Maneno ya Utangulizi
KUSUDI LA KITABU HIKI
Yehova Mungu anashauria watu wake ‘waendelee kutafuta’ uelewaji na utambuzi kama “hazina zenye kufichwa.” (Mez. 2:1-5) Ile inamaanisha kama tunapaswa kujikaza ili kutafuta majibu ya maulizo yenye tunajiuliza kuhusu Biblia na kutafuta musaada juu ya mambo yenye kutuhangaisha mu maisha. Kitabu hiki, ni kusema, Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova kimetayarishwa ili kukusaidia kutafuta habari mbalimbali.
Kitabu hiki hakiko kama endekse (Fahirisi), yenye inataja habari zote zenye zilizungumuziwa mu vichapo vyetu vyote. Hata hivyo, kila habari yenye kutajwa mu kitabu hiki inatuma mutu mu vichapo vyenye vimetolewa mu luga ya Kiswahili kuanzia mwaka wa 2000 na kuendelea.
NAMNA YA KUTAFUTA HABARI
Chunguza Habari Zenye Kuwa Ndani ku ukurasa wenye kufuata, na kisha uamue ni habari gani itakusaidia kupata mambo yenye unatafuta. Pengine itakuomba wakati fulani kuchunguza habari nyingi ili kupata mambo yenye unatafuta. Chini ya kila habari kuko vichwa vidogo-vidogo vyenye vimepangwa muzuri ili kukusaidia kupata mambo yenye unatafuta.
Kisha, enda ku ukurasa wenye kuonyeshwa ili kupata habari ao kichwa kidogo chenye ulichagua. Ku ule ukurasa utakuta vichwa vya habari na sura mbalimbali; chagua ile yenye unapenda kuchunguza. Ikiwa unaweza kupata vichapo kwako ku nyumba, ku maktaba ya Jumba la Ufalme, ao kwa njia ya kielektroniki, angalia ni habari ao sura gani yenye kuonyeshwa. Hata kama habari yenye umechagua inaonekana kuwa haipatane kabisa na mambo yenye unatafuta, ujue kama habari yenye kuonyeshwa ku ule ukurasa itakuwa na mambo yenye unatafuta juu ya habari yenye umechagua.
Ikiwa unatafuta mafasirio ya andiko fulani la Biblia, uende ku sehemu Maandiko Yenye Kufasiriwa. Ni maandiko yenye kufasiriwa katika njia fulani tu njo itapatikana kwa ile sehemu.
Kumbuka kama unatafuta “hazina zenye kufichwa;” kwa hiyo, inaomba wakati na bidii. Kwa hiyo, ukuwe muvumilivu wakati unatafuta muongozo ao jibu fulani kwa ulizo lenye unajiuliza. Ukizoea kutumia kitabu Kutafuta Habari, itakuwa mwepesi kwako kupata habari yenye unatafuta na utafurahia kukitumia. Yehova atakubariki ikiwa unajikaza kutafuta habari, na atakusaidia kupata hekima na uelewaji.—Mez. 2:6; 4:5.
ALAMA ZENYE ZITAKUONGOZA:
❐ = Habari zenye kuwa mu gazeti moja
§ = Kichwa kidogo, ao sehemu
fu. = Fungu ao mafungu
sura = Sura
uku. = Ukurasa ao kurasa
Na. = Namba
12/2004 = Mwezi/Mwaka
1/2/2010 = Siku/Mwezi/Mwaka
Vitabu vyenye kufuata, tayari viko na endekse (Fahirisi):
Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Tengenezo Lenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
‘Ona Nchi Nzuri’