Je! Programu Ya Mikutano Itabadilika?
Wakati makutaniko mengi yanayotumia Jumba lilelile la Ufalme yanakubaliana ili kukusanyika kwa kufuatana zamu kwa zamu au kurekebisha programu ya mikutano, yangepaswa kufanya marekebisho hayo mnamo Januari 1. Kwa kuwa tayari kutegemeza mpango huo, tunaonyeshana wamoja kwa wengine upendo na uthamini. Mara nyingi, mabadiliko katika programu ya mikutano yanafanywa kwa faida yetu ili kutuwezesha kuihudhuria kwa urahisi zaidi.
Tofauti na hilo, inawezekana kwamba marekebisho ya programu ya mikutano yatakayoanza mnamo Januari yasilingane vizuri zaidi na matumizi yetu ya wakati. Tutalazimika labda kufanya mabadiliko yatakayoyavuruga kidogo. Tukiwa wenye kushirikiana, tutaonyesha kwamba tunaelewa sababu ya kuwako kwa mpango huo unaoleta faida kwa wale wanaohusika.
Bila shaka, marekebisho yajayo ya programu ya mikutano yanaweza kutufaa vizuri zaidi. Kwa kungoja, tunatiwa moyo kufanya mabadiliko ya lazima yanayotuwezesha kuhudhuria kwenye mikutano yote ya juma, kulingana na programu iliyoamuliwa na kutaniko. Tujitahidi kulinda maoni yaleyale kama mtunga zaburi, aliyesema: “Nilifurahi wakati waliponiambia: ‘Twende kwa nyumba ya [Yehova]!’”—Zab. 122:1.
Katika miji ambako makutaniko mengi yanatumia jumba lilelile, inafikia kwamba kutoelewana kunatokea kati ya mabaraza ya wazee kuhusu programu ya mikutano. Tunaweza kusoma yafuatayo katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1988, ukurasa 19, fungu 15: “Mathalani, ikiwa makundi mawili yanashirikiana utumishi wa Jumba la Ufalme moja, kundi moja halipaswi kuchukua msimamo wa kwamba hilo ndilo “mwenyeji” wa jumba hilo na kwamba ndilo lenye mamlaka ya kuamrisha kiimla nyakati za mikutano au mambo mengineyo kwa kundi lile jingine. Kustahiana na kufanyiana ushirikiano kunapasa kuwepo sana.”—1 Pt. 3:10-12.