Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/96 uku. 1
  • Kufaidika na Shule ya Huduma ya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kufaidika na Shule ya Huduma ya
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Shule Inayotuandalia Vifaa kwa Ajili ya Utendaji wa Maana Zaidi Maishani
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2001
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Jinsi Tunavyofaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Shule ya huduma ya kitheokrasi mnano 2000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 3/96 uku. 1

Kufaidika na Shule ya Huduma ya

Kitheokrasi ya 1996 — Sehemu ya 2

1 Muda mfupi tu kisha kuanzishwa kwa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi katika 1943, moja ya matawi ya Sosaiti iliripoti hivi: “Mpango huu bora umesaidia ndugu wengi, waliojisikia kuwa hawawezi kusema mbele ya watu wote, kuwa kwa muda mfupi tu wasemaji wazuri na wahubiri wenye kustahili.” Shule inaendelea kutoa mazoezi imara, ambayo sisi sote tunahitaji.

2 Usomaji wa Biblia: Wale wanaotoa hotuba mbalimbali si wao tu wanaofaidika na shule. Jambo la hakika ni kwamba sisi sote tunapewa mgawo: Usomaji wa Biblia wa kila juma. Programu ya shule yaonyesha sura gani inatupasa kusoma kila juma. Maandiko yanayo vikumbusho vingi ambavyo hukazia ulazima wa kusoma Biblia kila juma. (Yos. 1:8; Zab. 1:2 ; Mdo. 17:11) Usomaji huo ni wa lazima sana kwa afya yetu nzuri ya kiroho ; unalisha akili na moyo. Kwa kusoma Biblia dakika 5 hivi kila siku, tunaweza kufuata programu ya kila juma. Mwishoni mwa mwaka, tutakuwa tumesoma zaidi ya sura 150 ya Neno la Mungu. Tukiwa na Biblia karibu, itawezekana kwetu kusoma sehemu ndogo yayo kila siku.

3 Hotuba ya Maagizo: Ili kuwachochea ndugu na dada kumtumikia Yehova kwa uaminifu na bidii, msemaji anayetolea hotuba ya maagizo anapaswa kuwa mfundishaji mzuri, anayewezesha wanaomsikiliza kutia moyoni maana ya habari zinazochunguzwa na kuwafanya wakuze shukrani kwa Yehova, Neno lake na tengenezo lake. Wazee na watumishi wa huduma watafikia lengo hilo kwa kujitayarisha vizuri, kwa kufanya hotuba zao ziambatane na kichwa cha habari, kwa kusema kwa usadikisho na pia kwa kufanya habari ziwe hai. (Héb. 4:12) Ni jambo la lazima kwamba msemaji aheshimu wakati aliopewa. Kitabu “Kila Andiko” kinajaa na marejezeo mengi ya Biblia na pia kinaelezea maandiko fulani yenye kuvutia, ambayo tunaweza kufaidika nayo kiroho. Kitabu Prédicateurs kinaeleza historia ya tengenezo linaloonekana la Yehova na pia kinazungumzia mambo yaliyopata kutukia katika maisha ya watu halisi walioonyesha imani, bidii, kujitoa na pia upendo. Tuna mengi ya kujifunza kuhusu mwongozo wetu wa kitheokrasi wa wakati uliopita na pia juu ya namna Yehova anavyobariki watu wake wa wakati wetu.

4 Mambo Makuu Kutokana na Usomaji wa Biblia: Ndugu wanaopewa mgawo huo wanapaswa kuchagua mistari inayotoa habari kamili, ambayo wataweza kuonyesha matumizi yayo kwa kutaniko. Kwa hiyo ni jambo la maana kwamba wasome sura zote zilizopangiwa, watafakari juu yazo na pia wafanye utafiti juu ya mistari iliyochaguliwa ili kupata maelezo yatakayofafanua maana. Mwishoni mwa Index des publications de la Société Watch Tower, kunayo “Index biblique,” ambayo huenda ikawa ya lazima sana tunapofanya utafiti wa habari kuhusu andiko fulani. Ndugu wanaotoa kipindi hiki wangepaswa kuonyesha busara nzuri na pia kuepuka kuzungumzia nukta zisizokuwa na uhusiano na habari zinazochunguzwa. Hawangepaswa kutayarisha maelezo mengi zaidi ambayo haiwezikani kuyatoa katika muda wa dakika sita.

5 Kila mmoja wetu anaweza kufaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Inaweza kutusaidia kutengeneza vizuri uwezo wetu mbalimbali wa wasemaji na wafundishaji. Kufaidika kikamilifu na mpango huo kutatusaidia bila shaka kufanya ‘maendeleo yetu yaonekane wazi kwa watu wote.’—1 Tim. 4:15.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine