Matangazo
◼ Vitabu vya kutolea mnamo Machi: Ufunuo—Upeo Wao Mtukufu U Karibu! Aprili na Mei: Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Juni: Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Mnamo juma na katika maeneo yanayotembelewa mara kwa mara, tutaweza kutumia broshua mpya Mungu Anataka Nini Kwetu?
◼ Afisi ilituma kwa kila kutaniko furushi la fomu ili kutosheleza mahitaji ya mwaka mzima. Tunawaomba kuzitumia tu kwa ajili ya kazi ambayo zinakusudiwa na si kwa matumizi ya binafsi.
◼ Wahubiri wanaotaka kuwa mapainia wasaidizi mnamo (mwezi huu) wa Machi na mnamo Mei wangepaswa kupanga mambo yao tangu sasa na kujaza maombi yao mapema vya kutosha. Hilo litasaidia wazee kuchukua hatua za lazima kwa ajili ya mahubiri na kutayarisha stoki ya kutosha ya magazeti na vichapo vingine. Majina ya wale wote ambao ombi liliweza kukubaliwa yatatangazwa kutanikoni.
◼ Tunaendelea na toleo la pekee la kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha katika lugha zote ambamo kinapatikana kwa bei inayoonyeshwa katika barua ya Sosaiti.