Matangazo
◼ Vitabu vya kutolea mnamo Desemba: Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Tutafanya bidii ya pekee ili kurudi kuwaona wale wote waliokubali kitabu, tukiwa na kusudi la kuanzisha mafunzo ya Biblia. Januari: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Februari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1984 kilicho katika stoki ya kutaniko. Makutaniko ambayo hayana vidhaa hivyo yatatolea Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Machi: La vie: comment est-elle apparue? Évolution ou création? au Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Tutaweza pia kutolea haidhuru kitabu gani cha kurasa 192 kilicho ndani ya stoki ya kutaniko.
◼ Makutaniko yaliyo na trakti Habari Njema za Ufalme Na. 34 yataweza kuwatia wahubiri moyo kuzitolea kwa namna ileile kama trakti nyingine, iwe nyumba kwa nyumba au kwa aina nyingine ya ushuhuda. Ikiwa inawezekana katika eneo lao, wahubiri wataacha labda nakala moja kwa kila mtu asiyekuwako, wakihakikisha kwamba trakti haionekani na wapita njia. Bidii ingepaswa kufanywa ili kugawa nakala zote zinazobaki za trakti hiyo iliyo na ujumbe wa maana.