Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/00 uku. 4
  • Je, wewe unathamini uvumilivu wa Yehova?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, wewe unathamini uvumilivu wa Yehova?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uvumilivu wa Yehova na Yesu Unatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Muendelee Kuwa na Uvumilivu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Katika Kazi Yetu ya Kuhubiri—Tunapaswa Kuonyesha Uvumilivu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Uvumilivu​—Onyesha Sifa Hii na Uko na Tumaini
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 7/00 uku. 4

Je, wewe unathamini uvumilivu wa Yehova?

1 Ikiwa Yehova hangekuwa mvumilivu kwa miaka 10, 20, au zaidi iliyopita, akiruhusu ushahidi wenye kupanuka utolewe, je, ungeweza kupata kujifunza kweli? Sisi ni wenye shukrani kama nini kuona kwamba ameruhusu watu wengine wengi “wafikie toba.” Hata hivyo, siku kubwa ya Yehova ya hukumu “itakuja kama mwizi.” (2 Pet. 3:9, 10) Kwa hiyo, uvumilivu wa Yehova haupaswi kuonwa kimakosa kuwa kuchelewa katika kuleta mwisho wa mfumo huu wa mambo.—Hab. 2:3.

2 Hurumia watu: Uvumilivu wa Yehova unapita kwa mbali uelewevu wetu. Hatupaswi kusahau kusudi lake. (Yona 4:1-4, 11) Yehova anaona hali yenye kuhuzunisha ya wanadamu, naye ni mwenye huruma kwa ajili yao. Yesu anahisi vivyo hivyo. Kwa kuwa alihurumia makutano makubwa ya watu ambayo alihubiria, alitaka kazi ya kueneza evanjeli ipanuke ili watu wengi zaidi wapate nafasi ya kupata uzima wa milele.—Mt. 9:35-38.

3 Wakati mambo ya huzuni na misiba inapotokea, je, mioyo yetu haisikii huruma kuelekea wale wasiojua kweli? Watu leo ni kama “kondoo wasio na mchungaji” kadiri wanavyojaribu kukabiliana na kuelewa hali ya machafuko katika ulimwengu. (Mk. 6:34) Kwa kuhubiri kwa bidii habari njema, tunafariji wale walio na mwelekeo mzuri wa moyo na tunaonyesha uthamini wetu kwa uvumilivu wa Yehova.—Mdo. 13:48.

4 Kazi yetu ni ya haraka: Mwaka jana watu 323,439 walibatizwa, na zaidi ya 14,000,000 walihudhuria Ukumbusho. Kuna uwezekano kama nini kwa wengine wengi kuokoka uharibifu wa mfumo huu mbovu! Hatujui “umati mkubwa” utakuwa mkubwa kadiri gani. (Ufu. 7:9) Hatujui utume wetu wa kuhubiri utaendelea kwa wakati gani. Lakini Yehova anajua. Habari njema itahubiriwa mpaka atakapotosheka, “na ndipo mwisho utakapokuja.”—Mt. 24:14.

5 Wakati unaobaki umepunguzwa, nayo siku ya Mungu inakaribia. (1 Kor. 7:29a; Ebr. 10:37) Hakuna shaka kwamba “wokovu wetu uko karibu zaidi kuliko tulipopata kuwa waamini.” (Rom. 13:11) Acheni tusikose kusudi la uvumilivu wa Mungu. Badala yake, acheni tuhubiri kwa haraka ili wengi walio na tamaa ya uadilifu wapate rehema kubwa ya Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2026)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine