Mikutano Ya Hali Ya Juu
1 Kama vile watumishi wa Mungu wa kale, Mashahidi wa Yehova wanakusanyika ili ‘kufundishwa na Yehova.’ (Is. 54:13) Wanakuwa wangalifu ili waweko kwenye mikutano, huku wakijua kwamba Yehova anawatolea chakula cha kiroho kwa wakati wenye kufaa kupitia Yesu Kristo na kwa njia ya kidunia ambayo anatumia, ni kusema “Mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” Mikutano hiyo inachukua nafasi ya maana ya wakati wetu. Tunataka hivyo kufanya kwamba iwe yenye manufaa zaidi, kwamba imtukuze Yehova na kuchangia kwa kuimarika kwa watu wake. Mashauri fulani au vikumbusho vinavyofuata vitatusaidia kufanya mikutano ya hali ya juu.
2 Mafundisho Wakati wa Mkutano wa Watu Wote: Msemaji atakuwa sikuzote mwangalifu ili kutumia maneno ambayo watu wanaokuja kwenye Jumba la Ufalme mara ya kwanza wanaelewa vizuri. Tunatamani kusaidia watu, na si kuwachekelea; hatupendi kuwadharaulisha, lakini kuchochea uwezo wao wa kufikiri na uamuzi wao nzuri. Kwa mfano, ikiwa hotuba inazungumzia kisio la mageuzi, msemaji hangepaswa kutoa mawazo yake kwa namna ya kuwachekelea wale wanaoamini nadharia (fundisho) hiyo. Kwa kupenda kufanya utoaji wa kuchekesha, hatutaweza kuamsha kupendezwa kokote kwa wale wanaoamini kisio la mageuzi.
3 Mafundisho Wakati wa Funzo la Mnara wa Mlinzi: Ndugu anayeongoza funzo ataepuka matangulizi marefu. Atasoma maulizo yanayohusiana na fungu na atatoa usemi kwa wahudhuriaji walioinua tu mkono kwa kadiri wakati unavyoruhusu. Atatia wahudhuriaji moyo kutoa maelezo mafupi na yanayolingana ili majibu mengi yapate kutolewa kwa kila ulizo. Atafanya kwamba hesabu kubwa zaidi iwezekanavyo ya wahudhuriaji waseme wakati wa funzo. Inawezekana kuwatia moyo watu wanyamavu kwa kuwachagua mbele ya wakati ili kusoma maandiko ya Biblia ambayo yataelezwa ikiwa wakati unaruhusu. Ndugu anayeongoza funzo ataweza mwenyewe kuongeza maelezo wakati wazo la lazima lilirukwa wakati wa uchunguzi wa fungu. Hangepaswa hata hivyo kufanya hilo pindi kwa pindi, na maelezo yake yatakuwa sikuzote mafupi sana.
4 Nukta kubwa za funzo zinalingana kwa kawaida na maulizo ya kisanduku yanayotumiwa kwa kujikumbusha. Itafaa kuangalia hivyo ili kujulisha nukta hizo kubwa wakati wa funzo.
5 Ikiwa funzo la Mnara wa Mlinzi linahusu uchunguzi wa andiko kwa andiko la sura fulani ya Biblia, ni jambo la muhimu kujulisha hilo mwanzoni mwa funzo. Katika hali hiyo, kwa kawaida ni jambo lenye manufaa sana kusomesha kila andiko, hata kabla ya kuuliza ulizo linalokusudiwa kwa fungu.
6 Kwa upande mwingine, iwe haidhuru ni habari gani inayochunguzwa, ndugu anayeongoza funzo ataalika wasikilizaji kuchukua Biblia ili kusoma maandiko ya lazima. Kwa uchunguzi unaosawazika wa habari, ataangalia ili kutokawia sana kwenye mafungu ya utangulizi, lakini atashikamana badala yake na habari ya makala ya funzo, iliyo na mawazo ya muhimu zaidi.
7 Kuhusu kushiriki kwa wasikilizaji, ndugu atatoa usemi kwa watoto kwa namna yenye akili na yenye kufaa. Haifai kwamba wapewe usemi kwa mfululizo kibinafsi inapohusu mafungu ya muhimu yanayoomba mafasirio yaliyo wazi na yenye kuchambua mambo kwa undani.
8 Mafundisho Wakati wa Mikutano ya Utumishi: Habari za kuchunguza kwa maulizo na majibu hazipaswi kufanyiwa utangulizi mrefu. Utangulizi mfupi sana unatosha. Maulizo yatakuwa wazi, kamili, ya moja kwa moja na yatalingana na yaliyomo katika mafungu. Kulingana na wakati uliopo, wakati mwingine ni jambo lenye kufaa kusomesha mafungu yaliyo ya muhimu ya sehemu inayochunguzwa. Ndugu anayeongoza mazungumzo atapendezwa na maneno ya muhimu ya maandiko ya Biblia yanayotajwa na atafanya matumizi yake kulingana na kichwa cha habari kinachozungumziwa. Kwa kutayarisha maonyesho, inafaa kujali mahitaji ya kutaniko na hali za kweli tunazokutana nazo katika mahubiri; inafaa pia kutayarisha vipingamizi vinavyotokezwa katika eneo na namna ya kushindana navyo. Vivyo hivyo, tutaweza kuonyesha jinsi ya kuitikia wakati vichapo vinapokataliwa. Maonyesho hayo yatakuwa ya hali zilizo za kweli. Katika hali zote, itafaa kuepuka zaidi maonyesho ya hali za kuwazia, ambayo si ukweli wa jinsi mambo yalivyo hakika.
9 Ikiwa washiriki wa kutaniko hawachukui uamuzi wa kutangaza habari njema kwa namna ya vivi hivi, wazee watachukua wakati, muda wa mkutano wa utumishi, kueleza mambo yaliyoonwa au kufanya maonyesho juu ya namna ya kutoa ushuhuda wa vivi hivi.
10 Ni “Matangazo” yanayohusu kutaniko peke yake ndiyo yangepaswa kusomwa, na “Habari za Kitheokrasi” zinaweza wakati mwingine kupambwa na mambo yaliyoonwa yanayotokana na Kitabu-Mwaka; nchi zinazojulikana kidogo zitaweza pia kuonyeshwa upande zinapopatikana kijeografia.
11 Ndugu anayeanza wa kwanza wakati wa mkutano wa utumishi hangepaswa kutakia wahudhuriaji ujio mwema, kwani tayari wamekwisha kutakiwa ujio mwema mbele, mwanzoni mwa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi (kwa kuwa yenyewe ndiyo inayoanza).
12 Barua za Sosaiti zinazotumwa kwa ukawaida kwenye makutaniko zingepaswa kusomwa kwa shauku na kwa uzito. Kwa sababu ya umuhimu wazo, ni vizuri zaidi, awe ni mzee, atakayefanya usomaji; ataweza kimbele kupiga mistari maneno ya muhimu na mawazo ya lazima ya barua. Wakati mwingine, itakuwa lazima kukazia mawazo makubwa ya barua kwa kuyarudilia.
13 Mafundisho Wakati wa Ukumbusho: Hotuba ya Ukumbusho haingepaswa kutolewa kwa wasemaji kwa kuachiana zamu, kwa kusudi la kuifanya itolewe na wazee wote. Kwa kuona umuhimu wa mkutano huo wa pekee, ni peke yake mwalimu au walimu bora wa kutaniko watakaotoa hotuba ya Ukumbusho, hata ikiwa wamekwisha kuitoa wakati uliopita. Tutatumia maneno mepesi, yanayoeleweka na wasikilizaji wanaokuja kwa mara ya kwanza katika Jumba la Ufalme. Makutaniko yasiyo kuwa mbali na Betheli yanaweza kuomba Sosaiti iwatumie msemaji. Vivyo hivyo, ikiwa mwangalizi wa mzunguko au wa wilaya wanalitembelea kutaniko, lingekuwa jambo lenye kufaa kuwatumia ili kutoa hotuba ya Ukumbusho, katika kutaniko linalotembelewa au katika kutaniko linalopatikana kando kando.
14 Mashauri Fulani kwa Ujumla: Kuhusu wimbo, tunakumbusha kwamba ni vizuri kuonyesha kichwa cha wimbo na andiko la Biblia juu yake wimbo unategemea. Ni vizuri bila shaka kwamba wahudhuriaji waimbe kwa moyo wao wote. Ndugu anayesimamia vikuza-sauti atahakikisha kwamba sauti ya muziki iliyorekodiwa ni ya kutosha, kwani inafikia wakati fulani kwamba sauti ya wahudhuriaji inafunika muziki. Hilo ni hatari ikiwa ni wimbo ambao muziki unajulikana kidogo na wahudhuriaji.
15 Wakati watu wanapoingia mara ya kwanza katika Jumba la Ufalme, inafaa kuwapokea kwa shauku. Wahudhuriaji hawatakazia macho wapya hao, hata ikiwa wanasema au wanavaa kwa namna isiyo ya kawaida. Watu wa kila aina wanaweza kupendezwa na mikutano yetu. Mahali petu pa ibada ni wazi kwa watu wote. Inawezekana kwamba wakuu wa polisi au wateule wa mtaa wanakuja kujionea jinsi mikutano yetu inavyoendeshwa, na wote wanapaswa kujisikia kuwa wenye kukaribishwa vema.
16 Tutaepuka pia misemwa fulani yenye makosa wakati tunapojielekeza kwa akina ndugu na dada wa kutaniko. Tazama mojawapo ya misemwa hiyo:
— Si jambo lenye kufaa kusema kwamba ‘le frère Untel prononcera la prière’ au kwamba ‘la sœur Unetelle présentera tel exposé’. Maneno ‘ndugu’ au ‘dada’ hayapaswi kutanguliwa na sarufi ya Kifaransa le au la. Ni jambo lenye kufaa kusema: ‘Frère Untel prononcera la prière’ au ‘Sœur Unetelle présentera l’exprosé suivant.’
— Tunasikia mara nyingi watu wakisema: “Ndugu Fulani atatuhudumia kwa sala.” Si sahihi katika Kiswahili. Badala yake ni vizuri kusema: “Ndugu Fulani atatoa (au atafanya) sala.” Vivyo hivyo, tuepuke kusema: “Kupitia sala hii.” Tuseme badala yake kwamba “mkutano unawekwa chini ya uongozi wa roho takatifu” au kwamba “uamuzi ulichukuliwa katika sala.”
— Badala ya kusema “wema usiyostahiliwa wa Yehova,” ni sahihi na jambo linalopatana na Biblia kusema “fadhili isiyostahiliwa.”
— Tutajilinda pia na makosa ya kuunganisha maneno, kama lile la kawaida (katika Kifaransa), ambalo linahusu kuongeza kimakosa ‘t’ kwa aina ya tatu ya upekee ya viarifa (verbes) fulani. Kwa mfano, “il va-t-être”; ni vizuri kusema “il va être”.
17 Haiombi, katika hali hizo tofauti, kuwa mwenye kushikilia mambo kwa ukakamavu wala kuanzisha mabishano ikiwa makosa fulani yanarudiliwa. Hayo ni mawazo tu tunayoonyesha yatakayotuwezesha hata hivyo kusema kwa usahihi, jambo ambalo litachangia kwa ubora wa mikutano yetu.
18 Umetambua hakika kwamba mojawapo ya mashauri yaliyo hapo juu yanahusu zaidi hali si undani wa mambo; kwa namna nyingine, yanazungumzia hasa utoaji wa mikutano au wa vipindi. Yanaweza kuonekana machoni pako kama mambo madogo madogo, lakini hata hivyo yana umuhimu wayo ikiwa tunataka kwamba mikutano yetu iwe yenye kuelimisha na ya hali ya juu. Ikiwa tunatambua ulazima wa kuangalia kila mara kuboresha mikutano, itamtukuza kikamilifu Yehova. Washiriki wote wa kutaniko wataingojea kwa shangwe, wakijua kwamba itawajenga na kuwatia moyo kiroho. Tujikaze sote kufanya kila mara mikutano ya hali ya juu!