Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w18 Mwezi wa 8 uku. 31-32
  • Namna Mbegu za Kwanza za Ufalme Zilipandwa Katika Ureno

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna Mbegu za Kwanza za Ufalme Zilipandwa Katika Ureno
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
w18 Mwezi wa 8 uku. 31-32

VITU VYA MAANA SANA VYA HISTORIA YETU

Namna Mbegu za Kwanza za Ufalme Zilipandwa Katika Ureno (Portugal)

WAKATI mawimbi ya Bahari ya Atlantiki yalikuwa yanapiga-piga mashua yenye ilikuwa inasafiri kuenda Ulaya, George Young, mumoja wa wasafiri, alikuwa anafikiria kwa furaha mambo yenye alikuwa amefanya kwa ajili ya Ufalme katika Brazili.a Lakini, wakati safari ilikuwa inaendelea, Ndugu Young alianza sasa kufikiria mugao wake mupya, ni kusema, maeneo makubwa ya Hispania na Ureno yenye yalikuwa hayajahubiriwa. Wakati alifika kule, alitumainia kufanya mupango ili atolee watu trakte 300 000 na ili Ndugu Rutherford atoe hotuba zenye kutegemea Biblia!

George Young anasafiri kwa kutumia mashua

George Young alisafiri katika bahari wakati alifanya safari nyingi za kuhubiri

Kisha tu Ndugu Young kufika Lisbon katika kipindi cha mvua ya mwisho mwaka wa 1925, alikutana hali ya muvurugo. Katika mwaka wa 1910, kulikuwa mapinduzi yenye yalifanya utawala wa familia ya kifalme ufikie mwisho na hilo lilifanya Kanisa Katoliki lipoteze nguvu zake. Watu walipata uhuru mwingi, lakini vita ya watu wenyewe kwa wenyewe iliendelea katika inchi hiyo.

Wakati tu Ndugu Young alikuwa anafanya mipango ili Ndugu Rutherford atoe hotuba yake, serikali ililazimisha kwamba inchi itawaliwe na maaskari kwa sababu kulikuwa jaribio la kuangusha utawala. Muandishi wa Chama cha Biblia cha Uingereza na Inchi za Kigeni alionya Ndugu Young kwamba angepata upinzani mukubwa. Hata hivyo, Ndugu Young aliomba ruhusa ya kutumia jumba kubwa la kufanyia mazoezi la Masomo ya Segondere ya Camões, na ombi lake lilikubaliwa!

Kisha, tarehe 13 Mwezi wa 5 ikafika, ni kusema, siku yenye ilipangwa ili Ndugu Rutherford atoe hotuba yake. Watu walingojea kwa hamu sana hotuba hiyo! Pankarte kwenye majengo na magazeti vilitangaza hotuba ya watu wote yenye kichwa “Namna ya Kuishi Milele Duniani.” Wapinzani wa kidini walichapisha haraka habari fulani katika gazeti lao ili kuonya wasomaji wao juu ya “manabii wa uongo” wenye walikuwa wamefika. Kwenye mulango wa jumba la mazoezi, wapinzani walitolea pia watu maelfu ya broshua zenye zilikuwa na habari za kuonya watu juu ya mafundisho ya Ndugu Rutherford.

Lakini, watu 2 000 hivi walijaa katika jumba hilo, na wengine 2 000 hivi hawakuruhusiwa kuingia kwa sababu nafasi ziliisha. Wasikilizaji fulani wenye kupendezwa walikamatilia kwenye ngazi za kamba zenye zilikuwa kwenye ngambo zote za jumba hilo; na wengine walipanda juu ya vyombo vya kufanyia mazoezi.

Mambo yote hayakuendeka muzuri. Wapinzani walikuwa wanalalamika na kuvunja-vunja viti. Lakini Ndugu Rutherford aliendelea kuwa mutulivu na alipanda juu ya meza ili watu wamusikie muzuri. Wakati alimaliza hotuba yake, karibu na katikati ya usiku, watu zaidi ya 1 200 wenye kupendezwa waliacha majina yao na adresi zao ili wakuwe wanapata vichapo vyenye kutegemea Biblia. Siku yenye ilifuata, gazeti la habari O Século lilichapisha habari yenye ilizungumuzia hotuba ya Ndugu Rutherford.

Katika Mwezi wa 9, 1925, gazeti Munara wa Mulinzi la luga ya Kireno lilianza kuchapishwa katika inchi ya Ureno. (Mbele ya pale, gazeti hilo la Munara wa Mulinzi la luga ya Kireno lilikuwa limekwisha kuchapishwa katika inchi ya Brazili.) Karibu na wakati huo, Virgílio Ferguson, Mwanafunzi mumoja wa Biblia katika Brazili, alianza kufanya mipango ili kuhamia Ureno kusudi asaidie katika kazi ya Ufalme. Zamani, alitumika pamoja na Ndugu Young katika biro ndogo ya tawi ya Wanafunzi wa Biblia katika Brazili. Bila kukawia, Virgílio alisafiri pamoja na Lizzie, bibi yake, ili kujiunga tena na Ndugu Young. Ndugu Ferguson alifika kwa wakati wenye kufaa kabisa kwa sababu Ndugu Young alipaswa kuhama ili kuhubiri katika maeneo mengine, kutia ndani Muungano wa Sovieti.

Vikaratasi vya Lizzie na Virgílio Ferguson vya kukubaliwa kukaa katika inchi, mwaka wa 1928

Vikaratasi vya Lizzie na Virgílio Ferguson vya kukubaliwa kukaa katika inchi, mwaka wa 1928

Wakati mapinduzi ya kijeshi yalileta utawala wa kidikteta katika Ureno, upinzani uliongezeka. Ndugu Ferguson hakuogopa na alichukua hatua fulani ili kulinda kikundi kidogo cha Wanafunzi wa Biblia na kutegemeza kazi zao. Aliomba ruhusa ili nyumba yake itumiwe kwa ukawaida kwa ajili ya mikutano. Alipewa ruhusa hiyo katika Mwezi wa 10, 1927.

Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa kidikteta, watu karibu 450 katika Ureno walijiandikisha ili wakuwe wanapata gazeti Munara wa Mulinzi. Zaidi ya hilo, kupitia trakte mbalimbali na vijitabu, neno la kweli lilifika katika maeneo ya mbali zaidi ya Utawala wa Ureno, maeneo kama vile Angola, Açores, Cap Vert, Timor Mashariki, Goa, Madeira, na Musumbiji (ao Mozambique).

Katika mwaka wa 1929, Manuel da Silva Jordão, Mureno mumoja mwenye alikuwa anafanya kazi ya kutunza mabustani, alikuja Lisbon. Wakati alikuwa anaishi katika Brazili, alisikia hotuba ya watu wote yenye Ndugu Young alitoa. Mara moja alitambua kama amepata kweli na alikuwa tayari kumusaidia Ndugu Ferguson ili kueneza kazi ya kuhubiri. Ili kueneza kazi hiyo, Manuel alifanya kazi ya kolportere, ni vile mapainia walikuwa wanaitwa zamani. Kwa sababu kazi ya kuchapisha na kugawanya vichapo vyenye kutegemea Biblia ilikuwa sasa imepangwa muzuri, kutaniko mupya katika Lisbon liliendelea muzuri!

Katika mwaka wa 1934, Ndugu Ferguson na bibi yake walipaswa kurudia Brazili. Lakini, mbegu za kweli zilikuwa zimepandwa. Wakati wa vita ya watu wenyewe kwa wenyewe katika Hispania na wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu kulikuwa muvurugo katika Ulaya, lakini kikundi cha ndugu na dada waaminifu katika inchi ya Ureno kiliendelea kushikamana na Yehova. Kwa wakati fulani, walionekana kama vile makaa yenye kuwaka, lakini katika mwaka wa 1947, iliomba kuwachochea, kwa njia ya mufano, wakati John Cooke, misionere wa kwanza alifika kule, mwenye alipata mazoezi kwenye Masomo ya Gileadi. Kisha pale, wahubiri wa Ufalme waliendelea kuongezeka sana. Hata wakati serikali ilikataza kazi za Mashahidi wa Yehova katika mwaka wa 1962, kuliendelea kuwa ongezeko. Katika Mwezi wa 12, 1974, wakati Mashahidi wa Yehova walikubaliwa na sheria, kulikuwa wahubiri zaidi ya 13 000 katika inchi hiyo.

Leo, wahubiri wa Ufalme zaidi ya 50 000 wako wanahubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu katika Ureno na katika visiwa fulani kwenye luga ya Kireno inazungumuzwa, kutia ndani Açores na Madeira. Kati ya wahubiri hao leo, kuko wazao wa watu fulani wenye walifuata hotuba yenye haiwezi kusahaulika ya Ndugu Rutherford katika mwaka wa 1925.

Tunamushukuru Yehova na ndugu na dada hao waaminifu wa kwanza-kwanza, wenye kupitia ujasiri wao, walikuwa kwenye mustari wa mbele katika kazi wakiwa ‘watumishi wa watu wote wa Kristo Yesu kwa mataifa.’​—Ro. 15:15, 16.​—Kutoka katika vitu vya maana sana vya historia yetu vya Ureno.

a Ona habari yenye kichwa “Kungali Kazi Kubwa ya Mavuno” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 15 mwezi wa 5, 2014, uku. 31-32.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine