Utangulizi wa Sehemu ya 13
Yesu alikuja ku dunia ili atoe uzima wake kwa ajili ya wanadamu wenye hawakamilike. Hata kama alikufa, alishinda ulimwengu. Yehova alikuwa mushikamanifu kwa Mwana wake na alimufufua. Wakati alikuwa muzima hapa ku dunia, Yesu alitumikia watu kwa unyenyekevu na kuwasamehe wakati walimukosea. Kisha kufufuliwa, Yesu alitokea wanafunzi wake. Aliwafundisha kufanya kazi ya maana sana yenye aliwapatia. Kama uko muzazi, saidia mutoto wako aelewe kama sisi pia tunapaswa kufanya ile kazi leo.