Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lfb somo 85 uku. 198-uku. 199 fu. 1
  • Yesu Anaponyesha Mutu Siku ya Sabato

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yesu Anaponyesha Mutu Siku ya Sabato
  • Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wafarisayo Wanauliza Maulizo Mwanaume Mwenye Alikuwa Kipofu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Yesu Anaponyesha Mwanaume Mwenye Alizaliwa Kipofu
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Wanakata Masuke ya Nafaka Siku ya Sabato
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
lfb somo 85 uku. 198-uku. 199 fu. 1
Wafarisayo wanamuuliza mutu mwenye alikuwa kipofu maulizo

85

Yesu Anaponyesha Mutu Siku ya Sabato

Wafarisayo walimuchukia Yesu, na walitafuta sababu za kumukamata. Walisema kama hakupaswa kuponyesha wagonjwa siku ya Sabato. Siku moja ya Sabato, Yesu aliona mwanaume mumoja kipofu mwenye alikuwa anaomba-omba mu barabara. Yesu akaambia wanafunzi wake: ‘Muone namna nguvu za Mungu zitaponyesha huyu mwanaume.’ Yesu akatema mate chini, kisha akafanya matope kwa kuchanga udongo na ile mate, na akaipakaa ku macho ya ule mwanaume. Kisha Yesu akamuambia: ‘Uende unawe katika kiziwa cha maji cha Siloamu.’ Ule mwanaume akafanya vile, na kwa mara ya kwanza mu maisha yake, akaanza kuona.

Watu walishangaa sana. Walianza kuulizana: ‘Huyu njo ule mwanaume mwenye alikuwa anaomba-omba ao ni mutu mwingine wa kumufanana?’ Ule mwanaume akawajibu: ‘Ni mimi! Nilizaliwaka kipofu!’ Wakamuuliza: ‘Hauko tena kipofu, ulipona namna gani?’ Wakati aliwaelezea jambo lenye lilifanyika, wakamupeleka kwa Wafarisayo.

Ule mwanaume akaambia Wafarisayo: ‘Yesu alinipakaa matope ku macho, kisha, aliniambia niende ninawe ili kutosha ile matope ku macho. Nilifanya vile, na sasa ninaona.’ Wafarisayo wakasema: ‘Kama Yesu anaponyesha siku ya Sabato, ni kusema, nguvu yake ya kuponyesha haitoke kwa Mungu.’ Lakini wengine wakasema: ‘Kama ile nguvu haikutoka kwa Mungu, hangeweza kuponyesha watu.’

Kisha Wafarisayo wakaita wazazi wa ule mwanaume na kuwauliza: ‘Sasa ni nini ilifanya mutoto wenu aanze kuona?’ Wazazi wa ule mwanaume waliogopa kwa sababu Wafarisayo walikuwa wamesema kama mutu mwenye atamuamini Yesu angefukuzwa mu sinagogi. Kwa hiyo, wakajibu: ‘Hatujue. Mumuulize.’ Wafarisayo wakaendelea kuuliza ule mwanaume, na ku mwisho akasema: ‘Nimewaambia mambo yote yenye ninajua. Juu ya nini munaendelea kuniuliza?’ Wafarisayo wakakasirika na kumufukuza.

Yesu akaenda kuona ule mwanaume na akamuuliza: ‘Unaamini Masiya?’ Ule mwanaume akamujibu: ‘Kama ningemujua ningemuamini.’ Yesu akamuambia: ‘Mimi njo ule Masiya.’ Yesu alimutendea muzuri kabisa. Kwanza alimuponyesha, na kisha alimusaidia akuwe na imani.

“Munakosea, kwa sababu hamujue Maandiko wala nguvu za Mungu.” ​—Matayo 22:29

Maulizo: Namna gani Yesu alisaidia mwanaume mwenye alikuwa kipofu? Juu ya nini Wafarisayo walimuchukia Yesu?

Yohana 9:1-41

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine