Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea mnamo Septemba: Broshua ya kurasa 32 kati ya zifuatazo: Je! Kweli Mungu Anatujali?; Je! Uamini Utatu; Serikali Itakayoleta Paradiso; Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa; Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? Kuishi Milele Duniani Katika Furaha; “Tazama! Mimi Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya.” Ikiwa hali itaruhusu, tutaweza kutolea broshua: Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?; Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli?; Nos problèmes — Qui nous aidera à les résoudre? Oktoba: La vie: comment est-elle apparue? Évolution ou création? Makutaniko yaliyo nacho katika stoki yataweza pia kutolea vitabu: Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani au Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha. Novemba: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ikiwa mtu fulani anaonyesha kupendezwa wakati wa ziara za kurudia, itawezekana kumtolea uandikisho. Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Tutafanya bidii ya pekee ili kurudi kuwaona wale wote waliokubali kitabu, tukiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia.
◼ Kila kutaniko litapokea fomu kwa ajili ya mwaka wa utumishi 1997. Tafadhali zitumieni kwa utambuzi. Zitawekwa kwa ajili ya matumizi tu ambayo zilikusudiwa.
◼ Je! mmekwisha kutuma fomu ya hesabu ya vichapo (S-18)? Tunawakumbusha kwamba inapaswa kutumwa kwenye afisi mapema ikiwa ni nyuma Septemba 6. Lindeni nakala ya pili katika faili zenu. Nakala ya tatu itatumiwa kama karatasi ya kazi. Mwandishi atasimamia hesabu, na fomu yenye kujazwa vizuri itachunguzwa na mwangalizi-msimamizi. Mwandishi na mwangalizi-msimamizi wataitia sahihi.
◼ Makutaniko yataanza kuomba Kalenda ya Mashahidi wa Yehova 1997 juu ya maombi yayo ya vichapo ya Septemba.