Majibu Kwa Maulizo Yenu
◼ Tunapaswa kufikiria nini tunaposoma mafungu kwenye mikutano?
Sehemu kubwa ya wakati unaopangwa kwa ajili ya funzo la Mnara wa Mlinzi na funzo la kitabu unatolewa kwa usomaji wa mafungu. Hilo humaanisha kwamba msomaji ana daraka kubwa la lazima kuhusiana na mafundisho. Anapaswa kusoma kwa namna ya ‘kutoa maana’ ya habari ili kwamba wasikilizaji waelewe, lakini pia wapate kusukumwa kutenda. (Neh. 8:8) Ni kwa sababu hiyo msomaji anapaswa kujitayarisha vizuri. (1 Tim. 4:13; ona somo la 6 la Kiongozi cha Shule.) Zifuatazo ni nukta za lazima kwa usomaji mzuri wa watu wote.
Kuonyesha Mkazo Unaofaa. Chagua mapema maneno au sentensi ambazo inafaa kukazia ili kuwezesha uelewevu sahihi.
Kutamka Maneno kwa Usahihi. Ni jambo la lazima kusema vizuri na kutamka ili kwamba wasikilizaji waelewe misemwa inayotumiwa katika vichapo. Tafuta katika kamusi maneno ambayo hauyajui au yanayotumiwa mara haba.
Kusema kwa Namna Yenye Kusikika na kwa Shauku. Kwa kusema kwa sauti kubwa na kwa shauku, utachochea kupendezwa kwa wasikilizaji, utaamsha hisia-moyo zao na utawahimiza.
Kusema kwa Shauku na kwa Sauti ya Mazungumzo. Kusema kama kawaida kunatokana na urahisi wa maneno. Kwa kujitayarisha na kwa kurudilia-rudilia, msomaji atakuwa mwenye starehe zaidi na hilo litafanya usomaji wake uwe wenye kuvutia badala ya kuwa wenye kuchosha na kuuzi.—Hab. 2:2.
Kusoma Yote Yanayoandikwa. Maneno yaliyo chini ya ukurasa na pia maelezo yanayopatikana kati ya vifungo vya mviringo au vifungo vya mraba kwa kawaida yanasomwa kwa sauti kubwa ikiwa yanaongeza kitu fulani kwa maandishi. Mitajo inayohakikisha tu chanzo cha habari peke yayo haisomwi. Maneno chini ya ukurasa yanapaswa kusomwa mahali ambapo yanayoonyeshwa katika fungu na kufanyiwa utangulizi huu: “Maneno chini ya ukurasa yanasema . . .” Baada ya kuyasoma, inatosha tu kuendelea na sehemu inayobaki ya fungu.
Usomaji mzuri wa peupe ni mojawapo ya njia za lazima ambazo kusudi ni ‘kufundisha wengine kushika mambo yote ambayo alituamuru’ Mwalimu wetu mkuu.—Mt. 28:20.