Uwe mtendaji mwenye furaha
1 Yesu alisema kwamba wakati wa kuwapo kwake, watu walio wengi sana ‘hawangejali,’ kama vile tu katika siku za Noa. (Mt. 24:37-39) Hivyo, inatazamiwa kwamba watu wengi hawatasikiliza habari njema ya Ufalme. Ni nini kinachoweza kutusaidia kuendeleza roho yenye shangwe kadiri tunavyotimiza huduma yetu?—Zab. 100:2.
2 Kwanza, tunahitaji kulinda akilini kwamba ujumbe wetu na utume wetu wa kuhubiri vinatoka kwa Mungu. Kutoitikia kokote katika huduma, ijapokuwa jitihada zetu bora zaidi, ni kumkataa Yehova kwelikweli. Kukumbuka kwamba uaminifu wetu katika kuhubiri una upendeleo wake kutatusaidia tuendeleze shangwe yetu na furaha yetu ya ndani tukiwa watendaji wa neno la Mungu.—Yak. 1:25.
3 Pili, bado kuna watu watakaokubali njia ya Yehova ya wokovu. Ingawa watu walio wengi wanaweza kuwa wasiojali, kuna wale wenye mfano wa kondoo ambao bado wanapaswa kukusanywa, hata wakati huu wa mwisho kabisa. Tunahitaji kuendelea kuhubiri, tukienda “katika jiji lolote au kijiji chochote” ili ‘kutafuta kabisa ni nani humo anayestahili.’—Mt. 10:11-13.
4 Endeleeni kuwa na mtazamo wenye kufaa: Yale mambo mabaya yaliyotendwa na dini isiyo ya kweli yamefanya wengine wasiwe tena wenye kudanganywa. Wengine ‘wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku’ na mfumo huu wa mambo. (Mt. 9:36) Huenda wengi wakawa wenye kulemewa sana na ukosefu wao wa kazi, wa matunzo ya kiafya, na wa usalama. Kuelewa hilo kutatusaidia tuendelee kwa bidii katika kazi yetu. Jitahidini kuanzisha mazungumzo yenye kuhusu maswala yanayohangaisha zaidi watu katika eneo letu. Wasaidieni waone kwamba Ufalme wa Mungu ndilo suluhisho pekee. Tumieni Maandiko na nukta fulani katika vichapo ili kufanya habari njema iguse mioyo yao.—Ebr. 4:12.
5 Watendaji wenye furaha wa neno la Mungu hukumbuka sikuzote kwamba “furaha ya BWANA ni nguvu [yetu].” (Neh. 8:10) Hakuna uhitaji wa kupoteza shangwe yetu. “Nyumba ikistahili, salama yenu iifikilie; lakini kama haistahili, salama yenu irudi kwenu.” (Mt. 10:13, ZSB) Yehova hufanya upya shangwe na nguvu yetu kadiri tunavyovumilia kwa utulivu katika utumishi wake mtakatifu, naye hubariki uaminifu wetu.