Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/98 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Ya Novemba

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mikutano Ya Utumishi Ya Novemba
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 11/98 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Ya Novemba

Juma Toka Novemba 2

Wimbo 38

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochaguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme. Toa maelezo juu ya ripoti ya utumishi wa shambani wa Agosti katika nchi na katika kutaniko lenu.

Dak. 15: “Inafaa Wote ‘Wakubali Neno kwa Ukunjufu wa Moyo’!” Vérifier titreKwa maulizo na majibu. Toa pia madokezo kutoka nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996, fungu 21.

Dak. 20: “Nataka Funzo la Biblia!” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji yakiongozwa na mwangalizi wa utumishi. Fasiria jinsi, katika kutaniko, watajitia katika kufanya ziara za kurudia. Kadiri iwezekanavyo, wahubiri wenye ustadi watasaidia wapya. Wale wanaotembea katika gari moja wataangalia wasiwe wengi, jambo litakalofanya iwezekane kwao kufanya ziara za kurudia nyingi. Rudilieni madokezo yaliyotolewa katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mei 1998, mafungu 12-15. Onyesho: mhubiri mwenye uwezo anapendekeza funzo wakati wa ziara ya kurudia. Tia moyo kila mmoja ajitahidi kuanzisha funzo la Biblia.

Wimbo 35 na sala ya mwisho.

Juma Toka Novemba 9

Wimbo 187

Dak. 13: Matangazo. Hali ya akaunti. Majibu kwa Maulizo Yenu.

Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko.

Dak. 17: “Tujengane kwa Kutoa Maelezo Kwenye Mikutano.” Kwa maulizo na majibu. Fasiria namna kutoa maelezo kunavyotusaidia tufanye maendeleo kiroho. (Ona Kiongozi cha Shule, somo 38, fungu 4.) Omba baadhi ya wahudhuriaji waseme jinsi walivyoshinda ukosefu wa shauku ya kutoa maelezo kwenye mikutano na faida wanazopata kutokana na jambo hilo.

Wimbo 51 na sala ya mwisho.

Juma Toka Novemba 16

Wimbo 182

Dak. 8: Matangazo. Tangazeni mipango ya pekee iliyofanywa kwa ajili ya mahubiri mwisho-juma. Adaptation RDC

Dak. 20: “Waangalizi Wanaoongoza​—Mwangalizi wa Shule ya Huduma ya Kitheokrasi.” Hotuba inayotolewa na mwangalizi wa shule. Rudilieni Kiongozi cha Shule, kurasa 10-11, mafungu 6-​12.

Dak. 17: See E“Tuwe Wenye Matokeo Katika Huduma Yetu.” Vérifier titre Mazungumzo kwa maulizo na majibu ya mafungu 1-7 ya nyongeza. Tia mkazo juu ya mawazo yanayotumika kipekee katika eneo la kutaniko lenu.

Wimbo 167 na sala ya mwisho.

Juma Toka Novemba 23

Wimbo 89

Dak. 8: Matangazo. See EEleza mambo yaliyoonwa yanayoandikwa kwenye ukurasa wa mwisho wa Amkeni! ya Agosti 8, 1998 kuhusu jinsi kitabu Yule Mtu Mkuu kilivyogusa moyo wa watu. Wahubiri wangepaswa kuvizia nafasi za kutolea kitabu hicho.

Dak. 17: See E“Tuwe Wenye Matokeo Katika Huduma Yetu.” Vérifier titreMazungumzo kwa maulizo na majibu ya mafungu 8-21 ya nyongeza. Kazia nukta zinazohusu eneo la kutaniko lenu.

Dak. 20: Mapendekezo ya Kufanya Usomaji Wako wa Biblia Uwe Bora. Hotuba iliyo na msingi juu ya Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1995, kurasa 16-​17. Tia mkazo juu ya faida zinazotokana na usomaji wa Biblia wa kila siku. Toa kifupi cha mapendekezo yaliyofanywa na useme jinsi ya kuyatumia. Wahubiri wawili au watatu wanasema jinsi wanavyofaidika na usomaji wa kila siku wa Neno la Mungu.

Wimbo 46 na sala ya mwisho.

Juma Toka Novemba 30

Wimbo 64

Dak. 15: Matangazo. Kumbusha wote watoe ripoti yao ya utumishi. Tia moyo wale ambao hawakuanzisha funzo la Biblia mnamo Novemba waendeleze jitihada zao mnamo Desemba, kwa kuwa tutatolea kitabu Ujuzi na Tafsiri ya Ulimwengu Mpya. Katika onyesho, mhubiri mwenye uwezo anatumia kisanduku kwenye ukurasa 19 wa kitabu Ujuzi, na anaonyesha jinsi ya kutumia kitabu hicho ili kujua mafundisho ya Biblia; anaanzisha funzo.

Dak. 15: Tutumie Vema Kalenda ya Mashahidi wa Yehova ya 1999. Hotuba. Sema juu ya mambo yanayopatikana katika kalenda: (1) picha zenye kugusa moyo zinazoonyesha matukio na mafundisho ya maana ya Biblia; (2) programu ya usomaji wa Biblia wa kila juma kwa ajili ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi; (3) programu ya usomaji wa Biblia kwa ajili ya Ukumbusho; (4) tangazo la kujikumbusha kwa kuandika kunakokaribia; (5) vikumbusha kwa ajili ya kushiriki kikawaida katika ugawaji wa magazeti. Sema namna ya kutumia nafasi zinazoachwa wazi: kuandika programu yetu ya mahubiri, kuandika wakati tuliopitisha katika mahubiri na mikutano kwa ajili ya mahubiri, vipindi tunavyogawiwa, ziara ya mwangalizi wa mzunguko na mikusanyiko ya karibuni. Kwa kuweka kalenda mahali penye kuonekana nyumbani au mahali petu pa kazi, tunaweza kutokeza nafasi za mazungumzo ya kibiblia. Sema mambo yaliyoonwa yanayoelezwa katika Kitabu-Mwaka 1988, ukurasa 8.

Dak. 15: Tufaidike na Broshua Mpya Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa? Toa kifupi cha nukta kubwa za broshua hiyo. Inaonyesha vyanzo vya imani katika kutoweza kufa kwa nafsi na inafunua jinsi imani hiyo ilivyokuja kuwa ya msingi katika karibu dini zote za ulimwengu. Inaonyesha kwa njia yenye kuvutia yale ambayo Bibla husema kuhusu nafsi, sababu ya sisi kufa, hali ya wafu, tumaini la uhai baada ya kifo na sababu kwa nini tunapaswa kujua kweli kuhusu maswali hayo. Kila mtu angepaswa kusoma broshua hiyo. Onyesha baadhi ya zile picha zake 40, na pia mitajo inayopatikana mwanzoni mwa kila sehemu ambavyo tunaweza kuvitumia ili kuamsha kupendezwa kwa watu. Onyesha jinsi ya kupendekeza funzo la Biblia kwa kutumia sehemu ya mwisho. Alika wahubiri fulani waseme jinsi wanavyofikiria kutumia broshua hiyo katika mahubiri.

Wimbo 121 na sala ya mwisho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine