Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 3 uku. 3
  • Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Namna ya Kupiganisha Huzuni Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Mambo Yenye Unapaswa Kutazamia
    Amuka!—2018
  • Utangulizi
    Amuka!—2018
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 3 uku. 3

Habari Kubwa

Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa

“Mungu anajua muzuri, mupendwa. . . . U . . . si . . . lie.”

Mwanamuke mumoja mwenye kuitwa Bebe ndiye aliambiwa maneno hayo kwa sauti ya chini kwenye sikio. Alikuwa kwenye maziko ya baba yake, mwenye alikufa katika aksidenti ya motokari.

Bebe na baba yake walikuwa wanapendana sana. Bebe aliambiwa maneno hayo na rafiki fulani wa familia yao mwenye nia ya muzuri, lakini maneno hayo yalimuumiza kuliko kumufariji ao kumutuliza moyo. Aliendelea kujiambia hivi: “Kifo chake halikukuwa jambo la muzuri.” Miaka mingi kisha hapo, wakati Bebe alieleza habari hiyo katika kitabu fulani, ni wazi kama alikuwa angali na huzuni nyingi.

Kama vile Bebe alijionea, inaomba wakati ili kupiganisha huzuni, zaidi sana ikiwa mutu mwenye alifiwa alipendana sana na marehemu. Katika Biblia, kifo kinaitwa kwa kufaa “adui wa mwisho.” (1 Wakorintho 15:26) Kifo kinatokea na kuvuruga maisha yetu na hakuna kitu chenye kinaweza kukizuia, mara nyingi kinafika wakati hatuko tayari kabisa, na kinatunyanganya watu wenye tulipenda sana. Hakuna mutu mwenye anaweza kuepuka matokeo ya kifo. Kwa hiyo, haishangaze kuona tunajisikia kuwa hatujue la kufanya ili kupambana na kifo na matokeo yake.

Pengine umekwisha kujiuliza hivi: ‘Inaomba muda gani ili huzuni imalizike? Namna gani mutu anaweza kupiganisha huzuni? Namna gani ninaweza kufariji watu wenye wamefiwa? Kuko tumaini fulani kwa ajili ya watu wenye tunapenda wenye wamekufa?’

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine