Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/00 uku. 2-3
  • Matangazo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Matangazo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 6/00 uku. 2-3

Matangazo

◼ Toleo la vichapo la Juni: Mungu Anataka Nini Kwetu? Kazeni fikira juu ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Julai na Agosti: Yoyote kati ya broshua zifuatazo zenye kurasa 32 inaweza kutumiwa: Jambo Gani Hutufikia Tunapokufa?, Je! Kweli Mungu Anatujali?, Je! Uamini Utatu?, Jina la Mungu Litakaloendelea Milele, Kuishi Milele Duniani Katika Furaha!, Mtu Fulani Umpendaye Anapokufa, Ni Nini Lililo Kusudi la Uhai—Wewe Waweza Kulipataje? na Serikali Itakayoleta Paradiso. Broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote?, Kitabu kwa Ajili ya Watu Wote, Nos problèmes — Qui nous aidera à les résoudre? na Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je! Ziko Kweli? zinaweza kutolewa inapofaa. Septemba: La vie: Comment est-elle apparue? Évolution ou création?

◼ Tunaomba makutaniko yote yenye kuongoza yaandike sikuzote ‘Lenye Kuongoza’ juu ya maombi yao ya vichapo (S-14).

◼ Ili kila mhubiri awe na gazeti lake, tulirekebisha kikamili maombi kusudi hilo liwezekane katika makutaniko yote kuanzia Januari 1, 2000. Hata hivyo, tunapokea maombi mengi ya makutaniko yanayotaka kuongeza vya kutosha hesabu yayo ya magazeti. Makutaniko fulani yanataka sasa kuzidisha mara mbili, au hata mara tatu kiasi chayo. Tunawajulisha kwamba kuongeza maombi ya magazeti kutafanywa hatua kwa hatua. Ikiwa kuna maongezeko makubwa ya wingi wa magazeti, hayo yatarekebishwa na ofisi. Ikiwa kutaniko lina sababu nzuri ya kuongeza vya kutosha ombi lake la magazeti, litajulisha jambo hilo kupitia barua.

◼ Tunawajulisha kwamba, ili kurahisisha mambo na kulinda fedha, hatutatoa tena magazeti yanayofanyiwa andikisho, isipokuwa andikisho kwa magazeti katika lugha isiyozungumzwa katika eneo. Wengi wa watu wanaotamani kupokea magazeti yetu kwa ukawaida ni wanafunzi wa Biblia na labda watu wanaohudhuria mikutano ya kutaniko. Ikiwa mtu fulani anataka kupokea kwa ukawaida magazeti yetu, fanyeni nguvu ili kuhakikisha ikiwa anaonyesha kupendezwa kwa unyofu kwelikweli. Ikiwa ni hivyo, mtaamua labda kuingiza mtu huyo katika njia yenu ya magazeti, jambo litakalofanya iwezekane kukomaza kupendezwa kwake. Tunawakumbusha kwamba wahubiri wote wanapaswa kupokea magazeti yao kwenye meza ya vichapo ya kutaniko lao.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine