Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/2 uku. 27
  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matibabu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matibabu?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matunzo?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Je, Mukristo Anaweza Kukubali Matunzo ya Kiganga?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Je, Umekawia?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Je, Unajua Maamuzi Unayoweza Kufanya?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/2 uku. 27

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Je, Mashahidi wa Yehova Wanakubali Matibabu?

▪ Yesu alisema kwamba “watu wenye afya hawahitaji tabibu, bali wenye kuugua ndio wanaomhitaji.” (Mathayo 9:12) Hivyo, alikuwa akionyesha kwamba si kosa kulingana na Biblia kutafuta msaada kutoka kwa wataalamu wa tiba. Hivyo, Mashahidi wa Yehova hukubali dawa na matibabu bila shida. Wanataka kuwa na afya nzuri na maisha marefu. Kwa kweli, kama Mkristo wa karne ya kwanza, Luka, baadhi ya Mashahidi wa Yehova ni madaktari.—Wakolosai 4:14.

Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova hawakubali matibabu yanayopingana na kanuni za Biblia. Kwa mfano, hawakubali kutiwa damu, kwa sababu Biblia inazuia kutumia damu kutibu mwili. (Mwanzo 9:4; Mambo ya Walawi 17:1-14; Matendo 15:28, 29) Neno la Mungu pia linakataza matibabu yanayotia ndani kutumia “nguvu za uchawi,” au kuwasiliana na pepo.—Isaya 1:13; Wagalatia 5:19-21.

Wataalamu wengi wa tiba hutoa matibabu ambayo hayapingani na kanuni za Biblia. Mara nyingi matibabu ya aina hiyo, ambayo wengi wa Mashahidi huyakubali, ni bora zaidi yakilinganishwa na yale yaliyo kinyume cha matakwa ya Mungu.

Kwa kweli, watu wana maoni mbalimbali kuhusu afya. Matibabu yanayoweza kumfaa mtu mmoja huenda yasimsaidie mtu mwingine. Kwa hiyo, watu wanaotafuta vipimo na matibabu sahihi ya magonjwa yao wanaweza kutafuta maoni ya madaktari tofauti-tofauti.—Methali 14:15.

Si kila Shahidi atachagua matibabu yaleyale. Neno la Mungu linawaruhusu Wakristo watumie dhamiri zao ikiwa hakuna kanuni ya Biblia inayovunjwa. (Waroma 14:2-4) Hivyo basi, kila mtu anapaswa kuchunguza matibabu yanayopendekezwa na kuhakikisha kwamba hayapingani na dhamiri yake iliyozoezwa na Biblia.—Wagalatia 6:5; Waebrania 5:14.

Shahidi atafikiria kila uamuzi anaofanya kama vile dereva afanyavyo anapofika sehemu ya barabara ambapo magari mengi yanapishana. Ikiwa dereva huyo atayafuata tu magari yaliyo mbele yake na kuvuka sehemu hiyo bila kupunguza mwendo, anaweza kusababisha uharibifu mkubwa. Dereva mwenye busara atapunguza mwendo na pia kukadiria mwendo wa magari mengine kabla ya kuvuka. Vivyo hivyo, Mashahidi hawafanyi maamuzi yanayohusu matibabu haraka-haraka, wala hawafuati maoni ya watu wengine bila kufikiri. Badala yake, wanafikiria aina ya matibabu wanayoweza kuchagua na kuchunguza kanuni za Biblia kabla ya kufanya uamuzi.

Kwa kweli, Mashahidi wa Yehova wanathamini sana bidii na kujitoa kwa wale wanaotoa huduma za afya. Na pia, wanafurahia sana wataalamu hao wanapowasaidia kupata nafuu kutokana na magonjwa yao.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine