Mikutano Ya Utumishi Ya Januari
Juma Toka Januari 5
Wimbo 57
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa ya Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 15: “Tuseme Juu ya Yehova Kila Siku.” Kwa maulizo na majibu. Wakati wa uchunguzi wa fungu 4, toa maelezo kutokana na somo 16 la kitabu Kiongozi cha Shule, maf. 14-16.
Dak. 20: “Biblia: Kiongozi Kilichotolewa na Mungu kwa Watu Wote.” Mzee mmoja anachunguza makala pia na sababu ambazo zingepaswa kusukuma kila mmoja aichunguze Biblia. (Ona broshua Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, maf. 30, 32.) Hoji kwa kifupi wahubiri wawili watakaofasiria namna wanavyojitayarisha kutumikisha madokezo ya maf. 3-8. Fanyeni onyesho moja linalotegemea moja la mafungu hayo ili kuonyesha mazungumzo ya kwanza, na onyesho lingine kwa ajili ya ziara ya kurudia.
Wimbo 165 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 12
Wimbo 58
Dak. 10: Matangazo. Hali ya akaunti.
Dak. 20: Kwa Nini Kufunua Lililo Ovu? Hotuba itakayotolewa na mzee na itakayotegemea Mnara wa Mlinzi wa Agosti 15, 1997, kur. 26-30.
Dak. 15: “Kutokuwako Kwako Hakukosi Kutambuliwa!” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji, yakiongozwa na mzee. Sema ni watu ngapi wanaohudhuria kwa wastani kwenye mikutano ya kutaniko. Alika ndugu na dada fulani wafasirie sababu kwa nini kukusanyika kwenye jumba la Ufalme kunawatia nguvu mpya.
Wimbo 172 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 19
Wimbo 63
Dak. 5: Matangazo.
Dak. 15: Mahitaji ya Kutaniko.
Dak. 25: “Tungepaswa Kuwa Walimu, Si Wahubiri Tu.” Kwa maulizo na majibu. Wakati wa uchunguzi wa fungu 11, someni fungu 11 la somo 15 katika kitabu Kiongozi cha Shule.
Wimbo 174 na sala ya mwisho.
Juma Toka Januari 26
Wimbo 138
Dak. 8: Matangazo. Kumbusha wahubiri kuleta nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya februari 1998 kwa ajili ya mkutano wa juma lijalo.
Dak. 17: “Shule ya Huduma ya Kitheokrasi Katika 1998.” Hotuba itakayotolewa na mwangalizi wa Shule. Fasiria namna gani kila mmoja anaweza kufaidika zaidi tena na Shule katika mwaka huu. Tia kila mmoja moyo kufuata “Programu ya ziada ya usomaji wa Biblia.”
Dak. 20: Tuhubiri Habari Njema Kila Mahali. Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakitegemea kitabu Huduma Yetu, kur. 92-7, kwa msaada ya maswali yafuatayo: (1) Kwa nini matumizi ya vichapo vyetu ni yenye matokeo katika kutangaza habari njema? Kwa nini tungepaswa kuvitolea kila wakati? (2) Kwa nini tunapaswa kujikaza kutoa ushuhuda kwa namna ya vivi hivi? Ni nini baadhi ya njia za kufanya hivyo? (Alika wahubiri kuripoti mambo yaliyoonwa kuhusiana na ushuhuda wa vivi hivi.) (3) Kwa nini kutaniko linapaswa kujitoa kutembelea eneo lote lililogawiwa? Mahali ambapo kazi haikosekani, kwa nini ni jambo lenye manufaa mtu kuwa na eneo lake mwenyewe? (4) Ni nini manufaa ya mipango inayochukuliwa ili kuhubiri katika kikundi? Tunawezaje kupanga utendaji wetu wa kuhubiri ili kufanya matumizi bora ya wakati wetu?
Wimbo 222 na sala ya mwisho.