoto wake walikuwa wanafanya, lakini hakufanya kitu. Je, Yehova angeacha ile hali iendelee?

Hata kama Samweli alikuwa mutoto kuliko Hofni na Finehasi, hakufuata mufano wao. Yehova alifurahia Samweli. Usiku moja, Samweli alikuwa analala, kisha akasikia sauti inamuita. Akaamuka, akakimbia kwa Eli na kumuambia: ‘Mimi huyu!’ Lakini, Eli akamuambia: ‘Sikukuita. Rudia ulale.’ Samweli akarudia kulala. Kisha, akasikia sauti inamuita tena. Wakati Samweli alisikia ile sauti mara ya tatu, Eli akatambua kama Yehova njo alikuwa anamuita. Akaambia Samweli hivi: “Kama anakuita, umuambie, ‘Sema, Yehova, kwa maana mutumishi wako anasikiliza.’”

Samweli anaelezea Eli mambo yenye Yehova alimuambia

Samweli akaenda tena kulala. Kisha, akasikia sauti inamuita: ‘Samweli! Samweli!’ Akajibu: ‘Sema, mutumishi wako iko anasikiliza.’ Yehova akamuambia: ‘Uambie Eli kama nitamupatia malipizi yeye na familia yake. Anajua kama watoto wake wako wanafanya mambo ya mubaya mu tabenakulo yangu, lakini hafanye kitu.’ Asubui ya kufuata, Samweli alifungua milango ya tabenakulo kama vile alikuwa anafanya kila siku. Alikuwa anaogopa kuelezea kuhani mukubwa mambo yenye Yehova alimuambia. Lakini Eli akamuita na kumuuliza: ‘Mutoto wangu, Yehova alikuambia nini? Niambie mambo yote.’ Kisha Samweli akamuelezea mambo yote.

Samweli aliendelea kukomaa, na Yehova aliendelea kuwa pamoja naye. Mu inchi yote ya Israeli, watu wote walijua kama Yehova amechagua Samweli ili akuwe nabii na muamuzi.

“Basi, kumbuka Muumbaji wako Mukubwa katika siku za ujana wako.”​—Muhubiri 12:1

Maulizo: Hofni na Finehasi walikuwa wanafanya nini, je, Samweli alifuata mufano wao? Yehova aliambia Samweli nini?

1 Samweli 2:12-17, 22-26; 3:1-21; 7:6

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine