Matangazo
◼ Vichapo vya kutolea katika Januari: Tafsiri ya Ulimwengu Mpya pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Februari: Kitabu chochote cha kurasa 192 kilichotangazwa kabla ya 1984 kinachopatikana katika stoki ya kutaniko. Makutaniko ambayo hayana vidhaa hivyo yatatolea Kuokolewa Kuingia Katika Dunia Mpya. Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili: Siri ya Furaha ya Familia.
◼ Makutaniko yatachukua mipango ifaayo kwa ajili ya Ukumbusho, ambao utaadhimishwa mwaka huu Siku ya Yenga Machi 23, kisha kutua kwa jua. Kwa kuwa hakuna mkutano mwingine wowote ambao utafanyika siku ile, isipokuwa mkutano kwa ajili ya mahubiri, mabadiliko ya lazima yangepaswa kufanyika ili kwamba funzo la Mnara wa Mlinzi lifanyike wakati mwingine. Wangalizi wa mzunguko wangepaswa pia kurekebisha programu yao juma hilo kulingana na hali za mahali. Ni vizuri zaidi kwamba makutaniko yaadhimishe kwa umbalimbali Ukumbusho, ingawa hilo haliwezekani sikuzote. Mahali ambapo makutaniko mengi yanaendesha mikutano yao katika Jumba la Ufalme lile lile moja, itawezekana labda kwamba moja au mengi kati yayo yatumie majengo mengine jioni hiyo. Ukumbusho haungepaswa kuanza nyuma kiasi cha kukasirisha watu wanaopendezwa na ukweli hivi karibuni. Zaidi ya hilo, haingefaa kwamba programu iwe karibu-karibu sana kiasi cha kukosa wakati wa kutosha wa kusalimiana na waalikwa kabla na kisha Ukumbusho, kuwatolea watu fulani msaada wa kiroho wenye kufuatiwa au kutiana moyo. Baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote yanayohusika, wazee wataamua yale yanayostahili kufanywa ili kuwezesha wote watakaokuja kwenye Ukumbusho kufaidika nao kikamilifu.
◼ Kwa sababu ya umuhimu wa tukio hilo, baraza la wazee lingepaswa kuchagua kama msemaji kwa ajili ya Ukumbusho mmoja wa wazee aliye na uwezo zaidi badala ya kuridhika kwa kutaja mtu fulani kwa kuachiana zamu au kwa kutumia ndugu yule yule kila mwaka.
◼ Katika 1998, Ukumbusho utaadhimishwa Siku ya Posho Aprili 11, kisha kutua kwa jua. Tarehe hiyo inatangazwa mapema ili kuwezesha kulinda au kukodisha majumba mahali ambapo makutaniko mengi yanatumia Jumba la Ufalme lile lile moja, jambo ambalo linawalazimisha kupata majengo mengine.
◼ Hotuba ya pekee inayopangwa katika kipindi cha Ukumbusho itatolewa Siku ya Yenga Aprili 6, 1997. Makutaniko yaliyo na ziara ya mwangalizi wa mzunguko, kusanyiko lao la mzunguko au kusanyiko lao la pekee la siku moja juma hilo yatasikiliza hotuba ya pekee juma lifuatalo. Hakuna kutaniko litakalopanga programu ya hotuba hiyo mbele ya Aprili 6.
◼ Vichapo vipya vinavyopatikana:
Pourquoi adorer Dieu en amour et en vérité? (broshua aina kubwa).
Mwimbieni Yehova Sifa— Lingala.
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo— Swahili.
◼ Kaseti mpya zinazopatikana:
Faisons ce qui est droit aux yeux de Dieu— Kifaransa (audio)
Jusqu’aux extrêmités de la terre— Kifaransa (vidéo)
Mélodies du Royaume (instrumentales)— Kifaransa
◼ Wakati wa mkutano wa utumishi wa Januari 6, inafaa kuweka tayari kwa ajili ya wahubiri wote wenye kubatizwa hati “Instructions médicales — Pas de sang” na kadi za utambulisho kwa ajili ya watoto.