Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/1 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kutenda Wakati Banatutendea Bila Haki
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • 4 Mungu Hatendi kwa Haki—Je, Ni Kweli?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • ‘Muamuzi wa Dunia Yote’ Anafanya Sikuzote Mambo Yenye Kuwa Sawa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/1 uku. 16
Mwanamuke mumoja na watoto wake wanaoishi maisha ya umaskini sana

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Mungu ni mutu wa aina gani?

Mungu ni mutu wa roho asiyeonekana. Aliumba mbingu, dunia, na vitu vyote vilivyo na uzima. Mungu hakuumbwa na hana mwanzo. (Zaburi 90:2) Mungu anapenda watu wamutafute na wajue kweli juu yake.​—Soma Matendo 17:24-27.

Mungu ni mutu na tunaweza kujua jina lake. Tunaweza kutambua sifa zake fulani kwa kutazama vitu ambavyo aliumba. (Waroma 1:20) Lakini ili kujua Mungu vizuri, ni lazima tujifunze Biblia, Neno lake. Biblia inatujulisha sifa nzuri za Mungu.​—Soma Zaburi 103:7-10.

Mungu anajisikia namna gani anapoona ukosefu wa haki?

Yehova, Muumbaji wetu, anachukia ukosefu wa haki. (Kumbukumbu la Torati 25:16) Aliwaumba wanadamu kwa mufano wake. Ndiyo sababu watu wengi kati yetu wanachukia ukosefu wa haki. Ukosefu wa haki ambao tunaona kila mahali hauletwe na Mungu. Mungu aliwapatia watu uhuru wa kuchagua. Jambo la kuhuzunisha ni kwamba watu wengi wanatumia vibaya uhuru wao na wanafanya matendo ya ukosefu wa haki. Yehova anaumia moyoni mwake.​—Soma Mwanzo 6:5, 6; Kumbukumbu la Torati 32:4, 5.

Yehova anapenda haki, na hataacha ukosefu wa haki uendelee milele. (Zaburi 37:28, 29) Biblia inaahidi kwamba hivi karibuni Mungu atamaliza ukosefu wote wa haki.​—Soma 2 Petro 3:7-9, 13.

Biblia inaahidi kwamba Mungu ataleta haki duniani pote

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 1 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine