Habari Za Kitheokrasi
◼ Benin, Kamerun, Côte d’Ivoire, Ghana, Liberia na Nigeria, nchi zipatikanazo katika Afrika ya Magharibi, zimeripoti zote vilele vipya katika hesabu ya wahubiri mnamo Februari.
◼ Wakimbizi wengi hurudi Liberia ambako njaa halisi ya kweli hutawala. Mnamo Februari, kilele cha wahubiri 2 286 waliripoti mafunzo ya Biblia 6 277.
◼ Huko Macao, hesabu ya wahubiri iliongezeka kwa asilimia 16 kwa kulinganisha na wastani wa mwaka uliopita, kukiwa watu 135 waliotoa ripoti ya utumishi mnamo Februari.
◼ Fidji, visiwa vya Solomon na Tahiti, katika Pasifiki ya Kusini, vilifikia vipeo vipya katika hesabu ya wahubiri mnamo Februari.
◼ Huko Madagaska, hesabu ya juu sana ya wahubiri 9 484 ilifikiwa, hiyo ikimaanisha ongezeko la asilimia 14 kwa kulinganisha na wastani wa mwaka uliopita. Mnamo Februari, zaidi ya mafunzo ya Biblia 20 000 yaliongozwa vile vile.