Habari Za Kitheokrasi
Burundi: Ijapokuwa hali yenye msukosuko na kuripuka kwa mitego ya kuharibu vifaru (mines antichars), makusanyiko mawili ya mzunguko yalifanyika mnamo Machi na Aprili. Pa Nyabihanga, nchini, hudhurio lilikuwa la watu 830 na 32 walibatizwa. Katika mji mkuu, Bujumbura, hudhurio lilifikia watu 2,103; wapya 60 walijitoa wakfu kwa Yehova kwa njia ya ubatizo!